Skip to main content

Posts

Showing posts from February 11, 2024

MADIWANI WANAWAKE WANAVYOSIMAMIA VYEMA UWONGOZI

  NA  AMRAT KOMBO, ZANZIBAR@@@@ SIKU zote baadhi ya watu wanaimani ya kuwa, mwanamke bado ni mama wa nyumbani pekee. Ambae anatakiwa kuchunga familia yake tu peke yake, lakini bila ya kufikiri kuwa mwanamke anaweza kufanya mambo makubwa ya kuwasaidia jamii na kuleta maendeleo katika nchi. Ushahidi wa hili, sasa usiangalia tena Marekani na kwengineko, njoo kwa Rais wa Jamuhuri wa Muungano wa Tanzania, alivokuwa jasiri na mchapa kazi, katika nafasi yake ya uwongozi. Hivyo inaonesha kuwa, mwanamke sio mdhaifu kama watu wanavoona, hebu tuangalie baadhi ya viongozi mwanamke wanavyowajibika katika nafasi zao. Fatma R as hid Juma ni diwani wa   Chukwani Unguja, anasema kabla ya kushika nafasi hiyo, alikuwa mfanya biashara   mjasiria mali mdogo, huku akiwa mwanancha wa chama cha mapinduzi CCM. Anasema katika mwaka 2020, alijishirikisha katika kugombea udiwani wakiwa na wagombea wenzake 11, wakiwa wanawake watatu na wanaume nane, na kubahatika kutokea mshindi kwenye kinyanganyiro hi

KATIB ABEIDA ATOA TAARIFA YA MTOTO ALIYEKUWA AKIPIGWA NA MAMA YAKE

  Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto bi Abeida Rashid Aballah amesema mtoto Farhia Omar Mohamed (10) ambaye aliyekuwa anapigwa na mamaake wa kambo huko Bububu, Unguja hali yake inaendelea vizuri. Ameyasema hayo jana wakati alipomtembea mtoto huyo katika nyumba ya kulea watoto Mazizini, Unguja.   Bi Abeida amesema mtoto Farhia atapatiwa haki zake zote za msingi kama sheria ya mtoto inavyoeleza . Amefahamisha kwamba sheria ya mtoto sheria Na 2 ya mwaka 2011 imeainisha haki za mtoto ikiwemo haki ya kupata elimu, matibabu, kuishi, nk.   Ameeleza ni wajibu wa Wizara ya Maelendeleo ya Jamii , Jinsia , Wazee na Watoto kusimamia utekelezaji wa sheria hiyo kwa maslah ya taifa.   Aidha katibu Mkuu Abeida ametoa wito kwa wazazi na walezi kutumia busara zaidi wakati wa kumuadhibu mtoto endapo amefanya kosa, kwani ikumbukwe kwamba mtoto ni wa Serikali hivyo, Serikali haitovumilia kuona mtoto anafanyiwa vitendo vya udhalilishaji wa aina yeyote ikiwemo kupigwa, kunyanya

SHEHA SHUNGI: ‘CHIMBENI MASHIMO SALAMA KUHIFADHIA MAJI TAKA’

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ UONGOZI wa shehia ya Shungi wilaya ya Chake chake Pemba, umewataka wananchi, ambao bado hawajachimba mashimbo ya kuhifadhi maji taka, kufanya hivyo haraka, ili kuzuia uwezekano wa kukumbwa na magonjwa ya mripuko. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi shehiani hapo, Sheha wa shehia hiyo Hamad Ramadhan Soud, alisema shehia haitomvumilia mwananchi yeyote, anetiririshaji maja taka, kwani athari yake inaweza kuenea kwa shehia nzima. Alisema, kila mwananchi ahakikishe amechimba shimo maalum na kisha kulifunika vyema, ili kuhifadhi maji anayotumia kutoka nyumbani mwake, badala ya kuyaacha yasambae. Alieleza kuwa, maji yanayotumiwa hata kwa kukoshea vyombo au kukogea chooni, ndio chanzo cha magonjwa kama matumbo ya kuharisha damu, kipindu pindu na minyoo. Sheha huyo alieleza kuwa, amekuwa akitoa elimu hiyo kila muda kwa wananci wake, ili kuona wanajikinga na magonjwa mbali ambayo yanaweza kusababishwa na maji taka. ‘’Niwatake wananchi wangu, haraka sana

UGONJWA WA ‘RED EYES’ WAKWAMISHA KESI DAWA ZA KULEVYA PEMBA

    NA MARYAM NASSOR, PEMBA@@@@       KESI ya kupatikana na dawa zinazoaminika kuwa ni za kulevya, iliyopo mahakama kuu Zanzibar, kanda ya Pemba, imeshindwa kuendelea, baada ya shahidi nambari moja, ambae ni Mkemia kushindwa kufika   mahakamani hapo, kwa   udhuru wa   ugonjwa wa ‘RED EYES’.   Awali, ilidaiwa mahakamani hapo kuwa, mtuhumiwa katika shauri hilo, Omar Khatibu Juma, alikutwa na misokoto 700 yanayosadikiwa kuwa ni dawa za kulevya   aina ya bangi, yenye uzito wa gramu 2836.75, eneo la Machomane wilaya ya Chake chake. Mara baada ya kufika mahakamani hapo, mtuhumiwa akiwakilishwa na wakili wake Zahran Mohamed Yussuf aliambiwa   na upande wa mashtaka ulioongozwa na Mwendesha mashtaka kutoka Afisi ya Mkurugenzi wa mashtaka, Mohamed   Ali Juma, kuwa walikuwa wanategemea kupokea mashahid watatu.   Alidai kuwa, kesi hiyo ipo kwa ajili ya kusikilizwa,   na wamepokea mashahidi wawili, kati ya watatu waliyoitwa, ingawa shahidi nambari moja ambae ni Mkemia, hajafika mahakaman

MITAZAMO INAVYOCHANGIA WANAWAKE KUTOGOMBEA UONGOZI.

     NA AMRAT KOMBO, ZANZIBAR @@@@ Wapo wanawake ambao wanao uwezo mkubwa wa kuwa viongozi, lakini baadhi ya mitazamo katika jamii inawarudisha nyuma na kuamua kukaa pembeni. Kwa bahati mbaya mitazamo hii,   inahusishwa na maelekezo ya dini kutokana na tafsiri potofu inayotolewa na badhi ya watu juu ya maelekezo ya dini na kuonekana kwa kiasi fulani.   Hata utekelezaji wa mikataba ya kikanda na kimataifa juu ya haki na nafasi za wanawake, ikiwa pamoja na katika uongozi, ambayo nchi yetu imeiridhia inatekelezwa kwa kuchechemea au kufumbiwa macho kwa visingizio mbali mbali. Miongoni mwa mikataba inayohimiza kulindwa kwa haki za wanawake ni tamko la kimataifa kuhusu haki za binadamu la 1948 ambao umelenga kutokomeza aina zote za kuwabagua   wanawake. Kifungu cha pili cha Mkataba wa Afrika juu ya haki za binadamu,inajumuisha kanuni yakutobagua kwa misingi ya rangi, kabila ,jinsia ,lugha,dini,siasa au maoni mengine yoyote. Zanzibar inayo idadi kubwa ya waumini wa dini ya Kiislam

WANAWAKE WENYE ULEMAVU SHUNGI WATAKA NAFASI ZA UONGOZI

    NA ZUHRA JUMA, PEMBA@@@@ UONGOZI wa Kamati ya kutetea haki za watu wenye ulemavu shehia ya Shungi wilaya ya Chake chake Pemba, imesema wakati umefika sasa, kwa wanawake wenye ulemavu, nao kupewa nafasi za uongozi, kwani ni haki yao kikatiba. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Katibu wa kamati hiyo, Asha Mohamed Yussuf, alisema bado wanawake wenye ulemavu, hawaonekani kuwa wanaweza kuongoza, jambo ambalo sio sahihi. Alisema, kelele zinazopigwa juu ya wanawake na uongozi, hazijawangalia wanawake wenye ulemavu, jambo ambalo wao kama wanaharakati linawarejesha nyuma. Alifafanua kuwa, wanawake wenye ulemavu wanauwezo mkubwa wa kuongoza iwe nafasi za usheha, kwenye vikundi vya kijamii, ukuu wa wilaya na hata ngazi ya urais, ingawa changamoto ni kukosa watetezi. ''Wanawake na wanaume wana haki sawa za kuongoza, lakini maandiko na maazimio kadhaa iwe ya kikanda na kimataifa, hajamuangalia mwanamke mwenye ulemavu,''alieleza. Katika hatua nyingine, alisema kazi inayof

WAZIRI SULEIMAN ASHAJIISHA UTOAJI MAONI SERA MAMBO YA NJE

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu Zanzibar Ali Suleiman Ameir amewataka wananchi na wadau mbali mbali kutumia fursa ya kutoa maoni kwenye rasimu ya sera mpya ya mambo ya nje, ili kujenga sera madhubuti ambayo ni dira ya maendeleo itakayowanufaisha kijamii, kisiasa na kiuchumi. Akizungumza katika kongamano la kukusanya maoni kuhusu marekebisho ya sera hiyo ya mwaka 2001 alisema, Serikali imeelelekeza kushirikishwa wadau ili kuwezesha kupata sera madhubuti itakayoboresha. Alisema kuwa, ni muhimu kwa wadau kuunda sera madhubuti ambayo italiwezesha Taifa hili kunufaika ipasavyo na kukuza ushirikiano baina ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mataifa mengine duniani. "Tayari tumeshafanya makongamano haya katika mikoa mengine na sasa tunaendelea, haya yanalenga kupata sera yenye tija ambayo itakidhi matarajio ya wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania," alisema. Kwa upande wake Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk alise