NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI wa shehia ya Mgogoni wilaya ya Chake chake, wameliomba Jeshi la Polisi mkoa wa kusini Pemba, kuharakisha upelelezi wao, ili kumbaini mtu aliyedaiwa kumbaka na kisha kumuua mwanamke mmoja wa kijiji hicho mwenye miaka 55. Wananchi hao walisema, kitendo alichitendewa mwananchi mwenzao, sio cha kiungwana na kinafaa kulaaniwa na kila mmoja, na kuliomba Jeshi la Polisi kuharakisha upelelezi wao. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, walisema wanasikitishwa mno na mzazi mwenzao, kufanyiwa kitendo hicho na kisha mwili wake, ukiwa hauna nguo kutelekezwa kichakani. Mmoja kati ya wananchi hao, Mohamed Juma Maalim, alisema kilichobakia kwa sasa pamoja na kushirikiana na Jeshi la Polisi, lakini wanalisubiri kuona upelelezi wao unazaa matunda gani. “Ni kitendo kinachoumiza hadi ndani ya miili yetu, kuona mtu aliyefanya kitendo hicho, hakuishia tu kwenye kumdhalilisha kingono, lakini kisha kuondoa uhai wake,’’alisema. Nae Khadija Mjaka Makame, alisema wali...