Skip to main content

Posts

Showing posts from February 6, 2022

POLISI KASKAZINI PEMBA LAMDAKA KIJANA NA MISOKOTO 60 BANGI

  NA ZUHURA   JUMA, PEMBA JESHI la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba limemkamata kijana Hemed Omar Ali mwenye umri wa miaka 21 mkaazi wa Konde Chanjaani baada ya kupatikana na misokoto 60 ya dawa za kulevya aina ya bangi yakiwa nyumbani kwake. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba Juma Sadi Khamis alisema, mtuhumiwa huyo amekamatwa Febuari 6 mwaka huu majira ya saa 9:30 jioni huko nyumbani kwake Konde Chanjaani Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba alipatikana na misokoto 60 ya bangi. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Kamanda huyo alisema, mtuhumiwa huyo ni maarufu kwa uuzaji wa madawa ya kulevya, hivyo Jeshi la Polisi limemshikilia baada ya kufanya operesheni katika maendeleo mbali mbali ya Mkoa. “Pamoja na Jeshi la Polisi kufanya msako katika maeneo yote ya Mkoa, lakini walikuwa hawajafanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo, kwa bahati nzuri tulimkamata na tunaendelea mahojiano”, alieleza Kamanda huyo. Kamanda Sadi alieleza kuwa, upelelezi wa kesi hiyo unaendelea na

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

IRELAND YARIDHISHWA UTEKELEZAJI MRADI WA ARDHI PACSO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA NAIBU Balozi wa Ireland nchini Tanzania Mags Gaynor, ameridhishwa na utekelezaji wa mradi wa umiliki wa rasilimali ardhi kwa wanawake, uliokuwa ukitekelezwa na Mwemvuli wa asasi za kirais Pemba ‘PACSO’ na kumalizika hivi karibuni. Naibu Balozi huyo alisema, kutokana na majibu ya wanufaika wa mradi huo alivyozungumza nao, ameridhishwa na utekelezaji wa mradi huo, na hasa kwa kuwafikia walengwa. Alisema mradi huo ulilenga kuwafikia wanawake ili kuwajengea uwelewa, juu ya umilikiwa wa rasilimali ikiwemo ardhi, jambo ambalo sasa, limewanufaisha hasa kwa kuwepo wanufaika waliopata haki zao. Naibu Balozi huyo aliyasema hayo ofisi za PACSO Chake chake Pemba, kwenye kikao cha tathimi kilichojumuisha wanufaika wa mradi wa uongozi wa PACSO. Alieleza kuwa, kwa vile wapo wanawake kisiwani Pemba walionufaika moja kwa moja, ikiwa ni pamoja na kurithi, kununua ardhi na kulalamikia ucheleweshaji urithi ni hatua kubwa. “Serikali ya Ireland, imeridhishwa mno na mradi

WADAU WA ELIMU PEMBA: WATAKA SERA IJAYO YA ELIMU IKIREJESHEE HADHI CHUO CHA UALIMU NKURUMAH

  NA HAJI NASSOR, PEMBA WADAU wa elimu kisiwani Pemba, wamependekeza kua sera mpya ijayo ya elimu, ilazimishe kukirejeshea hadhi na uasili wake Chuo cha uwalimu Nkurumah, ili kupata waalimu wenye sifa na uwezo zaidi wa kufundisha. Walisema kwa sasa kuna waalimu waliosoma sana na na sio waliosomea, jambo linalochangia kushuka kwa hadhi ya elimu Zanzibar, ikilinganishwa na muongo mmoja uliopita. Wakizungumza na waandishi wa habari katika miji ya Chake chake, Wete na Micheweni wadau hao walisema, ni vyema sera ikatambua na kukirejeshea hadhi hicho hicho cha waalimu. Walisema, chuo hicho kilitoa mafunzo ya kina kwa waalimu na kuwajenga kiuwezo hata kama hawakua na elimu ya juu mfano wa shahada na uzamilivu. Mmoja kati ya wadau hao mwalimu mstaafu skuli ya Uweleni, Mohamed Ussi Shaame, alisema chuo hichoo kilikuwa mwarubaini wa kuipandisha hadhi elimu ya Zanzibar. “Kwenye sere mpya ya elimu ijayo ni vyema ikatamka wazi wazi, suala la kukifufua kimafunzo na kimasomo chuo cha uali

TIMU ZA SOKA ZA MAHAKAMA, WAZEE WA CHAKE CHAKE ZAHESHIMIANA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA TIMU za soka za mahakama kuu Pemba, na ile ya wazee ya mji wa Chake chake, zimeshindwa kutambiana kwenye mchezo maalum, wa kuisindikiza siku ya kilele cha maadhimisho ya siku ya sheria Zanzibar, mchezo uliopigwa uwanja wa Polisi Madungu jioni. Katika mchezo huo, uliohudhuriwa na watazamaji wengi kiasi, ulianza kwa kasi, ili kila tumu iondoke na ushindi uwanjani hapo. Dakika ya 22, nusura timu ya Mahakama kuu Pemba, ijipatie goli la kuongoza, baada ya mshambuliaji wake Adam Abdalla, kuachia fataki zito langoni mwa timu ya wazee, ingawa liliokolewa na mlinda mlango wao, Said Mohamed. Dakika 45 za awali, zilimalizika kwa kosa kosa za hapa na pale, na kipindi cha pili, kilianza kwa kasi na mashambulizi ya kushtukizia kila upande. Dakika 79, baada ya timu ya wazee kugongeana vyema, na kisha mpira kumfikia   Saleh Said, aliburura na kuwapiga chenga walinzi wa mahakama, ingawa shuti lake, lilikuwa chakula   mbele ya mlinda mlango wao Abubakar Ali. Timu ya m

MABADILIKO SHERIA YA HABARI ZANZIBAR NI LAZIMA

  DEMOKRASIA ni neno lenye uwanja mapana, lakini ikitekelezwa katika jamii ama katika nchi huwa kuna faida kubwa hasa ikizingatiwa kuwa hoja za wengi ndizo zinazofuatwa na kutekelezwa. Hata hivyo, kwenye jamii yenye kuzingatia demokrasia ya kweli wachache kwa uchache wao nao husikilizwa hoja zaa na sio kupuuzwa na inapotokea hoja za wachache zina mantiki sio dhambi kutekelezwa. Wataalamu wengi wanakubaliana kuwa uwepo wa vyombo vya habari vya aina mbalimbali una mchango mkubwa kwenye ujenzi wa demokrasia na pia suala la kupata habari linahesabiwa kama miongoni mwa haki muhimu za binaadamu. Ili vyombo vya habari vitekeleze vyema jukumu la kujenga demokrasia katika nchi, lazima viwe huru katika kutekeleza majukumu yake pasiwepo na taasisi ama mtu ambaye kwa nguvu zake ama utashi wake atakuwa anaamrisha habari ipi itoke na ipi isitoke, pengine tu kwa maslahi yake sio maslahi ya jamii. Uhuru huo wa vyombo vya habari katika nchi, lazima uambatane na uwepo wa sera, sheria na kanuni rafiki za

NYUMBA ZA UZUNGUNI WETE KUFANYIWA MATENGENEZO.

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA WAKAAZI wa nyumba za Serikali zinazosimamiwa na Wakala wa Majengo Pemba, ambazo zipo Uzunguni Wete wametakiwa kuhama, ili kupisha matengenezo ya nyumba hizo. Akizungumza na baadhi ya wakaazi wa nyumba hizo, Afisa Mdhamini Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Pemba, Bakar Ali Bakar alisema, ni vyema wananchi wakahama katika nyumba hizo, kwani zinahatarisha usalama wa maisha yao. Alisema kuwa, kutokana na ubovu wa nyumba hizo haistaki tena kuishi wananchi, hivyo ni vyema wakasikiliza maagizo ya Wizara kuhusu kuhama eneo hilo, ili ziweze kufanyiwa matengenezo. “Tuliwahi kuwapelekea barua ili wahame kwenye nyumba hizi kwa sababu ni mbovu na tayari zimeshafanya mipasuko, hivyo ni hatari kwa maisha yao, lakini baadhi yao bado hawajakubali kuhama”, alisema Mdhamini huyo. Aliwaomba wakaazi hao kuridhia maagizo ya kuhama kwenye nyumba hizo, huku Wizara ikiandaa utaratibu wa kuzijenga, ili kuepuka maafa yanayoweza kutokea. “Serikali ina azma nzuri kwenu, ha