Skip to main content

Posts

Showing posts from January 1, 2023

WANAFUNZI WA MADRASSA CHAKE CHAKE WAPEWA NJIA KUJIKINGA NA UDHALILISHAJI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA::: IDARA ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar, ofisi ya Pemba, imewakumbusha wanafunzi wa madrassa za qur-an kisiwani Pemba, kujitenga mbali na watu wanaowanesha dalili za vitendo vya udhalilishaji, ikiwa ni pamoja na kuwawekea picha chafu kupitia simu zao. Kauli hiyo imetolewa leo Januari, 7 2023 kwa nyakati tofauti, na mwakilishi wa Idara hiyo Mohamed Massoud Said, wakati akizungumza na wanafunzi wa madarassa za Vikunguni na Machomane wilaya ya Chake chake, kwenye ziara maalum, ya kutoa elimu ya kupambana na matendo hayo.   Alisema, moja ya dalili ya mtu anaetaka kumdhalilisha mtoto huanza kwa kumuonesha picha za ngono, kumnunulia zawadi, kumpa fedha, na kuendelea kwa maneno ya ushawishi juu ya udhalilishaji. Alisema ni jukumu lao, kwanza kutoshirikiana na watu wa aina hiyo, hata ikiwa ni wazazi wao, au kutoa taarifa kwa watu wengine, kabla ya kufanyiwa vitendo vya udhalilishaji. Mwakilishi huyo wa Idara ya Katiba na msaada wa kisheria, aliwataka

IDARA KATIBA YAUKARIBISHA MWAKA MPAY KWA KUTOA TAHADHARI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:: WANANCHI kisiwani Pemba, wametakiwa kuufanya mwaka mpya wa 2023, uwe wa mageuzi kwa kupunguza matukio ya ukatili na udhalilishaji, kwa kuwatumia wasaidizi wa sheria, ili kupata elimu, ushauri na msaada wa kisheria.   Kauli hiyo imetolewa na Afisa sheria, kutoka Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria Zanzibar, ofisi ya Pemba Bakari Omar Ali, wakati akizungumza na mwandishi hizi, katika kuukaribisha mwaka mpya.   Alisema, matukio ya ukatili na udhalilishaji kwa wanawake na watoto bado yalikuwa yameshika kasi kwa mwaka 2022, hivyo amewataka wananchi, kwa huu 2023 uwe mwaka wa mageuzi kwa kupunguza matukio hayo.   Alieleza kuwa, Idara inaowasaidizi wa sheria katika kila jimbo, la uchaguzi, hivyo ni vyema wakawatumia ili kupata uwelewa wa kisheria, sambamba na elimu ya kupambana na matukio hayo.   Afisa sheria huyo alifafanua kuwa, wasadizi hao wa sheria, wako tayari na saa yoyote kutoa elimu na msaada wa kisheria bila ya malipo, hivyo ni wajibu wa

WAZIRI RAHMA APONGEZA UZALENDO WA KIVITENDO GANDO

  WAZIRI wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanzibar, Rahma Kassim Ali amewashukuru wananchi wa Kijiji cha Gando Pemba kwa uzalendo wao wa kutoa eneo la ardhi kwa kikosi cha KMKM kwa ajili ya ujenzi wa   kituo cha Afya. Kauli hiyo ameitowa wakati alipoweka jiwe la msingi katika eneo hilo ikiwa ni shamra shamra za maadhimisho ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar kutimiza miaka 59 tangu yalipotokea mwaka 1964. Alisema wananchi wa Kijiji cha Gando wameonesha   moyo wa uzalendo na kueka kando itikadi za kisiasa kwa kutoa eneo lao kuwapa Kikosi cha KMKM kujenga Kituo cha Afya. hivyo ni jambo   jema na la kuwashukuru. “Hakika nyinyi ni wana mapinduzi halisi na mmeonesha kwa vitendo jinsi mnavyoshirikiana na Serikali kuleta maendeleo katika eneo lenu. Nasaha zangu kwa wananchi wengine Unguja na Pemba kuiga   mfano wenu hasa ikizingatiwa kuwa maendeleo hayana chama, nakushukuruni kwa dhati kwa kutoa eneo lenu kwajili ya kituo cha afya,”alisema. Pia aliwashukuru mafundi na vibarua wa KMKM,

MAPINDUZI YA MWAKA 1964 MKOMBOZI WA MAWASILIANO MTANDAO ZANZIBAR, MIAKA 59 SASA DUNIA WA KIGANJA

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA::: MAPINDUZI ya 1964 chini ya jemedari wake marehemu Abeid Amani Karume, yamekuja kutatua changamoto za wananchi pamoja na kuimarisha sekta mbali mbali ya kimaendeleo, hapa nchini. Miongoni mwa hayo ni kuimarisha huduma za mawasiliano ya kimtandao, kila kona ya Zanzibar, ili kuhakikisha kwamba wananchi wanafanya kazi zao vizuri kupitia mawasiliano. Mawasiliano ya kimtandao ni muhimu, katika maisha ya kila siku ya mwanadamu, kutokana na kurahisisha kila kitu katika ulimwengu huu wa sasa kidijitali. Wanajamii wana msemo wao usemao… ‘dunia kiganjani’ hii inaonesha dhahiri kwamba mawasiliano ya kimtandao, yamerahisisha kila kitu katika ulimwengu huu na sasa kuwa kiganja. Njia mbali mbali zinatumika kuwasiliana kwa sasa, ukilinganisha na zamani kabla ya Mapinduzi yam waka 1964 ambayo sasa tunasherehekea miaka 59, ambapo watu walilazimika, kupeleka barua kufikisha ujumbe ambapo ulikuwa ukichukua muda mrefu. Lakini kwa miaka hii 59 ya Mapinduzi matukufu y

MIAKA 59 YA MAPINDUZI: DK. MWINYI AFUNGUA SKULI YA GHOROFA MWAMBE, AAHIDI KUJENGA NYINGINE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:: RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameigaiza wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, kushirikiana kwa karibu na Idara ya Utumishi, ili kuajiri waalimu nchini. Alisema, changamoto ya uhaba wa waalimu anajua kuwa, ipo, lakinini ni vyema kwa wizara husika, kuongeza kasi ya kuajiri waalimu na kipaumbele, iwe ni wale ambao walishajitolea siku za awali. Alieleza kuwa, wakati serikali ikijenga skuli mpya zikiwemo za ghorofa na kuzifanyia ukarabati zile za zamani, lazima na suala la kuajiri waalimu nalo liangaliwe kwa haraka. Dk. Mwinyi ameyasema hayo Mwambe wilaya ya Mkoani Pemba, mara baada ya kuifungua skuli mpya ya ghorofa mbili ya msingi Mwambe, wakati akizungumza na wanafunzi na wananchi wengine, ikiwa ni shamra shamra za miaka 59, ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964. Alieleza kuwa, anasisitiza kuwa, wakati wizara hiyo ikiajiri waalmu wakiwemo wa masomo ya sayansi, iwape kipaumbele waalimu wenye sifa,

BLOG PEMBA TODAY YASAIDIA KUIREJESHA HUDUMA YA MAJI SHUMBA MJINI PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:: WANANCHI 6,680 wa shehia ya Shumba mjini wilaya ya Micheweni Pemba, waliokuwa wakikabiliwa na ukosefu wa huduma ya maji safi na salama kwa muda wa mwezi mmoja, sasa huduma hiyo, imerejea kama kawaida.   Itakumbukwa kuwa, Novemba 20, mwaka 2022, blog hii   https://pembatoday.blogspot.com/2022/11/shumba-pemba-watumia-maji-ya-bahari-kwa.html ilichapisha habari ikielezea tatizo la ukosefu wa huduma hiyo kwa wananchi   hao.   Walisema, huduma hiyo kwa sasa imerudi kama asili yake, baada ya huduma ya nishati ya umeme, nayo kurudi kama kawaida hasa kwenye kisima chao cha maji safi na salama kilichopo Shumba wilayani humo.   Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kupitia blog hii, walisema huduma hiyo imerejea vyema, baada ya blog ya pemba today kuripoti ukosefu huo mwezi mmoja uliopita.   Walisema kabla ya kurejea kwa huduma hiyo, awali walilazimika kununua kwa dumu moja lenye ujazo la lita 20, kati ya shilingi ya 500 hadi shilingi 1,000, kutoka