Skip to main content

Posts

Showing posts from March 13, 2022

WATAALAMU WA SHERIA WAIPA KAZI IDARA YA KATIBA NA MSAADA WA KISHERIA

                                   NA HAJI NASSOR, PEMBA WATAALAMU wa sheria Zanzibar, wameitaka Idara ya Katiba na Msaada wa sheria Zanzibar, kuongeza jitihada za elimu ili kusaidia kubadili mawazo, mitazamo na uwelewa wa watu maskini, ili kuongeza matumizi ya huduma za msaada wa kisheria.   Walisema, Idara inapaswa kuweka kipaumbele cha pekee cha kutoa mafunzo hayo, ili kuona walengwa wa mfumo wa kutoa elimu, ushauri na msaada wa kisheria ambao ni watu maskini wanafaidika nao. Kwa mujibu wa tafsiri ya ripoti ya tathmini ya awali ya hali halisi ya msaada wa kisheria Zanzibar ya mwaka 2020, iliyotolewa na wizara ya Katiba na sheria, walisema azma ya uwepo wa msaada wa kisheria ni kwa watu wasio na uwezo. Wataalamu hao kwenye ripoti hiyo walisema, suala la utoaji wa msaada wa kisheria linazingatiwa kuwa ni miongoni mwa viashiria vya msingi ya upatikanaji haki. Walieleza kuwa, taifa lolote lile duniani haliwezi kufurahia uwepo wa baadhi ya haki za binadamu bila ya kunawiri mfum

JAJI RABIA AWATAKA WANANCHI KUWALALAMIKIA WATUMISHI VISHOKA WA MAHKAMA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA WANANCHI kisiwani Pemba, wametakiwa kuitumia Kamati ya maadili ya watumishi wa mahakama, kwa kufikisha malalamiko yao pale wanapoona wamekwazwa kwa njia moja ama nyingine, na mtumishi yeyote wa mahakama. Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Jaji wa mahakama kuu Zanzibar, Rabia Hussein Mohamed, wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari, juu ya uwepo wa kamati hiyo. Alisema kwa wananchi waliopo Pemba, wanaweza kufikisha malalamiko yao kwa njia ya maandishi kwenye jengo la mahakama kuu Chake chake, na kisha kamati hiyo kuyasikiliza kwa kina. Alisema, kamati hiyo baada ya kusikiliza hupeleka mapendekezo kwa Jaji mkuu kwa ajili ya hatua nyingine za kinidhamu, kwa mujibu wa sheria na kanuni za utumishi wa umma. Jaji Rabia alieleza kuwa, kamati hiyo ambayo inaundwa na wajumbe watano, inalengo la kuona watumishi wa mahakama wanafanyakazi zao kama sheria na kanuni za utumishi zinavyoelekeza. Aidh Mwenyekiti alisisitiza kuwa, huu sio wakati te