Skip to main content

Posts

Showing posts from September 21, 2025

CHILO: WAGOMBEA CCM MTAMBILE KULIBADILI JIMBO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MJUMBE wa Kamati Kuu ya Halmshauri kuu ya CCM taifa Khamis Hamza Chilo, amesema wateule waliopewa ridhaa na chama hicho, wanatosha kulibadili jimbo la Mtambile kimaendeleo. Chilo, aliyasema hayo Septemba 27, 2025 uwanja wa mpira Kengeja jimbo la Mtambile, wilaya ya Mkoani, kwenye uzinduzi wa kampeni kwa nafasi ya ubunge, uwakilishi na udiwani wa jimbo hilo. Amesema, CCM haijawi kufanya kosa katika kuteua wagombea, iwe ngazi ya udiwani, uwakilishi, ubunge na urais, kwani huwa tayari wameshaandaliwa kiutumishi. Alieleza kuwa, wananchi wa Jimbo la Mtambile, wahakikishe kura zao ikifikapo Oktoba 29 mwaka huu, wanawapa kura za ndio wagombea hao, ili kuja kuwalipa maendeleo. Chilo alifahamisha kuwa, wagombea wote hawana shaka, na suala la kushirikiana na wananchi, katika kutekeleza Ilani ya CCM ya mwaka 2025/2030. ‘’Mimi nawahidi wananchi wa Jimbo la Mtambile kuwa, wagombea mlioletewa sio maji taka, ni wapambanaji, wapiganaji na wenye uchu wa maendeleo,’’alifa...

DK. MWINYI AKIWA MAKOMBENI AWAKUNA WANAOYASHUGHULIKIA MASHAMBA YA MIKARAFUU YA SERIKALI

          NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MGOMBEA Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema kuelekea uchaguzi mkuu wa vyama vingi, Oktoba mwaka huu, suala la kuhubiri amani na utulivu liwe ndio ajenda. Mgombea huyo wa urais aliyasema hayo jana, uwanja wa mpira wa Makombeni wilaya ya Mkoani Pemba, kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni kwa chama hicho, kuelekea uchaguzi mkuu mwezi Oktoba mwaka huu. Alisema, haiwezekana kutekeleza jambo lolote pasi na kuhubiri amani na utulivu, maana ndio msingi wa kila jambo. Alieleza kuwa, kama kuna mtu anadhani hilo sio jambo la msingi, sio vyema kuungwa mkono, kwani hakuna jambo ambalo linaweza kutekelezeka pasi na amani na utulivu. ‘’Kwanza niwambie kuwa tutaendelea, kuhubiri amani, mshikamano na umoja maa andio msingi mkuu wa kila kitu,’’alifafanua. Aidha, Dk. Mwinyi alisema anakusudia kuwa Zanzibar kusiweko na skuli hata moja, ambayo wanafunzi wanaingia mikondo miwili, bali ...

MAJAALIWA ASEMA HEMED ATOSHA KIWANI, AWAAHIDI WANANCHI AMANI

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@ MJUMBE wa Kamati kuu ya Halmashauri kuu ya CCM taifa Majaaliwa Kassim Majaaliwa, amewataka wanachi wa Jimbo la Kiwani, kuwachagua wagombea wote wa CCM kwenye uchaguzi wa mkuu mwaka huu. Alisema, kama wananchi wanataka maendeleo ya kweli, wagombea waliopitishwa ndani ya jimbo hilo wanatosha, kufikia maendeleo yao. Majaaliwa aliyasema hayo leo Septemba 21, 2025, Kwareni Mwambe jimbo la Kiwani wilaya ya Mkoani, alipokuwa akiwanadi wagombea ubunge, uwakilishi na madiwani wa jimbo hilo, kuelekea uchaguzi mkuu, mwezi Oktoba mwaka huu. Alieleza kuwa, tayari CCM imeshandaa mpango kazi wa miaka mitano ijayo, ambapo ndani yake eneo la Jimbo la Kiwani, limeshaelezwa vya kutosha. Alieleza kuwa, huduma zote muhimu ikiwemo maji safi na salama, afya, barabara na uwezeshaji wananchi kiuchumi, limetajwa ndani ya mpango huo. Alieleza kuwa, kila mmoja ajitokeze kupiga kura kwa amani, ingawa kura zao wahakikishe wanawapigia kura mbunge, mwakilishi wa madiwani wote wa Ji...