TAMWA - ZANZIBAR YAWAPIGA MSASA WAANDISHI KUTIPOTI HABARI ZA UDHALILISHAJI MAENEO YASIO RASMI NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ MRATIBU wa Program ya Mradi wa kupambana na vitendo vya udhalilishaji wa "Tunaweza kwa pamoja kutokomeza vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia" kwa wanawake na wasichana unaotekelezwa na chama cha waandishi wa habari wanawake TAMWA -ZANZIBAR kwa kushirikiana na UN - WOMEN, Asia Hakim Makame amewataka waandishi wa habari kutumia taaluma zao kuielimisha jamii juu ya masuali mbali mbali ya udhalilishaji wa kijinsia kwa wanawake na wasichana. Alisema waandishi wa habari wanamchango mkubwa katika kutoa elumu ya kupinga vitendo vya udalilishaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto hususan katika sekta zisizo rasmini ikiwemo ya uchumi,elimu, afya na usafirishaji. Aliyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya uandishi wa habari hizo yaliojumuisha waandishi kutoka vyombo mbali mbali vya habari watakao tekeleza mradi huo ...