IMEANDIKWA NA TATU MAKAME MAHUJAJI watarajiwa wameaswa kuacha kushughulikia simu wanapokuwa katika ibada ya Hijja, ili waweze kuitekeleza kwa utulivu, unyenyekevu na kupata radhi za Mwenyezi Mungu. Wito huo umetolewa na Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Ali Abdulghulam Hussein, wakati akifunga mafunzo kwa Mahujaji watarajiwa iliyofanyika katika Ukumbi wa Shantimba, Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja yaliandaliwa na Taasisi ya Khairat Hajj and Umra Travel. Alisema, ni muhimu kwa mahujaji kufuata miongozo wanayopewa na viongozi wa Hijja na kuepuka vitendo vinavyoweza kuharibu ibada hiyo, ikiwemo kutumia simu bila ulazima au kujihusisha na mambo yasiyo na tija. “Niwaase mahujaji watarajiwa msijishughulishe na mambo yasiyo na faida kama kuangalia michezo wakati wa ibada, hilo linaweza kuharibu utekelezaji wa nguzo ya tano ya Uislamu,” alisema Abdulghulam. Aidha, aliwataka kuwa wavumilivu katika kipindi chote cha ibada hiyo ili waweze kuitekeleza kikamilifu na...