Skip to main content

Posts

Showing posts from December 4, 2022

''WANANCHI 108,860 ZANZIBAR WASHINDA KESI ZAO BAADA YA MSAADA WA KISHERIA'' MKURUGENZI ZLSC

  NA HAJI NASSOR, UNGUJA::: WANANCHI laki 118,760 wakiwemo wanawake 60,203, wanaume 39,641 na watoto 18, 232 wamenufaika na elimu, msaada na ushauri wa kisheria kwa muda wa miaka 30 na kati   ya hao, laki 108, 860 wameshinda kesi na kupata haki zao mbali mbali. Aidha kati ya hao 11, 8760 ni wananchi 9, 216 pekee ndio ambao licha ya kupata elimu na msaada huo wa kisheria, walishindwa katika kesi zao . Akizungumza kwenye kongamano la maadhimisho ya siku ya haki za binaadamu duniani, leo Disemba 10, 2022 lililofanyika Kijangwani mjini Unguja, na kuandaliwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar 'ZLSC' kwa kushirikiana na Tume ya Haki za Binaadamu 'CHRAGG' kwa ufadhili wa Umoja wa Mataifa, Ofisi ya Haki za Binaadamu 'UN-OHCHR' Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo hicho Harusi Miraji Mpatani, amesema wastan kwa mwaka waliopatiwa msaada ni wananchi 3, 936. Ameeleza pia Kituo kiliwasaidia watoto na masuala ya kisheria 18,232, ambapo pia kwa upande mwengine, Kituo hicho

ZLSC, UN-OHCHR LEO WAADHIMISHA SIKU YA KIMATAIFA YA HAKI ZA BINAADAMU ZANZIBAR

      NA HAJI NASSOR, UNGUJA:::: KITUO   cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ kwa kushirikiana na O fisi ya Umoja wa Mataifa, ofisi ya haki za binadamu (UN- OHCHR)  asubuhi ya leo Disemba 10, 2022 wanatarajia kufanya kongamano maalum la maadhimisho ya siku ya kimataifa ya haki za binadamu ulimwenguni.   Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari ofisini kwake Kijangwani mjini Unguja, Disemba 9, 2022 Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo hicho Harusi Miraji Mpatani, alisema Mkurugenzi wa Mashataka Zanzibar Jailan, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi.                                                    Alieleza kuwa, kongamano hilo linatarajiwa kufanyika ofisini kwao Kijangwani mjini hapa, na maandalizi yote yameshakamilika kwa asilimia 100.   Alisema katika kongamani hilo la kuadhimisha siku ya kimataifa ya haki za binadamu, wameshirikiana kwa karibu na ofisi ya Umoja wa Mataifa, ofisi ya haki za binadamu (UN-OHCHR)   Alisema, tayari waalikwa wote wakiwemo, wanasheria, mawakilisi wa seri

MWENYEKITI BODI ZLSC AWAONYESHA NJIA POLISI KUMALIZA UHALIFU

NA HAJI NASSOR, UNGUJA::: MWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ Jaji wa Mahakama kuu Zanzibar, Mshibe Ali Bakari, amesema lazima jamii na walinzi waamke, kutokana na wahalifu kutumia mbinu mbadala za kihalifu. Alisema, hata wale wanaowadhalilisha wanawake na watoto wamekuwa wakitumia mbinu za ziada, kabla na baada ya kufanya matendo hayo, ambapo sio rahisi hata wataalamu wa kiulizi kubaini. Mwenyekiti huyo wa Bodi, ameyasema hayo ukumbi wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzbar ‘ZLSC’ Kijangwani mjini Unguja, wakati akifungua kongamano la siku mbili, la kuelekea siku 16 za kupinga ukatili.   Alisema, lazima jamii na jeshi la Polis i liongeza nguvu za zaiada katika utendaji wake wa kazi, ili kukabiliana vyema na uhalifu na udhalilishaji uliopo.                                                                                    Alieleza kuwa, urahisi wa usafiri, wa vyombo vya maringi mawili, boti, ndege na meli zinazoingia Zanzibar, la

USAFIRISHAJI HARAMU BINADAMU TANZANIA, WAZAZI WAELEMEWA NA TAMAA, MADALALI MANENO KAMA ASALI

    USAFIRISHAJI HARAMU WA BINADAMU TANZANIA -Wazazi wakiri tamaa, umaskini vyawaelemea kuwatoa watoto wao   -Wasema madalali wana maneno ya kumtoa nyoka pangoni   HAJI NASSOR, PEMBA:: cell phone:  +255656265945 emali:          hajipembatoday@gmail.com ‘’Mimi baada ya kuona mtoto wa jirani yangu mwaka 2000 alisafirishwa na mtu tunayemjua, na wangu mimi mwaka 2022 nimemtoa, ingawa naarifiwa alishauawa akiwa Oman,’’maneno ya mzazi.   Mzazi huyo aliyekataa kuchapishwa jina lake halisi, anasema atakubali kuhojiwa ikiwa mwandishi atatumia jina la Zawadi, kwa ajili ya kufanikisha mazungumzo haya baina yake.   Anasema mtoto wake wa kike mwenye miaka 17, baada ya kumaliza masomo, huku akiwa na watoto sita wanaomtegemea, baada ya baba yao kufariki kwenye meli ya Mv. Spice, hakuwa na wasi wasi, kumtoa kwenda Oman. Anasema alimjia mtu ambae hamfamu, ingawa alimueleza kuwa, alikuwa karibu mno na marehemu mume wake, na hivyo baada ya kuzoea mno kwake, kisha alimuamini.   Ali