Skip to main content

Posts

Showing posts from October 2, 2022

'MUDA NILIYODAIWA KUBAKA NILIKUWA NAPIGA MSWAKI' MTUHIMIWA PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MTUHUMIWA wa ubakaji, Sabour Juma miaka 47 mkaazi wa Chanjaani wilaya ya Chake chake, ameiambia mahkama ya makosa ya udhalilishaji ya mkoa wa kusini Pemba iliyopo Chake chake kuwa, muda aliyodaiwa kuwa amebaka, alikuwa kwake akipiga msuwaki.   Alidai kuwa, maelezo ya mashahidi kuwa majira ya asubuhi alimuingiza mtoto wa miaka 11 ndani ya choo cha nyumbani yake sio sahihi, kwani muda huo alikuwa nje ya nyumba akipiga msuwaki ‘ akisugua meno’ .   Aliyadai hayo mbele ya mahakama hiyo, chini ya Hakimu Muumini Juma Ali, wakati mtuhumiwa huyo aliyekuwa akiongozwa na wakili wake Suleiman Omar, akijitetea, baada ya upande wa mashtaka kufunga ushahidi wao.   Alidai kuwa, familia ya mtoto huyo inachoyo naye na imemtengenezea mazingira ili kumshitaki na kumfungisha, na wala hakumumbuki kumbaka mtoto huyo.   ‘’Sikumbuki kumbaka mtoto huyo wa miaka 11, aliyekuja kutoa ushahidi mahakamani hapa, bali wamenitengenezea zengwe kwa njia ya kunibambikizia kesi hii

KHAMIS 'soda' MIAKA 76 WA PEMBA AHEMEA RUMANDE KISA UBAKAJI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA::: MAHKAMA maalum ya makosa ya udhalilishaji mkoa kusini   iliyopo Chake chake, imelazimika kumrejesha tena rumande mtuhumiwa Khamis Haji Chumu ‘soda’ miaka 76, anayekabiliwa na makosa mawili, likiwemo la ubakaji, baada ya ombi lake la dhamana, kutosikilizwa na mahakama kuu.   Awali mtuhumiwa huyo akiwa na wakili wake, wameshapeleka ombi la dhamana yake mahakama kuu wiki iliyopita, hivyo kwa vile mahkama hiyo, bado halijalikalia kitako ombi hilo, amelazimika kurejeshwa tena rumade.   Mara baada ya kuwasili mahkamani hapo akitokea rumande, mtuhmiwa huyo, bila ya kuwepo kwa wakili wake, alidai kuwa hana taarifa zozote, ikiwa ombi lake limeshasikilizwa ama laa.   Hakimu wa mahakama hiyo Muumini Ali Juma, alimuuliza mtuhumiwa huyo, ikiwa ameshaarifiwa na wakili wake juu ya kupatiwa au kukataliwa kwa dhamana, na kujibu hana taarifa rasmi.   ‘’Mtuhumiwa wewe na wakili wako mlipeleka ombi la dhamana mhakama kuu, kutokana na hali yako, jee mmefikia wap

ZAWA WASAKENI MAFUNDI WA MAJI MITAANI - KADUARA

  Na Salma Lusangi WAZIRI wa Maji, Nishati na Madini Zanzibar Shaibu Hassan Kaduara ameagiza Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA) kuwatafuta na kuwachukulia hatua mafundi wa maji wa mitaani ambao wanaunga maji kwa wananchi kinyume na Sheria zilizoekwa na Wizara yake. Akizungumza katika kikao na uongozi pamoja na wafanyakazi wa ZAWA huko Gombani, Pemba mwishoni mwa wiki aliwataka watendaji hao kuwatambua   wateja wao pamoja na kuwasaka mafundi wa maji wa mitaani ambao wanaunga maji kwa watu kinyume na Sheria. Alisema Wizara ya Maji, Nishati na Madini kupitia taasisi yake ZAWA imeshatoa muongozo kwamba watu wanaohitaji kuungiwa maji wafike katika ofisi hiyo kwaajili ya kujisajili. “ ZAWA hamuwajui wateja wenu, hamuwatambui mafundi wa mitaani! Mapato ya maji yanapotea kwasababu hamjawajibika ipasavyo. ZAWA watambueni wateja wenu, mafundi wa mitaani wanaowaungia watu maji kinyume na sheria ”. Alisema kaduara Pia alisisitiza umuhimu wa ZAWA kujipanga katika kukusanya mapato ya maji.

MIRADI YA MAJI KUKABIDHIWA DISEMBA 2022

  Na Salma Lusangi::::: NAIBU Katibu Mkuu Wizara ya Maji Nishati na Madini Mwanajuma Majid Abdullah amesema Wizara yake inatarajia kukabidhiwa miradi ya maji ifikapo Disemba mwaka huu, hivyo amewaomba wananchi wawe na subra kwani miradi hiyo imefikia asilimia 80 ya utekelezaji wake ikiwemo wa uchimbaji wa visima, ulazaji wa mabomba na ujenzi wa Matangi ya maji. Akizungumza mara baada ya kushiriki ziara ya pamoja na kamati ya Ardhi, Mawasiliano na Nishati ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar katika maeneo mbali mbali ya miradi hiyo. Alisema anafahumu kwamba tatizo la maji halistahamiliki lakini amewaomba wananchi kuendelea kupokea huduma ya maji kwa mgao kwani sio muda mrefu tatizo la maji litamalizika Zanzibar. Alisema tatizo la maji Zanzibar limetokana na uwepo wa visima vichache ambavyo vinatumika pamoja na uchakavu wa miondombinu ya maji lakini kupitia jitihada za Mhe. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Mwinyi za kuwaondolea shida ya maji wananchi wake. W

MWALIMU SKULI YA MADUNGU ANAYEDAIWA KUMBAKA MWANAFUNZI WAKE AREJESHWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:::: MWALIMU wa skuli ya Madungu msingi Ali Makame Khatib miaka 25, anayetuhumiwa kumbaka mwanafunzi wake, amerejeshwa tena rumande na mahakama maalum ya makosa ya udhalilishaji, baada ya upande wa mashtaka kutopokea shahidi mpelelezi.   Baada ya kufika mahakamani hapo akitokea rumande, Mwendesha mashataka kutoka ofisi ya Mkurugenzi wa mashtaka Ali Amour Makame, alidai kuwa, shauri hilo lipo hatua ya kusikiliza ushahidi.   Alidai kuwa, walitarajia kumpokea shahidi ambaye ni Askari mpelelezi, ingawa hakutokeza mahakamani hapo, na wala upande wao, hawana taarifa za dharura yake.   ‘’Ni kweli mheshimiwa hakimu, shauri hili la mwalimu wa skuli ya Madungu, tulitarajia kumsikiliza shahidi wetu wa mwisho ambae ni askari mpelelezi, ingawa hakufika mahakamani hapa,’’alidai.   Hivyo wakili huyo, aliiomba mahkama hiyo, kuliahirisha shauri hilo na kulipangia siku nyingine, ili kuendelea na utaratibu mwengine mahkamani hapo.   Baada ya maelezo hayo, Haki

KADUARA ATOA AGIZO ZITO KWA ZECO PEMBA

  Na Salma Lusangi WAZIRI wa Maji, Nishati na Madini Zanzibar Shaibu Hassan Kaduara, ameuagiza uongozi wa Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) kufikisha huduma ya umeme haraka sehemu  ambazo wananchi wameekeza kilimo ili waweze kuzalisha kwa gharama ndogo na nafuu.                           Aliyasema hayo leo wakati akizungumza watendaji wa shirika hilo  Tibirizi Wilaya ya Chake Chake Pemba.  Alisema mkulima yeyeto akifikishiwa  huduma ya umeme ataweza kuzalisha mazao kwa gharama ndogo hali hiyo itapelekea bidhaa kuuzwa kwa bei ndogo kwasababu alizalisha kwa gharama ndogo. Alifahamishwa kwamba Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ameshatoa agizo  nguzo za umeme zitolewe bure kwa wananchi, hivyo ZECO harakisheni kuwafikishia wananchi nguzo za umeme hasa kwa wanaodhalisha mazao mbali mbali ili wapate urahisi wa kuzalisha bidhaa zao. “ZECO kwanini mnachelewesha kufikisha nguzo za umeme kwa watu wanaozalisha, acheni kuzipigia hesabu gharama za nguzo, hiz

RUZUKU YA TASAF YAWAPA UHAKIKA WA KIPATO WANAWAKE TUMBE PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA SHEHIA ya Tumbe Mashariki wilaya ya Micheweni Pemba, inawakaazi 7,675 kati ya hao, ni wananchi 225 wanaoendelea kupokea rukuzu kutoka TASAF. Kati hao, wapo wananchi 20 kutoka ndani ya mpango huo sasa, wameamua kujiajiri na kuendesha maisha yao, kwa kuanzisha miradi kama vile biashara na kilimo cha mboga mboga. Shehia ya Tumbe iliyoko wilaya ya Micheweni Pemba, ni kati ya zile shehia 78 zinazoendelea kuhudumiwa na TASAF, kwa wananchi wake kuendelea kupokea rukuzu. Maana TASAF, inao walengwa 14, 280 kwa wilaya zote nne za Pemba, ambao hao wapo walioanzisha vikundi vya ushirika iwe ni utengenezaji sabuni, mboga mboga, ufugaji ama biashara. Katibu wa sheha wa shehia ya Tumbe Mashariki, Makame Hassan Makame, anasema moja ya shehia ambazo TASAF imeacha alama ya mafanikio, ni yao kwao. ‘’Wapo walengwa wa kunusuru kaya maskini 20, hawa sasa hatuwatarajii kurudi tena kwenye umaskini wa kipato, kama ilivyokuwa kabla ya ujio wa TASAF,’’anaamini.   Pamoja na

'NJOONI MUFANYE MAZOEZI YA VIUNGO VILABU ''FULL NIDHAMU'

  NA HAJI NASSOR, PEMBA WANANCHI kisiwani Pemba, wameshauriwa kujiungu na vikundi vya mazoezi ya viungo, kwani vimejiwekea utaratibu mzuri, ambao unapingana na utovu wa nidhamu kwa wanamaoezi.   Kauli hiyo imetolewa na Katibu wa muda wa Umoja wa vilabu vya mazoezi ya viungo Pemba ‘PAFIC’ Khalfan Amour Mohamed, wakati akizungumza kwenye mafunzo ya siku moja, kwa wanamazoezi wa vilabu hivyo, yaliyofanyika skuli ya msingi Mchanga mdogo wilaya ya Wete.   Alisema, wamekuwa wakisemwa vibaya na baadhi ya watu, kuwa ndani ya vilabu vya mazoezi kuna kuvunjiana heshima, jambo ambalo sio sahihi.   Alieleza kuwa, wamekuwa na utaratibu mzuri ambao jinsia moja na nyingine, hazivunjiani heshima, hivyo kama wapo waliokuwa wakilihofia hilo, wasiwe na wasi wasi nalo.   Katibu huyo wa muda alifafanua kuwa, wanachama wa vilabu vyote, wamekuwa wakielimishwa kila siku, juu ya umuhimu wa kuheshimiana na kulindiana nidhamu, ili lengo la kufanya kwao mazoei lifikiwe.   ‘‘Kama wapo wananch