Skip to main content

Posts

Showing posts from February 26, 2023

UFUNGUZI WA IJITMAI PEMBA: WAISLAM WAKUMBUSHWA KUISHI KWA AMANI

  JUMA MUSSA, PEMBA. WAUMINI wa dini ya Kiislam wametakiwa kuishi kwa kuendana na malengo  ya Qur- an  ili kupata amani , maendeleo na  salama hapa ulimwenguni  na Akhera siku ya malipo. Afisa Mdhamini Tume ya Mipango Pemba Khamis Issa Mohamed aliyasema hayo Machi 3, 2023  kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba Matar Zahor Massoud Ole  Kianga  katika ufunguzi wa Ijitimai ya 24 ya Kitaifa inayofanyika  Kisiwani Pemba. Alisema bila kuwepo  umoja, maadili mema na mshikamano hakuna  maendeleo  yatakayopatikana kutokana na umma kuwa na fadhaa jambo ambalo  linatokana na kusahau maamrisho ya dini yao. “ Tusifichane ndugu  zangu waislamu bila ya nchi kuwa na amani  hakuwezi kupatikana maendeleo kwani kila mmoja atakuwa anapigania uhai  wake na hatimae hata kufanya Ibada jambo ambalo tumeletewa hapa u limwenguni tutakuwa muda hatuna hivyo tutakuwa na makosa mbele ya  Allah (S.W.T)”, alisema. Alifahamisha kuwa ili amani na utulivu wa nchi uweze kudumu ni wajibu  wa kila mmoja ni kutekeleza m

MILELE, OFISI YA DC: CHAKE CHAKE ZAPEWA TANO KUCHUNGUUZA AFYA ZA WANAFUNZI PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ AFISA Mdhamini wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Pemba, Zuhura Mgeni Othman, amesifu zoezi la awali la utambuzi wa ulemavu, kwa wanafunzi wa darasa ya kwanza wa skuli za Birikau na Michakaini, lilioendesha na Milele Zanzibar Foundation, kwa kushirkiana na ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Chake chake. Alisema zoezi hilo, ndio ambalo litawaibua mapema wanafunzi wenye magonjwa mbali mbali pamoja na wale wenye ulemavu, na kuanza matibabu mapema. Afisa Mdhamini huyo, aliyesema hayo skuli ya Michakaini, wakati akilifunga zoezi hilo la siku nne, ambalo liliwafikia wanafunzi zaidi ya 500 kwa skuli hizo. Alieleza kuwa, upo baadhi ya aina ya ulemavu unaweza kupona na kumuacha mtoto akiwa salama, kama hali hiyo itatambulika mapema, kama ilivyofanya Milele chini ya ofisi ya watu wenye ulemavu ya wilaya ya Chake chake. Alifafanua kuwa, msingi mkuu wa mwanafunzi kuweza kusikiliza kwa umakini, kupata ufahamu na kufikia lengo lake akiwa masomoni, afya njema na imara ni

TAMWA-ZANZIBAR YAPIGA MARUFUKU MICHEZO HATARISHI KWA WANAFUNZI-PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA::: WANAFUNZI wa skuli za msingi za Madungu na Michakaini wilaya ya Chake chake, wametakiwa kuacha mara moja aina yote ya michezo, inayoashiria kukamatana sehemu za siri, ukiwemo unaoitwa ‘cheni dole’. Hayo yameleezwa na Mratibu wa Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba Fat-hya Mussa Said, wakati akizungumza na wanafunzi, kwenye kampeni maalum ya kuongeza uwelewa, kwa wanafunzi wa skuli, madrassa, vyuo vikuu na klabu za sanaa. Alisema, ipo michezo katika skuli na madrassa inayofanywa na wanafunzi wa kike na kiume, ambayo mingi inaelekeza namna ya kukamatana, maeneo yao ya siri ikiwemo makalio. Mratibu huyo alieleza kuwa, michezo hiyo na mengine husababisha wanafunzi, kufukuzana hadi kichakani, na kisha kuanza kufanyiana vitendo viovu. ‘’Kuanzia leo michezo kama cheni dole, cheni saluti, nichum kwanza na nishike, iwe marufuku kwa watoto wote, kwani inaashiria udhalilishaji,’’alifafanua. Katika hatua nyingine Mrati

WIZARA YA ARDHI ZANZIBAR KUWANYANG'ANYA ARDHI WOTE WALIOSHINDWA KUZIENDELEZA

  Na Sabiha Keis::: Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imesema itawanyang'anya umiliki wa ardhi wanyenji na wageni ambao walipewa kwa ajili ya kuekeza lakini wameshindwa kuyaendeleza   hivyo sheria itachukua mkondo wake bila ya kumonea mtu muhali. Kauli hiyo imetolewa na Naibu waziri wa Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanzibar Juma Makungu Juma huko Wilaya ya kati Mkoa wa Kusini Unguja katika ziara maalumu ya kuyatembelea maeneo ambayo wageni na wenyeji walipewa kwaajili ya kuekeza lakini bado hawajaekeza. Alifahamisha kwamba sheria ya Umiliki wa Ardhi, sheria Nam: 12 ya mwaka 1992 kifungu Nam 48 (1a) kinaeleza ukiukaji wa ukodishwaji ardhi (Violetion of the Restrictions in a lease) hivyo wizara yake itahakikisha inafata sheria kwa wawekezaji wakigeni na wazawa ambao walipewa maeneo kwa ajili ya uwekezaji na kutoyaendeleza kwa muda uliowekwa. Alifahamisha kwamba lengo la ziara yake ni kuangalia pamoja na kuyatambua maeneo yote ya ardhi ambayo yametolewa na Serikali na k

MILELE ZANZIBAR FOUNDATION, OFISI YA DC: CHAKE CHAKE WAENDESHA ZOEZI LA UCHUNGUUZI KWA WANAFUNZI

      NA HAJI NASSOR, PEMBA:: WANAFUNZI wa skuli Pondeani na Michakaini wilaya ya Chake chake, wameanza kufanyiwa vipimo vya aina tofauti, ikiwa ni pamoja na usikivu, zoezi linaloendeshwa na Milele Zanzibar Foundation kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa wilaya hiyo, kupitia Ofisi ya watu wenye ulemavu wilayani humo. Akizungumza kwenye zoezi hilo skuli ya Michakaini msingi wilaya ya Chake chake, Afisa miradi Idara ya afya kutoka taasisi hiyo Mohamed Abdalla Rashid, alisema Milele imekuwa ikijali mno afya za jamii. Alisema, lengo la zeozi hilo ni kuangalia afya za watoto walioko skulini, ili kuwagundua mapema, hasa katika eneo la uoni, usikivu na kisha kupatiwa matibabu. Alieleza kuwa, katika zoezi hilo limewashirikisha wataalamu wa koo, maskio na macho, kwa lengo la kuwafanyia uchunguuzi kwa kina na kisha kufikishwa hospitali kwa huduma zaidi. Afisa huyo alieleza kuwa, zoezi hilo linaumuhimu mkubwa kwa mustkbali wa ukuaji wa watoto, kwani wakati mwengine wanaweza kugundua t

MDAU WA AMANI AKUNWA MIKAKATI YA KUIMARISHA AMANI ZANZIBAR

    NA HAJI NASSOR, PEMBA::: MDAU wa amani Abubakar Kabogi, amesema dunia inavutiwa mno na juhudi za serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kusimamia amani nchi. Alisema, dunia imekuwa ikifuatilia kwa karibu mno namna serikali inavyohamasisha utunzaji wa amani na utulivu, iwe kabla, baada ya uchaguzi au wakati wa uchaguzi mkuu wa vyama vingi. Mshauri huyo wa masuala ya amani barani Afrika aliyasema hayo ukumbi wa Samail Gombani Chake chake wakati akisalimiana na mabalozi wa amani kisiwani humo. Alisema, bado wadau wa ndani na wale wa kimatifa wanaendelea kuunga mkono juhudi za mabalozi hao pamoja na serikali kwa ujumla, katika mradi wa amani yangu, ambao upo Tanzania kwa muda mrefu. Mdau huyo alieleza kuwa, bado mabalozi hao wanawajibu wa kuendelea kufanyakazi kwa karibu na serikali yao, ili kuhakikisha amani iliyopo Zanzibar inaendelea kudumu. ‘’Visiwa hivi ni vizuri na ni sehemu yenye utulivu kuishi, hii ni kwa sababu ya kuwepo kwa amani ya kudumu,’’alieleza Abubakar.