NA MARYAM SALIM, PEMBA@@@@ KUTOKUFIKA kwa mtuhumiwa Zaid Mussa Zaid miaka (46) mkaazi wa Machomanne pamoja na wakili wake katika mahakama ya Mkoa ‘C’ Chake Chake Pemba, kumepelekea shauri hilo kuahirishwa mahakamani hapo na kupangwa tarehe nyengine kwa ajili ya utetezi . Mapema Mwendesha mashitaka akiwakilisha Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka wa serikali, Kheir Hassan Omar, aliieleza mahkama hiyo mbele ya Hakimu Hamisuu Saadun Makanjira kwamba, shauri hilo lilifikishwa katika mahakama hiyo, kwa ajili ya utetezi ingawa mtuhumiwa na wakili wake, hawakuhudhuria. "Mheshimiwa Hakimu, shauri lilimefikishwa mahakamani kwa ajili ya kusikilizwa utetezi, ambalo linamkabili mtuhumiwa Zaid Mussa Zaid, anaedaiwa kupatikana na dawa za kulevya. "In...