Skip to main content

Posts

Showing posts from May 21, 2023

WANAWAKE MAKOMBENI ""HATUNA UWELEWA MPANA DHANA UCHUMI WA BULUU"

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAWAKE wa shehia wa Makombeni wilaya ya Mkoani Pemba, wameomba kuongezewa ufahamu juu ya dhana ya uchumi wa buluu, ili waifahamu kwa kina malengo ya serikali kuu. Walisema, wamekuwa wakisikia juu juu ya dhana hiyo, ingawa bado wamekuwa hawana uwelewa wa ndani, na kusababisha kubakia na uwelewa wa wao zamani. Wakizungumza na waandishi wa habari wa Shirika la Magazeti ya serikali Zanzibar ofisi ya Pemba waliofika kusikiliza changamoto zao, walisema bado dhana hiyo haiku vyema kwenye akili yao. Walisema kua, wanahitaji mamla husika kufika Makombeni kuwaeleza kwa kina juu ya dhana ya uchumi wa buluu, ili waende samba mba na kaluli ya rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi. Mmoja kati ya wanawake hao Mayasa Makame Chumu, alisema bado baadhi yao wamekuwa wakisikiliza vyombo vya habari, ingawa dhana hiyo bado hawajaipata vyema. ‘’Dhana ya uchumi wa buluu tunaiskia kwenye vyombo ya habari, lakini hasa kuipata kwa

WANAHARAKATI, VYOMBO VYA ULINZI WATAJA MWARUBAINI KUKOMESHA KUJICHUKULIA HATUA MKONONI

    I NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ‘’ATAKAYE muua mwenzake, basi naye anyongwe, na kinga kuwa alikuwa na hasira isifanye kazi, yakifanyika hayo, kujichukulia sheria mikononi itakoma,’’wanasema wahanga wa matukio hayo. WAHANGA WANATOA RAI GANI? Mke ambaye muume wake aliuawa mwaka 2020 eneo la Micheweni kwa wananchi waliodaiwa kuwa na hasira, anasema njia pekee ya kuondoa utamaduni wa wananchi kujichukulia sheria mikononi, naye ni kuuliwa. Kijana Issa Haji Othman wa Mwanakwerekwe, anasema njia nyingine ya kukomesha wananchi kujichukulia sheria mikononi, ni kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria. Mayasa Haji Mzee wa Chake chake, anasema ili kukomesha wananchi kujichukulia sheria mikononi, ni wananchi kuelezwa mifumo ilivyo ya haki jinai. ‘’Wananchi hawaelewi kwa undani, mifumo ya haki jinai, kuanzia kesi inapokuwa Polisi, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka hadi Mahkamani pamoja na haki ya dhamana au rufaa,’’anasema. VYOMBO VYA KUSIMAMIA HAKI JINAI VINASEMAJE ?

VIFO VYA BODA BODA, WAHANGA, AMADEREVA, POLISI WATAJA MADHARA KWA JAMII

                              NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MOJA ya madhara ya vifo vya ajali za Boda boda ni kukatisha uhai wa abiria, madereva au waenda kwa miguu. Wahanga wanasema, licha ya magonjwa kama Corona, maleria, kipindu pindu kuwa yanapoteza wapendwa wao, lakini ajali za Boda boda zinachangia. Wanaainisha kuwa, boda boda zimekuwa zikikatisha uhai wa wapenzi wao, wakuu wao wa familia au wazazi wao, na kuwaacha wakiwa hawana uhakika wa maisha. Hassan Haji Mohamed wa Vitongoji wilaya ya Chake chake, anasema, kwa sasa anaishi na mguu mmoja kwa miaka saba, baada ya kupata ajali ya boda boda. ‘’Nilikuwa nimepakiwa nakwenda msibani kwa mdogo wangu, lakini kisha dereva alichanganya mwendo, na kuingia pembezoni mwa gari ya mzigi iliyokuwa imeegeshwa na kupata kilema cha kudumu,’’anakumbuka. Mohamed Othman Juma wa Mkoani mjini, anasema alipoteza vidole viwili vya mkono wa kulia, baada ya boda boda aliyokuwa amepanda kugongana na gari ya abiria. ‘’Mwendo u

WATU WENYE ULEMAVU MAKOMBENI WATAKA ELIMU KUANZISHA USHIRIKA

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WATU wenye ulemavu shehia ya Makombeni wilaya ya Mkoani Pemba, wamesema wana hamu ya kutaka kuanzisha vikundi vya ushirika, ingawa changamoto ni taaluma ndogo ya kuendesha vikundi hivyo. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi shehiani hapo, walisema wamekuwa na hamu ya kutaka kujikusanya, ili kufikia ndoto zao kupitia vikundi vya ushirika, ingawa changamoto ni elimu ndogo ya uanzishwaji wa vikundi. Walisema, wamekuwa wakigubikwa na umaskini wa kipato, ambao wanaamini kama wengekuwa na uwezo kielimu wa kuanzisha vikundi, wengekuwa na hali nzuri kimaisha. Mmoja kati ya watu hao wenye ulemavu wa ualibino Mbuke Ramadhan Mussa, alisema wamekuwa hawajui wapi pakuanzia ili hadi kufikia kuwa na kikundi cha ushirika. Alieleza kuwa, hawaelewi kuwa sheha anaweza kuwa chanzo cha wao kuanzisha vikundi vya ushirika, bali wapo kwenye makaazi wakiwa hawajui la kufanya. ‘’Ni kweli sisi watu wenye ulemavu wa shehia ya Mkoambeni, tunahitaji kupata uwelewa wa kuanzi

KIJALUBA iSAVE ZANZIBAR, MRADI JUMUISHI UNAOKUJA NA MBINU ZA KISASA KUKUZA PATO

                  NA HAJI NASSSOR, PEMBA@@@@ KIJALUBA iSAVE Zanzibar, ni mradi jumuishi, unaolenga kuwawezesha watu wenye ulemavu kiuchumi. Kupitia mradi huu, watu hao wenye ulemavu wa aina mbali mbali, utawajengea uwezo kuhusu maisha yao wenyewe na jamii zao, kwa ujumla. Maana, lengo kuu hasa la mradi huu wa Kijaluba iSAVE Zanzibar, unaangazia zaidi, kukuza uwezo wa watu hao, kwa kujenga mitazamo chanya, juu ya ushiriki wao, na kujiingiza katika shughuli za kujipatia kipato. Kipato hicho, hasa kwa aina ya maradi huo ulivyo, ni kupitia katika vikundi vyao vya kuweka na kukopa ‘saccos’ ambapo kwa baadhi ya maeneo, huitwa vikoba. MBINU ZA UTEKELEZAJI WA MRADI HUO Kwa mujibu wa Msaidizi Afisa Mradi wa kijaluba Mohamed Salim Khamis, anaefanyia kazi zake Pemba, anasema kwanza ni kuwawezesha watu hao kupata kipato. ‘’Lakini jengine ni kuwezeshwa, ili wawe na ushiriki kamili katika miradi na maendeleo ya jamii kwa ujumla, kutokana na mazingira yao,’’anasema. Mbinu nyingine

ZHC YAJA NA MPANGO WA NYUMBA KWA WENYE KIPATO CHA CHNI ZANZIBAR

  NA SALMA LUSANGI, ZANZIBAR@@@@ Shirika la Nyumba Zanzibar (ZHC) limesema linampango wa kujenga nyumba za kuwapangisha watu wenye kipato cha chini katika maeneo mbali mbali ya Unguja na Pemba.                                                                                                                                                   Kauli hiyo imetolewa mwisho wa wiki na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo Mwanaisha Ali Said wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Shirika hilo Darajani, Unguja.           Amesema Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imetenga ardhi ya akiba kwaajili ya Maendeleo hivyo Shirika litatumia fursa hiyo kujenga nyumba za kupangisha na  kuuza kwa wananchi mbali mbali  kwaajili ya kuleta makaazi bora.        Mkurugenzi Mwanaisha  amesema  ZHC kwasasa imeanza  kujenga nyumba za kuuza katika eneo la Mombasa kwa Mchina lakini hata mwananchi mwenyewe kipato cha chini anaweza kununua kutokana na utaratibu mzuri ambao ZHC  imepanga kuziuza nyumba hizo.  

‘’WAADHIBIWE WAZAZI WATAKAOWAKIMBIZA WATOTO WAO MAHAKAMANI’ : WADAU PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WADAU wa haki jinai kisiwani Pemba, wamesema ili kupunguza matendo ya ukatili na udhalilishaji, lazima kuwe na kifungu cha sheria, kinachowaadhibu wazazi na walezi, watakaobainika kuwatorosha watoto wao. Walisema, wazazi na walezi kwa sasa, wamekuwa wakiwatorosha watoto wao, iwe wa kike au kiume, mara baada ya kujitokeza kwa matendo hayo. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, juu ya uwepo wa wimbi kubwa la kufutwa kwa kesi za udhalilishaji, walisema kwa sasa, kumeibuka mtindo wa baadhi ya wazazi kuwatorosha watoto wao. Walisema, hayo hujitokeza kwa wazazi wa upande wa mtoto wa kike, na hasa ikiwa tayari wameshachukua rushwa au wameshaandaa mipango ya kuwafungisha ndoa. Mmoja kati ya wanaharakati hao, Dina Juma kutoka Jumuiya ya PEGAO, alisema wapo wazazi wamekuwa hawapendi kuendelea na kesi za watoto wao mahakamani, hivyo njia nyepesi ili kuiua kesi hiyo ni kumtorosha mtoto wake. ‘’Maana wanajua kuwa, mtoto aliyedhalilishwa huwa ni shahidi