Skip to main content

Posts

Showing posts from October 23, 2022

VIFARANGA VYA SAMAKI VYAWACHELEWESHEA WAFUGAJI PEMBA NDOTO ZA UCHUMI WA BULUU

  NA HANIFA SALIM, PEMBA UCHUMI wa buluu ni shughuli za kiuchumi zinazohusu matumizi bora ya rasilimali za bahari kwa ajili ya kuimarisha au kukuza pato la wavuvi na taifa. Kuna nafasi kubwa na nzuri ya kuifanya Zanzibar na Tanzania kwa ujumla kuwa na uchumi mzuri zaidi kwa kuifanyia maarifa zaidi ‘ Blue Economy’ .   Elimu na mafunzo katika uchumi buluu inapaswa kuratibiwa vizuri ili kukuza ukuaji wa sekta ya bahari, kwa hivyo unaweza kutoa moja ya fursa kubwa zaidi kwa mafanikio ya biashara. Sio kitu cha ajabu kwa Zanzibar kusikia neno uchumi wa buluu, ambapo ikiwa na maana kuwa ni shughuli zote za uendelezaji na ukuzaji wa uchumi kupitia matumizi bora ya rasilimali zote muhimu za bahari. Dhana nzima ya uchumi wa buluu ni pana, ambayo imebeba shughuli zote za msingi zinazofanywa katika bahari kama vile, uvuvi wa aina mbali mbali ikiwemo raslimali zote zitokanazo na bahari. Ikiwemo uvuvi wa kibiashara na usio wa kibiashara katika kina kirefu na kifupi cha maji, shughul

CCM MKOANI CHATOA MKONO WA POLE KIFO CHA KADA WAO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:: CHAMA cha Mapinduzi CCM wilaya ya Mkoani Pemba, kimeitaka familia ya mwanachama wao Omar Mohamed Hamad wa Chumbageni Wilayani humo, kuwa na moyo wa subra katika kipindi hiki kigumu. Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa CCM wilayani humo Ali Juma Nassor, wakati akizungumza na wanafamilia hao, kufuatia kifo cha mwanachama wao. Alisema, jambo hilo ni maandiko ya Muumba, hivyo ni vyema wawe wastahamilivu katika kipindi hiki kigumu, kwani suala la kuondokewa sio jambo jepesi. Aidha Katibu huyo alisema enzi za uhai wake, marehemu alikuwa mstari wa mbele katika ujenzi wa chama, hivyo mchango wake hautosahaulika daima. Alieleza kuwa, marehemu alikuwa karibu mno na chama, na maisha alikuwa hachoki kuendeleza mikakati na maono ya chama ili kuhakikisha kinasonga mbele. ‘’Kwanza tunawapa pole wanafamilia kwa kuondokewa na ndugu yenu ambae ni mwanachama wetu wa chama cha Mapinduzi, na endeleeni kumuombea,’’alishauri Katibu wa CCM jimbo la Chambani Amour Khei

RC KUSINI PEMBA AIKOLEZA 'SPEED' KAMATI MAANDALIZI SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA::: MKUU wa mkoa wa kusini Pemba, Mattar Zahor Massoud, amesema ana imani na kuiamini kamati maalum ya maandalizi ya kuelekea kilele cha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kisiwani Pemba.   Alisema, kamati hiyo imejipanga vyema na kutokana na shughuli ambazo wamezipanga kuzifanya zinaweza kuwa chanzo kizuri kwa kufikisha ujumbe kwa jamii husika.   Mkuu huyo wa mkoa ameyasema hayo mbele ya kamati hiyo ofisini kwake mjini Chake chake, wakati akizungumza na kamati hiyo, kuwasilisha mapendekezo ya shughuli zinazotarajiwa ndani ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.   Alisema, shughuli zilizopangwa ikiwa ni pamoja na matembezi, makongamano, elimu kwa jamii, vipindi vye redio na tv ni dhahiri kuwa elimu hiyo itasambaa na kuwafikia walengwa.   Alieleza kuwa, kamati hiyo imelenga hasa kule ambako serikali imekuwa ikitilia mkazo kila siku, juu ya elimu na kujadili changamoto katika kutokomeza matendo hayo kwa wanawake na watoto.   ‘’Kwanza ni

WAANDISHI PEMBA WAPEWA MBINU KUILINDA MITANDAO YAO

    AMINA AHMED MOH'D-PEMBA. Waandishi wa Habari Kisiwani Pemba wameaswa kuzidisha umakini katika utumiaji wa mitandao ya kijamii   ikiwa ni pamoja na kuweka ulinzi katika utumaji   wa taarifa zao ili zisiweze   kudukuliwa. Ushauri huo ulitolewa Oktoba 27, mwaka 2022 na   Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa Habari kisiwani Pemba (Pemba Press Club)   Bakar Mussa    Juma   alipokuwa akifungua mafunzo ya siku moja ya   Usalama wa Mitandao (Digital Security) kwa waandishi wa habari wanaotumia zaidi   mitandao ya kijamii    katika kazi zao   yaliofanyika   katika ukumbi wa   Ofisi hizo Misufini Chake Chake. Alisema    mitandao imekuwa ikipeleka ujumbe   kwa haraka   zaidi   kwa jamii    ukilinganisha na vyombo vyengine vya habari   vilivyopo nchini lakini kumekuwa na changamoto mbali mbali ambazo kama hawakuwa makini wanaweza kujiingiza katika matatizo wasio yategemea kwa vile kunaweza kukatokea wahalifu wakaharibu dhamira zao. Alieleza kuwa watumiaji wa mitandao wanawajibu wa

KILANGI: MCHAKATO MAREKEBISHO SERA YA MAJI WAIVA

NA SALMA LUSANGI:: KATIBU   Mkuu Wizara ya Maji, Nishati na Madini ( WMNM) Joseph Kilangi amesema Wizara yake ipo katika mchakato wa kuifanyia marekebisho sera ya maji ili iendane na wakati uliyopo sasa.     Akizungumza  katika kikao cha pamoja   nilichofanyika jana katika ofisi ya Mamlaka ya Maji safi na Mazingira Dodoma (DUWASA)  ambapo kikao hicho amekusudia kujitambulisha kwa viongozi wa Wizara ya Maji ya SMT baada ya uteuzi wa makatibu wa wakuu uliyofanyika June 30, 2022 .         Alisema wizara ya MNM inaendelea na kazi ya kupitia sera ya maji ili Sekta ya maji iweze kuleta tija kwa Serikali angalau wananchi wachangie huduma ya  maji.    Alifahamisha kwamba  lengo kuu, la wizara yake  kuwataka wananchi wachangie maji ni kuipunguzia Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ( SMZ) mzigo mkubwa wa kuendesha bure sekta hiyo kutokana gharama ziliyopo.   Katibu mkuu huyo alifafanua  kwamba gharama za kuendesha huduma ya maji ni kubwa ikiwemo, uchimbaji wa visima, ulazaji wa mabomba, ujenzi wa ma

ALIYEDAI KUBAKWA ASHINDWA KUFIKA MAHAKAMANI MARA 7 KUTOA USHAHIDI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:::: SHAHIDI nambari moja ambae ni mtoto wa miaka 13, aliyedai kubakwa, ameshindwa kufika mahakamani kutoa ushahidi, licha kuitwa na mahkama mara saba (7), na kisha mtuhumiwa kuachiwa huru.   Mtoto huyo pamoja na mama yake mzazi, walipelekewa wito ‘ samos ’ wa mahakama mara saba, kuanzisha Julai 22, na Septemba 21 mwaka huu, ili kufika mahakama ya makosa ya udhalilishaji kutoa ushahidi, lakini hawakufika.   Mwendesha mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa mashtaka Ali Amour Makame, aliimbia mahakama hiyo kuwa, mtoto aliyedai kubakwa anakua shahidi nambari moja kisheria.   Alidai kuwa, baada ya kumpata mtuhumiwa, walianza taratibu za kumuandikia muathirika ‘ shahidi nambari moja’ ili afike mahakamani yeye pamoja na mama yake, lakini hawakufika hata mara moja.   Wakili huyo wa serikali alidai kuwa, baada ya kuona mtuhumiwa anasota sana rumande na kesi hiyo kutokwenda, mbele, aliiomba mahakama kumuachia huru mtuhumiwa, ili akaendelee na shughuli z

WANANCHI PEMBA WAWAPA USHAURI WA BURE VIONGOZI WA UMMA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA WANANCHI kisiwani Pemba, wamewaomba viongozi wa ofisi za umma, kupunguza mikutano ya ndani ya nje ya ofisi, kwa siku ambazo wamezitenga wenyewe, kwa ajili ya kukutana na wananchi, kusikiliza malalamiko yao.   Walisema zipo ofisi za umma, zimejiwekea utaratibu wa kukutana na wananchi kila wiki mara moja au mbili, ingawa hata kwa siku hizo, imekuwa shida kuwapata.   Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, walipofika ofisini kulalamika, walisema viongozi wa ofisi za umma, wamejiwekea utaratibu wa kukutana nao, ingawa kwa baadhi yao imekuwa changamoto.   Mmoja kati ya wananchi hao Nassor Salim, alisema wamekuwa wakiitumia siku ya Jumanne na Alhamis, kumfuata mkuu wa wilaya ya Chake chake, ingwa changamoto ni mikutano isiyokwisha.   ‘’Wakati mwengine, anaingia kiongozi mwenzake anatumia zaidi ya saa mbili au tatu na sisi tunaendelea kusubiri bila ya kujua wakati gani tutampata,’’alieleza.   Nae Asha Issa Nassor, alisema tatizo hilo lilimkumba