Skip to main content

Posts

Showing posts from February 4, 2024

KAZI 529 ZA WAANDISHI WA HABARI ZASHINDANISHWA KUWANIA TUNZO ZANZIBAR

  NA NAFDA HINDI, ZANZIBAR JUMLA ya kazi 529 za waandishi wa habari zimewasilishwa TAMWA kwa ajili ya kuwania tuzo za umahiri za uandishi wa habari za takwimu za wanawake na uongozi. Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania Zanzibar, (TAMWA – ZNZ), Dkt. Mzuri Issa,amesema miongoni mwa kazi hizo ni pamoja na vipindi vya redio, televisheni, makala za magazeti na kutoka katika mitandao ya kijamii zilizoandikwa na kurushwa katika vyombo vya habari kuanzia mwezi Januari hadi Disemba 31, 2023. Dk Mzuri amesema lengo la tuzo hizo ni kuhimiza waandishi wa habari kutumia kalamu zao na vyombo vya habari kuelimisha umma kuhusu umuhimu wa masuala ya wanawake katika uongozi na kuongeza ushiriki wa wanawake katika ngazi mbalimbali za maamuzi. “Kazi hizo zinaonesha ni jinsi gani waandishi wamekuza mwamko wa kuandika habari za uongozi kwa wanawake ambapo zinashajihisha wanawake na vijana wakike kujiamini zaidi na kuwa na matumaini ya ku

AFISI YA MWANASHERIA MKUU ZANZIBAR: 'WANANCHI ANDIKENI, WASILISHENI MAMALAMIKO YANEU KWETU'

  Na Faki Mjaka-AMM-ZANZIBAR@@@@ Wakili wa Serikali Mkuu kutoka Afisi ya Mwanasheria Mkuu Zanzibar Hamisa Mmanga Makame amewaomba wananchi wenye Malalamiko na kadhia mbali mbali kuandika malalamiko hayo na kuyawasilisha katika Afisi ya Mwanasheria Mkuu ili kusaidiwa kupata ufumbuzi.   Amesema katika Afisi yao lipo Faili maalum kwa ajili ya malalamiko ya Mwananchi yeyote ili pale anapoyawasilisha, Afisi iweze kuyafanyia kazi malamiko hayo.   Wakili Hamisa amesema hayo wakati akizungumza na Wananchi wa Mangapawani Mkoa wa Kaskazini Unguja wakati Afisi ya Mwanasheria Mkuu ilipoenda kutoa elimu ya masuala mbali mbali ya kisheria kwa wananchi hao ikiwa ni shamra shamra ya wiki ya sheria Zanzibar.   Amefahamisha kuwa, pale Mwananchi atakapoandika malalamiko yake dhidi ya Taasisi yoyote ya kiserikali, Afisi ya Mwanasheria Mkuu huchukua jukumu la kuwaita walalamikiwa kwa lengo la kutafuta suluhu dhidi ya malalamiko hayo.   “Mwananchi anapoandika malalamiko yake, sisi tunampa ushauri wa kitaala