Skip to main content

Posts

Showing posts from April 28, 2024

MADAKTARI WATAKIWA KUTOA HUDUMA BORA KWA WAGONJWA

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA    MADAKTARI na wauguzi wa kituo cha Afya shehia ya Pandani wameshauriwa kuendelea kutoa huduma bora za kimatibabu ili jamii iwe na afya njema.   Akizungumza mara baada ya kukabidhi taa katika kituo hicho, Mkaguzi wa shehia hiyo Inspekta wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba Khalfan Ali Ussi alisema, licha ya changamoto wanazokumbana nazo lakini hawana budi kujitolea katika kazi zao.   Alisema kuwa, ili jamii ipate maendeleo inahitaji watu wake wawe na afya njema kwa ajili ya kufanyakazi vizuri, hivyo ni vyema kwa madaktari kuendelea kutoa huduma bora kwa mgonjwa anaefika kituoni hapo kwa matibabu.   "Kwa kweli madaktari wanafanya kazi kubwa, hivyo tuendelee kujitolea kwa moyo safi ili jamii ipate huduma bora na afya njema," alisema Mkaguzi huyo.   Inspekta Khalfan aliwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa wafanyakazi wa kituo hicho kuhakikisha kinadumu kwa muda mrefu, kwani wao ndio walengwa wa kupatiwa huduma. &qu

USHIRIKA WA WANAWAKE SHUNGI CHAKE CHAKE WAANZA KUUWAGA UMASKINI WA KIPATO

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANACHAMA wa ushirika wa ‘ twaomba kheir’ wa wanawake wa kijiji cha Chanjamjawiri shehia ya Shungi wilaya ya Chake chake Pemba, wamekopeshana mikopo minane, yenye thamani ya shilingi 800,000 katika kipindi cha mwaka jana pekee. Wapo wanachama sita, waliokopa shilingi 100,000 kila mmoja na wawili kukopa shilingi 50,000, kwa ajili ya kutimiza malengo yao mbali mbali, ikiwemo kukamilishia ujenzi wa nyumba zao. Ushirika huo wenye wanachama 15, unasema kima hicho cha fedha walichokopeshana sio kidogo kwa wao, kutokana na hali zao za umaskini wa kipato ulivyokuwa hapo awali. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Mashika wa ushirika huo Sharifa Mohamed Khamis, alisema fedha hizo zilitokana na michango yao ya awali ya kila mwanachama, kujiwekea hisa ya shilingi 8,000 kwa mwezi, sawa na shilingi 2,000 kila mwisho wa wiki. Alisema kuwa, utaratibu huo ulianza tokea mwezi Septemba mwaka 2022, ambapo kwa mwezi, wanauwezo wa kukusanya shilingi 120,000 wast

WAANDISHI WATAKIWA KUANDIKA HABARI ZENYE KULETA MABADILIKO

  IMEANDIKWA NA KHAULAT SULEIMAN    WAANDISHI wa habari nchini wameshauriwa kutumia kalamu zao vizuri, ili kuleta mabadiliko ya kimaendeleo katika jamii.   Akizungumza katika mahafali ya pili kwa waandishi wa habari vijana (YMF) yaliyofanyika katika Ukumbi wa Bima Mpirani Mjini Unguja, Mjumbe kutoka TAMWA Zanzibar Shifaa Said Hassan aliwataka waandishi hao kujitahidi katika kazi zao ili kuwaletea mafanikio yao na jamii kwa ujumla.   Alisema kuwa, wandishi wa habari ni chachu ya kuleta maendeleo katika jamii, hivyo ipo haja ya  kutumia kalamu zao vizuri kwa kuandika habari za kuibua changamoto ili zipatiwe ufumbuzi kwa kwa maslahi ya jamii na Taifa.   "Kuna waandishi wanajitahidi sana kuandika habari na tunaona zinaleta mabadiko chanya kwa jamii, hivyo tuendelee kujitolea katika kuisaidia jamii yetu ili tufanikiwe," alisema.   Aidha aliwataka waandishi hao vijana kuwahamasisha wengine pindi zinapotokea fursa za mafunzo washiriki kikamilifu, ili  kupta elimu

WARIOBA: 'VYOMBO VYA HABARI VINAJUKUMU KUELIMISHA UMMA MASUALA YA UCHAGUZI, DEMOKRASIA'

    NA MWANDISHI MAALUM, DODOMA@@@@ VYOMBO vya habari vina dhima na jukumu la kusaidia katika kuimarisha demokrasia hususan katika kuelimisha umma masuala ya uchaguzi ili waweze kushiriki kwa ukamilifu katika uchaguzi na kuimarisha demokrasia ya ushiriki wa wananchi kwa ukamilifu. Akizungumza katika kongamano la wadau wa habari na uchaguzi Tanzania lillilofanyika leo April 30, 2024,   katika ukumbi wa hoteli ya Dodoma Waziri mkuu mstaafu Jaji Joseph Warioba alisema kuwa nguvu ya vyombo vya habari havina budi kutumika katika mchakato wa uchaguzi tokea kujiandikisha hadi kupiga kura ili kuimarisha shughuli hizo za uchaguzi. Jaji warioba alisema kuwa bado vyombo vya habari havikufanya kazi zake kwa ukamilifu   katika chaguzi zilizopita hivyo kuna haja ya kubadilika katika vyombo vyetu vya habari ili viweze kufanya kazi zake kwa ufanisi. “Vyombo vya habari vinatoa habari sio elimu na vinajikita zaidi katika matokeo na havifanyi utafiti”, alifafanua. Jaji Warioba alisema kuwa enzi

MJUMBE BARAZA KUU TAIFA UVCCM AWAITA VIJANA UCHANGIAJI DAMU

  NA ASHA ABDALLA, PEMBA@@@@  MJUMBE wa Baraza  kuu la  Taifa umoja wa Vijana CCM kusini Pemba,  Amriya Seif Saleh Amewataka vijana kuhudhuria kwa wingi katika kuchangia Damu salama  kila ifikapo muda kwani kufanya hivyo nikuondoa changamoto mbalimbali ambazo zinajitokeza kwa Mama Wajawazito na ajali mbalimbali zinapotokea. Ameyasema hayo leo 25/4 /2024 huko Uwanja wa Gombani Wiilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba  wakati walipokua  na zoezi  la uchangiaji Damu Salama ikiwa ni shamra shamra za maazimisho ya mika 60 ya Muungano wa Tanzania.  Alisema kua vijana ndio nguvu pekee katika kuendeleza Muungano katika nchi nao wana  uwezo mkubwa wa kuchangia Damu salama  hivyo nivyema kuhamasishana na kuhudhuria kwa wingi kwani kufanya hivyo ni umoja na mshikamano katika kuujali Muungano. "Ndugu zangu niwambieni kwa sasa changamoto ya damu imekua ni yakudumu kitaifa na kimataifa sio kuwa ni ya Tanzania pekeee bali ni yadunia mzima "Alieleza  Aidha aliwapongeza vijana wote na Wana

'CITIZEN BRIGED' PEMBA WAONESHWA WALIPO WANAWAKE WA KUANDALIWA KIUONGOZI

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ MWENYEKITI wa Bodi ya Jumuiya ya  Utetezi wa Mazingira na Jinsia Pemba  ‘PEGAO’ Alhajji-Amran Massoud Amran, amewashauri wahamasishaji jamii kudai haki zao za uongozi, demokrasia na siasa ‘Citizen bragged’ kisiwani Pemba, kuelekeza nguvu zao ngazi ya vyuo, ili kuwaibua wanawake wenye nia ya kugombea nafasi za uongozi. Alisema, wanafunzi wanawake ambao wanajitayarisha kuja kuitumikia jamii, wako katika skuli za sekondari na vyuo vikuu, hivyo ni vyema kwa wahamasishaji hao, sasa kuhamia katika eneo hilo kufanya uhamasishaji. Mwenyekiti huyo wa bodi, aliyasema hayo jana, alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi juu nafasi ya wahamasishaji jamii kutoka TAMWA, namna ya kuwaandaa wanawake kuwa viongozi katika nafasi mbali mbali. Alisema, wanawake walioko ngazi ya elimu ya sekondari na vyuo vikuu, ndio tegemeo kubwa kwa jamii, hivyo ikiwa watawezeshwa mapema, kuingia katika nafasi za uongozi, itakuwa rahisi kwao, baada ya kumaliza masomo. ‘’Kwanza nipongez

Waandishi Chipkizi Zanzibar wang’ara kwenye Mradi wa kuleta mabadiliko ya wanawake na Uongozi

  Zanzibar: Nihifadhi Issa. Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania -Zanzibar – TAMWA-Z kimekutana na waandishi wa Habari chipukizi,wahariri,wamiliki wa vyombo vya Habari na wadau wa Habari kwa kuwatunuku   na kuwatunza waandishi wa Habari 23 waliokuwa kwenye mradi wa Waandishi wahabari vijana. Mahafahali hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Bima uliopo Maisara Mkoa Mjini Magharib Unguja. Khairat Haji ni   Kaimu Afisa Programmu TAMWA -Zanzibar amesema katika hatua za kumarisha uongozi kwa wanawake    mradi   huu ambao hii ni awamu ya pili ambapo kwa awamu ya kwanza uliwafunza na kuwasimamia waandishi vijana 18 kwa 2022   akieleza kuwa mwaka 2023 waandishi vijana 24 walipata fursa katika mradi huu wa Wamawake na Uongozi”Kupitia mradi huu   ulikuwa unahitaji kazi 348 na hadi kufikia leo kazi hizo ni 347,huku magazeti 47 ,Makala za radio 117 huku Makala za mitandamo 187 ambazo zinakamilisha kazi 347” Amesema Khairat Shifaa Said ni Jaji Kiongozi wa Tuzo za Waandishi wa Habari