Skip to main content

Posts

Showing posts from February 15, 2026

KUCHELEWA KUHAMIA WAJASIRIAMALI KITUO CHA MICHAKAINI, WALIKOSESHA BARAZA LA MANISPAA MILIONI 100

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ SHILINGI milioni 107,190,000 zilizotarajiwa kukusanywa na Baraza la Manispaa Chake chake Pemba, kuanzia mwezi Novemba, 2023 hadi Januari mwaka huu, hazikupatikana, baada ya wajasiriamali kugoma kukitumia kituo chao cha Michakaini, kwa wakati.   Imebainika kuwa, kituo hicho kipya kilichojengwa kwa ajili yao, kina milango 63 ya maduka, ambapo kila mmoja Baraza lilikusudia kuukodisha kwa shilingi 50,000 ili lijipatie shilingi milioni 3,150,000 kwa kila mwezi mmoja. Ingawa imebainika, baada ya wajasiriamali hao kukataa kuingia kituoni humo, Baraza hilo, kuanzia mwezi Novemba, 2023 hadi Januari mwaka huu, limeshapoteza shilingi milioni 85,050,000. Aidha mapato ya shilingi ya milioni 22,140,000 nayo hayakukusanywa na Baraza hilo kwa kipindi hicho, yaliokuwa yatokane na vizimba ‘ vikuta ’ 82, ambapo kila kimoja, kilitarajiwa kukukodishwa kwa shilingi 10,000 kwa wajasiriamali. Ikafahamika kuwa, vikuta hivyo kama vyengepata wajasiriamali, kw...

THBUB YAFIKA DUNGA KUWAPA ELIMU YA HAKI ZA BINAADAMU WANANCHI

  NA MWASHAMBA JUMA, (THBUB)@@@@ Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, THBUB ofisi ya Zanzibar, imewajengea uelewa mpana wanakijiji wa Dunga Kiembeni kuhusu masuala ya uvunjifu wa haki za binadamu na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora. Akizungumza na wanakijiji hao kwenye mkutano wa pamoja baina ya Tume na wananchi wa Shehia ya Dunga Kiembeni iliopo Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja, Afisa Sheria wa THBUB Bw. Wilfred Msagati aliwahimiza wananchi hao kutambua haki zao na kuzipambania pale zinapovunjwa. Sambamba na kuwaelekeza kufika Tume kwa lengo la kuwasilisha malalamiko yao endapo watakupamba na masuala ya uvunjwaji wa haki na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora. Wilfred aliyasema hayo wakati akiwasilisha mada ya “Majukumu ya THBUB” kwa wanajijiji hao pamoja ya kuwaelimisha haki mbalimbali ambazo binaadamu zinamstahikia na kumuwajibikia huku akiwafahamisha jinsi ya Tanzania ilivyoridhia mikataba ya kimataifa kutekeleza haki za binadamu zikiwemo haki za watoto...

UN-WOMEN YAAHIDI KUENDELEA KUFANYAKAZI NA FAWE-ZANZIBAR

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ SHIRIKA la Umoja wa mataifa la UN-Women, limesema litaendelea kufanyakazi na taasisi ya FAWE Zanzibar, kwa maslahi ya kuwasaidia wajasiriali wa mazao, yanayolimwa baharini na nchi kavu. Hayo yameelezwa jana Febuari 17, 2026 na Mwakilishi wa shirika hilo upande wa Tanzania Emile Kivugo Mwakafundu, alipokuwa akiwasalimia wajasiriamali, wanaoendelea na mafunzo ya mnyonyoro wa thamani, yanayofanyika kituo cha elimu mbadala Wingwi Micheweni Pemba. Alisema UN-Women ni mdau mkuu wa maendeleo ya jamii, wakiwemo wajasiriamali wa uzalishaji muhogo, majongoo bahari, mwani pamoja na wakulima wa migomba, ili kuziongezea thamani biadhaa hizo. Alisema, shirika hilo linawajali wajasiriamali hao, ili kuhakikisha wanaziongezea thamani bidhaa zao kwa lengo la kukuza pato lao. Alieleza kuwa, haiwezekani kwa mkulima, baada ya kuvuna mazao yake, kwenda kuyauza sokoni kama yalivyo, bali ni kuyachakata, ili aongeze pato lake. ‘’UN-Women inaendesha maradi huu ...