NA MWANDISHI MAALUM, ZANZIBAR Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto leo Mai 07 imekaa kikao kazi na Benki ya Dunia kwa ajili ya kupitia mipango ya utekeleza ya Mradi wa Kukuza Usawa wa Kijinsia Tanzania- PAMOJA, unaotekelezwa na Wizara hiyo kwa Kushirikiana na Wakala wa Uwezeshaji KIuchumi (ZEEA). Akizungumza katika kikao kilichofanyika katika Ukumbi wa Mradi wa PAMOJA Kinazini, Unguja. Mkurugenzi Idara ya Mipango, Sera na Utafiti, Wizara ya Maendeleo, Jinsia, Wazee na Watoto Ndugu Daima Mohammed Mkalimoto amesema kilao hicho kimeleta tija kutokana na michango ya wadau iliyotolewa ili kuhakikisha utekelezaja wa Mradi unawanufaisha walengwa walikusudiwa wakiwemo wanawake na watoto. Ameeleza kwamba Mradi wa PAMOJA unalengo la kuwainua wanawake kiuchumi kupitia ZEEA, pia luwalinda na kuwahifadhi wahanga wa matukio hayo, hivyo Benki ya Dunia wametoa maelekezo kwaajili ya kuleta ufani. Naye Mratibu wa Mradi wa PAMOJA Ndugu Aisha Abbas Seif amesema k...