NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI 710, wakiwemo wanafunzi wa kike 663, sambamba na wasikilizaji 4,800 wa redio mbalimbali, wamefikiwa na elimu ya kisheria, haki za binaadamu, kupitia mradi uliokuwa ukiendeshwa na Jumuiya ya wasaidizi wa sheria Wete ‘WEPO’ hivi karibuni. Hayo yalibainishwa na Mratibu wa Uwezeshaji wa upatikanaji wa haki, kutoka ‘WEPO’ Rashid Hassan Mshamata leo Mei 10, 2026 skuli ya sekondari ya Utaani Wete, wakati wa mjadala wa wazi. Alisema, wapo waalimu na wazazi, wakimwemo wanawake 27 na wanaume 19, walifikia wakati wa utekelezaji wa mradi huo. Alieleza kuwa, kwa sasa matumaini yao, ni kuona jamii, imebadilika na waliokalia haki za wingine, sasa wanapata haki zao, kama sheria zilivyo. Alifafanua kuwa, kwa mfano waligundua ipo familia, ambayo, haijarithi kwa miaka 30 sasa, ambapo wanaume, wamekalia mirathi, jambo ambalo linaendelea kuwanyima haki wingine. ‘’Mradi huu, tulifanya shughuli kadhaa, lakini mafanikio yapo, maana hata wakati wa urushaji ...