Skip to main content

Posts

Showing posts from October 5, 2025

UJENZI UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA PEMBA, BARABARA CHAKE CHAKE -MKOANI NJIA SAHIHI KUKUZA UCHUMI

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ILE dhamira ya Dk. Hussein Ali Mwinyi kuifungua Pemba kiuchumi kupitia uwanja wa ndege wa kimataifa, sasa imefana. Kwani uzinduzi wa ujenzi wa uwanja huo na barabara ya Chake Chake- Mkoani, umezinduliwa rasmi Septemba25, mwaka huu, katika uwanja wa ndege uliopo Furaha Pemba. Ni furaha kubwa kwa wananchi wa kisiwa cha Pemba, kuona kwamba kitu ambacho wamekisubiri kwa muda mrefu, sasa kinakwenda kufungua uchumi wao. Maana serikali ya awamu ya nane, imedhamiria kufanya mageuzi ya makubwa katika sekta ya usafiri wa anga Zanzibar, kwa lengo la kuimarisha miundombinu ya utoaji wa huduma katika uwanja wa ndege wa Pemba.   Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla amezindua ujenzi huo kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, jemedari wa uchumi.   Makamu huyo anasema, ujenzi wa miradi hiyo ni utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020/2025 ambapo malengo ya se...

TUME YA HAKI ZA BINAADAMU, YANGONGOMELEA MSUMARI KAMPENI JUMUISHI

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ TUME ya haki za binaadamu na utawala bora, ofisi ya Pemba, imetoa wito kwa vyama vya siasa   kuzingatia na kuhakikisha ushiriki wa watu wenye ulemavu katika mikutano ya kampeni zinazoendelea, kwa kuwawekea mazingira rafiki kwa kuzingatia aina zao za ulemavu. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Ofisini kwake Chake Chake Pemba, Afisa Mfawidhi wa tume hiyo Pemba Suleiman Salim Ahmad alisema, katika kuhakikisha ushiriki nzuri wa watu wenye ulemavu katika   upigaji kura, ni vyema ni vyema vyama vya siasa   kuhakikisha ujumuishi wao katika kampeni zinazoendelea. Alisema kwamba, mazingira mazuri kwa watu wenye ulemavu katika mikutano ya kampeni itasaidia kufuatilia sera zinazotolewa na wagombea wa vyama vya siasa katika nafasi za Urais, Uwakilishi, Ubunge na Udiwani, jambo litakalopelekea kuchagua viongozi wanaowataka kwa usahihi. Alisema kua, pamoja na jitihada mbali mbali zinazofanya na wadau   na watetezi wa haki za binaada...

NCHIMBI AONA MBALI MIAKA 5 IJAYO CCM IKIRUDI MADARAKANI

MGOMBEA MWENZA wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi CCM Dk. Emanuel John Nchimbi amesema, katika miaka mitano inayokuja wamedhamiria kuongeza kasi ya zoezi la utafiti wa rasilimali za bahari, ili wananchi wapate maisha bora, kwani uchumi wa buluu umeleta mafanikio makubwa katika nchi. Dk. Nchimbi ameyasema hayo wakati wa mkutano wa mkuu wa kampeni uliyofanyika katika viwanja vya Kinyasini Jimbo la Gando Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba. Amesema,  wanayo imani na matumaini makubwa kwamba ndani ya bahari kwa upande wa Pemba kuna rasilimali nyingi ambazo zitawasaidia wananchi kuwa na maisha bora, hivyo ilani ya CCM ya mwaka 2025/2023 imeweka wazi suala la kuongeza kasi ya zoezi la utafiti, ili kuimarisha zaidi uchumi wa wananchi. "Pia tutaimarisha ufungaji wa samaki, vizimba vya samaki na ukulima wa zao la mwani ili kuinua kipato cha wananchi na kuwaletea manufaa katika familia zao," alisema Dk. Nchimbi. Dk. Nchimbi alisema kuwa, anaamini kwamba chama kitap...

MTUMWA SULEIMAN: MGOMBEA UDIWANI ANAEPANIA KUMALIZA CHANGAMOTO

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@  "WANANCHI wa Wadi yangu wana upendo na mimi, nilipochaguliwa walinifurahia sana, hivyo sina wasiwasi na ushindi,"  Hayo si maneno ya mtu mwengine bali ni ya Mtumwa Suleiman Salum mwenye umri wa miaka 41 mkaazi wa Ole Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Mtumwa ambae ni mgombea udiwani Wadi ya Ole kupitia chama cha Mapinduzi CCM, anasema atakapofanikiwa kuchaguliwa atahakikisha wananchi wake wanafurahi zaidi, kwani atawashirikisha kila hatua ili kuona wanafanikiwa kwa haraka. Anaeleza, Wadi yake ni tofauti na nyengine kwani hata wananchi wa vyama vya upinzani wanampenda na kumuunga mkono, kutokana na kuwajali bila kuwabagua, hivyo anaimani atachaguliwa kuwa diwani wa Wadi hiyo. Wananchi wa Wadi yake walifurahi sana kuona kiongozi huyo mwanamke amepitishwa na wajumbe ili aweze kushika nafasi hiyo, kwani wanaamini kwamba, changamoto zao nyingi zitapatiwa ufumbuzi kipindi kitakachokuja. "Kwa kweli sina wasiwasi na nafasi hii na ...

JAMII YATAKIWA KUDHIBITI MABADILIKO YA TABIANCHI

   IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ MKURUGENZI wa Mwamvuli wa Asasi za Kiaraia Zanzibar (ANGOZA) Hassan Khamis Juma amesema, kutokana na maeneo mengi kuathiriwa na mabadiliko ya tabia nchi kisiwani Pemba, kuna haja kwa wadau kushirikiana pamoja katika kuhakikisha wanadhibiti hali hiyo katika jamii. Akizungumza wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau wa masuala ya mabadiliko ya tabia nchi katika Ukumbi wa Wizara ya Kilimo Pemba, Mkurugenzi huyo aliwataka kuyafanyia kazi mafunzo hayo kwa ajili ya kujenga mazingira bora ya sasa na baadae. Alisema kuwa, wamejikita kutoa mafunzo hayo hasa kwa wananchi wanaoishi maeneo ya ukanda wa bahari, ili kuelimisha jamii katika udhibiti wa mabadiliko ya tabia nchi ambayo yameathiri sehemu mbali mbali kisiwani hapa. "Tunaamini kwamba elimu hii tutaitumia ipasavyo katika kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi ili mulete mabadiliko chanya katika jamii," alisema Mkurugenzi huyo. Aidha aliwataka kufanya kazi vizuri ili wanajamii waelewe, ...

KHADIJA ANWAR: MGOMBEA ANAESAKA UWAKILISHI JIMBO LA WAWI

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ KHADIJA Anwar Mohamed mwenye umri wa miaka 40 mkaazi wa Wawi Mgogoni ni mwanamke shupavu mwenye ndoto ya kuwa kiongozi tangu akiwa mdogo. Aliamua kujiunga na chama cha CUF wakati huo ili kusudi apate nafasi ya kuwa kiongozi kwa lengo la kutatua kero za wananchi kwenye jamii iliyomzunguka. Mwaka 2000 Khadija alianza kupata nafasi za uongozi katika chama chake, ambapo alijiona tayari anaenda kutimiza ndoto zake alizokuwa akiziwaza mara kwa mara. Alianza kushika nafasi ya Mshikafedha wa tawi katika Jumuiya ya vijana na baada ya hapo ulifanyika uchaguzi kwenye chama na kufanikiwa tena kushika nyadhifa hiyo ya Mshikafedha lakini wa Jumuiya ya vijana kwenye jimbo. "Kwa vile lengo langu ni kuwa kiongozi na kuwatetea wananchi maendeleo, sikufikia hapo bali niliendelea kushika nyadhifa mbali mbali ndani ya chama changu mpaka nimefikia pale ninapopataka," anaeleza Khadija. Aliwahi kuwa Makamo Mwenyekiti mteule wa Kanda ya Pemba ambapo alikuwa anas...

UDP YAJA NA MPANGO WA KUIFUNGUA TANZANI KIUCHUMI IKIPATA RIHDAA

  NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ MGOMBEA Urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha United Democratic Party ‘UDP’ Saumu Hussein Rashid, amesema lengo la chama hicho ni   kufungua fursa za kiuchumi kwa kila mtanzania, ili aweze kujitosheleza kupitia biashara zao. Ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na wajasiriamali wa soko la Tibirinzi Chake chake Pemba alipokuwa akitoa sera ya chama hicho na kuomba kura kwa wafanyabiashara hao. Alisema   kuwa atahakikisha anakuza kipato cha watanzania, ili   kuifungua kiuchumi   kwa kila mjasiriamali, aweze kujitosheleza katika mahitaji yake. Alifafafanua kuwa atahakikisha anaweka miundombinu mizuri,   itakayowawezesha wajasiriamali wadogo wadogo,   ili waweze kuwa wafanyabiashara wakubwa kwa kuongeza pato lao. ‘’Niwambie wajasiriamali nina nia njema na ilani ya chama change ni kuwanyanyua kiuchumi, ili muwe wafanyabiashara wakubwa, muweze kujitosheleza katika mahitaji yenu,’’ alifafanua. Alielez...

VYAMA VYA SIASA TUMIENI MIFUMO SAHIHI SERA ZIWAFIKIE WATU WENYE ULEMAVU WA UZIWI

  NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@  TAASISI zinazoshughulikia masuala ya uongozi wa wanawake vimeviomba vyama vya siasa kuzingatia na kuhakikisha ushiriki wa watu wenye ulemavu katika mikutano ya kampeni zinazoendelea ili kuweza kufuatilia sera zinazotolewa na wagombea wa vyama vya siasa katika nafasi za Urais, Uwakilishi, Ubunge na Udiwani kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.  Taasisi hizo ambazo ni pamoja na Jumuiya ya Wanawake wenye Ulemavu Zanzibar (JUWAUZA), Jumuiya ya Mazingira, Jinsia na Utetezi Pemba (PEGAO), Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA) na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA-ZNZ) zimesema kuwa kuna baadhi ya vyama havijazingatia mahitaji ya watu wenye ulemavu katika mikutano yao jambo ambalo linawanyima haki yao ya msingi ya kufuatilia sera za vyama na hivyo kufanya maamuzi sahihi ya kura zao.   Walisema kuwa kuna baadhi ya vyama vimeshuhudiwa vikiendesha mikutano ya kampeni bila ya kuandaa mazingira rafiki kwa ...

LAILA: MWANAMKE SHUPAVU ANAYEANDIKA HISTORIA YA UONGOZI VISIWANI

NA AMRAT KOMBO, ZANZIBAR Kila binadamu ana malengo maishani, lakini kuyatekeleza kunahitaji mipango thabiti na ujasiri wa kipekee. Kwa Laila Rajab Khamis, maarufu kama Laila, ujasiri huo umekuwa silaha kubwa iliyomfikisha kwenye nyanja za siasa na kumuwezesha kuwa miongoni mwa wanawake wachache wanaopigania nafasi za juu za uongozi Zanzibar.  Laila alizaliwa mwaka 1968 Kengeja, Pemba, akiwa mtoto wa tatu kati ya watoto kumi wa familia ya Mzee Rajab. Elimu yake ya awali ilifika darasa la kumi katika Skuli  ya Uwelene. kabla ya kuingia kwenye siasa alikuwa mfanya biashara wa nguo mwaka 2000. Hata hivyo, ndoto yake haikuishia kwenye biashara pekee, bali kuandika historia ya uongozi kama mwanamke jasiri. Safari yake ya kisiasa ilianza rasmi mwaka 2008 alipojiunga na chama cha NCCR-Mageuzi na kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Jimbo la Rahaleo.  Hatua hiyo ilimfungulia mlango kushika nyadhifa mbalimbali ikiwemo Mjumbe wa Halmashauri Kuu, Mjumbe wa Kamati Kuu, Mlezi wa chama na hat...