Skip to main content

Posts

Showing posts from January 14, 2024

ACT-WAZALENDO CHAKE CHAKE CHAPATA VIONGOZI WAPYA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANACHAMA wa Chama cha ACT-Wazalendo mkoa wa Chake chake kichama, wamekamilisha uchaguzi wao mkuu, baada ya kuwapata viongozi wapya, watakaokiongoza chama hicho, kwa miaka mitano ijayo.   Katika uchaguzi mkuu huo, umemrejesha tena kwenye nafasi ya Katibu, aliyewahi kuwa Mwakilishi wa majimbo ya Vitongoji na Wawi wakati huo, Saleh Nassor Juma, baada ya nafasi yake kukosa mpinzani. Ambapo katika uchaguzi huo, uliofanyika Gombani Chake chake Pemba, alijizolea kura 65, kati ya kura 73 zilizopigwa, huku kura mbili zikiharibika na kura sita zikimkataa. Aidha Msimamizi wa uchaguzi huo Rashid Ali Abdalla, alimtangaaza Yussuf Salim Khamis, kuwa ndie Mwenyekiti wa Chama hicho kwa kipindi cha miaka mitano ijayo, baada ya kupata kura 39 na kumshinda mpinzake Mohamed Juma Khatib aliyepata kura 34. Katika uchaguzi huo, ulimchagua Khadija Ali Abeid kuwa Mshifa fedha wa Mkoa wa Chake chake kwa kura 36, baada ya kumuangusha mgombea mwenzake, Khadija Anuwar Mohamed,

WANANCHI PEMBA WASEMA JAMBO FEDHA ZA UVIKO19 KWENYE AFYA

     NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@@ WANANCHI kisiwani Pemba, wamesema fedha za ahuweni ya UVIKO 19, zilizoelekezwa kwenye miradi ya wizara ya Afya kisiwani humo, zimetumika vyema, na sasa wanaendelea kunufaika nazo. Walisema, serikali iliweka wazi mgao wa fedha hizo na matumizi yake, ambapo kwa upande wa Wizara ya Afya na hasa kisiwani Pemba, zilizitumia kwa ujenzi wa hospitali za kisasa. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, juu ya kumalizika na kuanza kazi kwa hospitali hizo, walisema majengo hayo yamekuwa ya kiwango cha juu, ujenzi wake. Walieleza kuwa, sasa wameshaachana na majengo ya zamani, ambayo hayakuwa na nafasi, kwa ajili yao na madaktari wanapotoa huduma kwa wagonjwa. Maryam Himid Mjaka wa Micheweni, alisema sasa wamekuwa na nafasi kubwa ya kukaa kumsubiri daktari, ikilinganishwa na hospitali yao ya zamani. Kazija Haji Mshamata wa Konde, alisema sasa wamekuwa na hamu ya kwenda kutafuta huduma kwenye hospitali ya Micheweni ama Kinyasini, kutokana na ubora wake.

MJUE MWANAMKE ANAYEZIPENDEZESHA FUKWE KWA USAFI

  NA AMRAT KOMBO, ZANZIBAR@@@@ Maisha ya binaadamu huwa   salama na ya afya njema kama mazingira yanayomzunguka yapo safi na salama na yanapokuwa yameharibika huwa hatarishi kwake, wanyama, wadudu na mimea. Hali hii ndio inayopelekea kusikia kila kukicha   wizara ya afya   kwa kupitia wataalamu wake mbali mbali inasisitiz umuhimu wa kuweka mazingira safi ndani na nje ya nyumba zetu, mitaani, vijijini na katika maeneo ya biashara kama masoko au ya kuuza na kununua chakula. Mwanamke amekuwa akionesha uongozi mzuri kwenye jamii zetu kwa kuanzia kwenye familia na kutokana na jamii yetu, katika miaka ya karibuni kutotilia maanani sana usafi wa mazingira kumepelekea kujitokeza watu kuongoza jamii kufanya marekebisho yanayohitajika. Miongoni mwa wana jamii waliojitokeza   kuwa mstari wa mbele kuongoza juhudi za kutunza mazingira ni mwana mama anyeiingoza Kikundi cha Ulinzi wa Mazingira, Siwema   Mshenga   Issa, kutoka Sheiha ya Bubwini Makoba. Yeye na wenzake walianzisha kikundi hic

ACT-WAZALENDO CHAKE CHAKE: 'CHAGUWENI VIONGOZI WATAKAOKIVUUSHA CHAMA 2025'

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANACHAMA wa mkutano mkuu maalum wa chama cha ACT-Wazalendo, mkoa wa Chake chake kichama, wametakiwa kuwachagua viongozi wenye uwezo na nia thabiti, ya kukivuusha chama katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2025. Ushauri huo,Januari 14, 2024 umetolewa na Mjumbe wa Kamati kuu taifa ya chama hicho, Isihaka Mchinjita, wakati akiufungua mkutano huo, uliofanyika ukumbi cha Chuo cha Samail Gombani Chake chake Pemba. Alisema, wajumbe wa mkutano huo mkuu maalum, ndio wenyejukumu la kuwapata viongozi watakaoshirikiana na wale ngazi ya taifa, katika kuelekea uchaguzi mkuu ujao. Alieleza kuwa, ikiwa watafanya makosa kwa kumchagua kiongozi kwa sifa za juu juu pekee, wanaweza kukipa wakati mgumu chama, wakati kinapoingia kwenye chaguzi mbali mbali. Alifahamisha, ili chama kiwe na nguvu, mwelekeo, dira inayotekelezeka, lazima kuwepo kwa viongozi imara kuanzia tawi, jimbo, mkoa na kisha taifa. ‘’Wajumbe wa mkutano huu mkuu maalum wa ACT-Wazalendo hapa mkoa Chake