Skip to main content

Posts

Showing posts from April 26, 2026

WAZIRI PEMBE: SHERIA MPYA YA HABARI ZANZIBAR KUTINGA BARAZANI MWAKA HUU

    NA HAJI NASSOR@@@@ WIZARA ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Zanzibar, imesema katika Baraza la Wawakilishi linalotarajiwa kuanza wakati wowote, sheria mpya ya habari, itasomwa kwa mara ya kwanza.   Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa wizara hiyo Riziki Pembe Juma, jana Mei 2, 2026 hoteli ya Madinatul-Bahar iliyopo nje kidogo ya mji wa Unguja, kwenye hafla ya utoaji tuzo, kwa waandishi wa habari za takwimu, kuhusu wanawake na uongozi.   Alisema, tayari kila kitu kimeshakaa sawa na kinachosubiriwa, ni kufika kwa siku ya kuanza kwa kikao cha Baraza hilo, na mswada huo kusomwa.   Alisema, wizara imeshakamilisha taratibu zote, na sasa wadau wa sheria hiyo wakiwemo waandishi wa habari, wafuatilie Baraza la Wawakilishi lijalo.   ‘’Najua mliowengi mnahamu ya kutaka kusikia, kuhusu nini wizara imefikia, juu ya sheria mpya ya habari, lakini niwaarifu kuwa, itapelekwa Barazani mwaka huu wa 2026/2027,’’alifafanua.   Katika eneo ji...

JE WAVIJUA VIFUNGU VYA KANUNI YA UTUMISHI WA UMMA AMBAVYO SIO MAARUFU KWA WATUMISHI?

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ SIKUKUU ya wafanyakazi duniani, ni kumbukumbu ya mauaji ya halaiki ya mwaka 1886, yaliyotokea katika viwanja vya Haymarket, Chicago nchini Marekani.   Taarifa za mitandao zinaeleza kuwa, Polisi walikuwa wakitawanya mkusanyiko wa wafanyakazi, wakati wa mgomo wa kupinga saa nane za kazi.   Papa Pio XII kunako Mei Mosi, ya mwaka1955 akamteua Mtakatifu Yosefu, kuwa tegemeo, mfano na mwombezi wa wafanyakazi wote duniani. Aliaminika kuwa, ndie atakayewasaidia kusimama kidete, kulinda na kutetea haki zao, ili kujenga na kudumisha utu, heshima, haki msingi. Mitandao inaendelea kuripoti kuwa, jumuiya ya kimataifa, inaadhimisha sikukuu ya wafanyakazi, lengo ni kuhamasisha utoaji wa haki msingi kwa wafanyakazi wote. Mei mosi, ni siku maalum ya kuonesha umoja na mshikamano kati ya wafanyakazi, sanjari na kuhimiza usawa na haki, katika maeneo ya kazi, sehemu mbalimbali duniani. Kwa Tanzania, nayo mwaka 20...

MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR WATIMIZA MIAKA 62, WAWAPA FAIDA YA UONGOZI WANAWAKE ZANZIBAR

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ TAIFA la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, sasa limo kwenye shamra shamra ya kusherehekea siku yake za kuzaliwa ‘birthday ’. Taifa hili ambalo liliasisiwa mapema Aprili 26, mwaka 1964, kwa wasisi, kuchanganya udogo kama ishara ya kuunganisha nchi mbili na kuwa na taifa moja. Maana kabla ya Muungano huo, tusema chini ya mwaka 1963, Zanzibar ikijulikana kama Jamhuri ya watu wa Zanzibar, ambapo baada ya Muungano huo, taifa jipya sasa limezaliwa, nalo ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Yapo malengo mablimbali yaliosababisha hata waasisi wetu, Julias Kambarage Nyerere kwa Tanzania bara na Sheikh Abeid Amani Karume kwa Zanzibar, yaliowasukuma kuungana. Moja wapo ni kuimarisha uhusiano wa umoja wa kitaifa, sambamba na kutanua fursa za uongozi, kwa nchi mbili hizi, ikiwa ni pamoja na kitaaluma, uongozi na biashara. Na ndio maana katika safu ya uongozi, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekuwa ikitanua wigo wa uongozi kwa wazanzibari, amb...