NA KHAULAT SULEIMAN, PEMBA@@@@ MKAGUZI wa jeshi la Polisi shehia ya Pandani wilaya ya Wete, Khalfan Ali Ussi, aliwakikishia mafundi wanaojenga kiuto cha cha Pandani kuwa, kua jeshi la Polisi kwa kushirikiana ulinzi shirikishi, kitakua bega kwa bega, ili kuhakikisha wanakamilisha ujenzi huo bila ya uhalifu. Alisema kua kazi ya jeshi la Polisi ni kuhakikisha usalama kwa wananchi wake, hivyo ni vyema kuendelea kufanya kazi zao wa weledi wa hali ya juu, na kujenga majengo yenye kiwango cha hali ya juu. Mkaguzi huyo aliwataka wafanyakazi wa kampuni hiyo, kufanya kazi kwa uzalendo na uaminifu, ili kujali na kulinda maslahi ya ya taifa. "Mkifanya hivyo mtaweza kujizuiya na matendo maovu, kama kujihusisha na vitendo vya udhalilishaji ikiwemo ubakaji, wizi, ulevi kwani jeshi la Polisi, halitosita kumchukulia hatua kali, kwa mfanyakazi yoyote atakaevunja sheria,"alisema. Nae Mkandarasi wa ujenzi huo pamoja na msimamizi wa mradi huo Laurent...