Skip to main content

Posts

Showing posts from August 31, 2025

KUTISHIWA TALAKA KUNAVYOKATISHA NDOTO ZA WANAWAKE WANAOHITAJI UZAZI WA MPANGO

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ UZAZI wa mpango ni suala lenye kuleta utata kwa baadhi ya wanajamii ambalo huchukuliwa kwa sura tofauti. Kwani kuna baadhi yao huamini kwamba, uzazi wa mpango ni kufunga kizazi moja kwa moja, jambo ambalo sio sahihi, kwa sababu ni sawa tu na kusema... ‘kumuachisha mtoto’. Na kuachishwa mtoto ni kumpa nafasi mama aliejifungua kupumzika kwa ajili ya kuimarisha afya yake na mtoto, hivyo ni sawa na uzazi wa mpango. Jamii ifahamu kwamba kutumia uzazi wa mpango ni muhimu sana katika kuimarisha afya za akinamama na watoto, kwani dini ya kiislamu imehimiza mtoto kunyonyeshwa miaka miwili. Qur-an tukufu katika Suratul-Baqara aya ya 233 imeeleza kuwa, ‘Wazazi wa kike wanyonyeshe watoto wao miaka miwili kwa mwenye kutaka kutimiza kunyonyesha…’ Hiyo inaonesha wazi kwamba, kuachisha mtoto kwa miaka miwili ni muhimu sana kwa akinamama kutokana na faida inayopatikana ndani yake. Lakini kuna baadhi ya akinababa huipa kisogo aya hiyo na kuamua ...

MFAMAU ACHAMBUA NEEMA ZA DK. MWINYI UWANJA WA GOMBANI

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ AFISA Mdhamini wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Pemba, Mfamau Lali Mfamau amesema, kwa kazi iliyofanywa na Rais Dk. Mwinyi ya kuimarisha uwanja wa michezo wa gombani, ikiwemo kuezekwa, ni dhahiri, kwa wanamichezo hana deni. Alisema, kwa sasa uwanja huo ambao unavutia umezekwa na kuwafanya watamazaji kutonyeshewa na mvua wala kupigwa na jua, wanapokuwa uwanjani hapo. Akizungumza na waandishi wa habari na wahariri wa vyombo vya habari vya Tanzania bara na Zanzibar, waliokuwa wakiangalia miradi ya maendeleo, alisema kwenye michezo amefanikiwa. Alieleza kuwa, kazi iliyofanywa na Dk. Mwinyi kwa uwanja huo wa michezo Gombani pekee, imedhihirisha kutekeleza tunu ya wanamichezo. Alifafanua kuwa, jingine ambalo limeimarishwa ndani ya uwanja huo, ni uwekaji viti uliozunguruka uwanja wote, jambo ambalo kabla, halikuwepo. Mdhamini huyo aliongeza kuwa, kwa sasa kunasehemu tatu maalum ‘VIP’, ikiwemo ya mawaziri, viongozi wakuu wa nchi ...

NYENZO UTEKELEZAJI SERA YA MAENDELEO YA WATOTO IMEPATIKANA

Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Abeida Rashid Abdallah amesema Mpango Jumuishi wa Malezi Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto wa Miaka Mitano (5) utakapokamilika utakuwa nyenzo muhimu ya utekelezaji wa Sera ya Maendeleo ya Watoto na Malengo ya Kitaifa na Kimataifa. Kauli hiyo ameitoa wakati akifungua kikao kazi cha siku tatu 01-3/09/2025 cha kuandaa Mpango huo kilichofanyaka katika Hotel ya Visitors Inn, Jambiani, Mjini Unguja kilicho andaliwa na Taasisi ya Afisi ya Rais Ufuatiliaji wa Utendaji Serikalini Zanzibar (ZPDB). Amesema Mpango Jumuishi wa Malezi Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto wa Miaka Mitano unahimiza huduma za afya, chanjo, lishe bora na ulinzi wa mtoto na malezi yenye mwitikio, hivyo kuchangia moja kwa moja kwenye Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs),hususan lengo nambari nne (4) linalohusiana na Kupunguza Vifo vya Watoto chini ya Umri wa miaka mitano.   Amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Ilani ya Chama cha M...

WANAFUNZI KIDATO CHA 6 KIWANI WASEMA TAYARI DK. MWINYI KESHAREJEA TENA IKULU

     HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI kidato cha sita, skuli ya sekondari ya Kiwani wilaya ya Mkoani Pemba, wamesema tayari Mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi ‘CCM’ Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesharejea tena Ikulu, kufuatia utekelezaji mkubwa wa Ilani, sekta ya elimu. Walisema, kujengwa skuli ya kisasa ya ghorofa na yenye vifaa vya kisasa vya sayansi, ni ishara ya kukubalika kwake, na tayari wanamuona ameshaingia ikulu kwa awamu ya pili. Wakizungumza na waandishi wa habari wa Unguja, Tanzania bara na wenyeji Pemba jana Septemba1, 2025, kwenye ziara maalum ya kuangalia utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025, walisema kwenye sekta ya elimu Dk. Mwinyi, hana mpinzani. Walieleza kuwa, ndani ya jimbo hilo la Kiwani pekee, zipo skuli zaidi ya tatu za ghorofa, ikiwemo yao, yenye vifaa vyote husika. Mmoja kati ya wanafunzi hao, Saleh Muhisn Haidar, alisema Dk. Mwinyi ni kiongozi mwenye maono na anayefikiria mbali, katika sekta kadhaa, ing...

NYUMBA ZA MADAKTARI MKOANI ZAWAPA UHAKIKA WA HUDUMA WAGONJWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ DAKTARI dhamana hospital ya Abdullah Mzee Mkoani Pemba, Khamis Suleiman Khamis, amesema kupatikana kwa makaazi ya ya madaktari, wanaofanyakazi hospitalini hapo, kumewapa uhakika wa matibabu wagonjwa wale wa dharurua na wa nyakati za usiku. Alisema, kazi iliyofanywa na Rais wa sasa wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi ya kuwajengea nyumba hizo, imeongeza bidii ya kazi kwa madaktari na kuwahakikisha huduma saa 24 wagonjwa. Daktari huyo dhamana aliyasema hayo leo Septemba 1, 2025, alipokuwa akizungumza na waandishi mbali mbali wa habari kutoka Zanzibar na Tanzania bara, katika ziara maalum ya kuangalia utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025. Alisema nyumba hizo 74 zimenodoa shida ya madaktari hao, kuishi mbali na kituo chao cha kazi, jambo ambalo lilikuwa likiwawiya vigumu wananchi, wanaohitaji huduma hasa wakati wa usiku. Alieleza kuwa, baada ya kumalizika ujenzi huo wa nyumba za kisasa, sasa, madaktari wameondokana na changamoto ya makaaz...