NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, asubuhi ya leo April 2, 2026, anatarajiwa kuwa mgeni, rasmi katika uzinduzi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa, utakaofanyika, uwanja wa michezo Gombani Chake Chake Pemba. Taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa kusini Pemba, Rashid Hadid Rashid, kwa vyombo vya habari, ilieleza kuwa, tayari maandalizi yote yameshakamilika kwa shughuli hiyo ya kitaifa. Taarifa hiyo ilieleza kuwa, Dk. Mwinyi ataingia kwenye kitabu cha kumbukumbu kwa zoezi hilo, ambapo kwa mara ya kwanza, lilifanyika zaidi ya miaka 10 iliyopita kisiwani humo. Mkuu huyo wa mkoa katika taarifa yake, ilifafanua kuwa, Dk. Mwinyi atawahutubia wananchi watakaohudhuria, pamoja na kuzindua rasmi mbio za mwenge wa uhuru kitaifa, kwa mwaka 2026. Alieleza kuwa, wananchi watakaohudhuria kwenye zoezi hilo la kitaifa, kabla ya Dk. Mwinyi kufanya uzinduzi huo, watashuhudia burudani kadhaa uwanjani hapo. Alisema, m...