Skip to main content

Posts

Showing posts from April 26, 2026

MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR WATIMIZA MIAKA 62, WAWAPA FAIDA YA UONGOZI WANAWAKE ZANZIBAR

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ TAIFA la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, sasa limo kwenye shamra shamra ya kusherehekea siku yake za kuzaliwa ‘birthday ’. Taifa hili ambalo liliasisiwa mapema Aprili 26, mwaka 1964, kwa wasisi, kuchanganya udogo kama ishara ya kuunganisha nchi mbili na kuwa na taifa moja. Maana kabla ya Muungano huo, tusema chini ya mwaka 1963, Zanzibar ikijulikana kama Jamhuri ya watu wa Zanzibar, ambapo baada ya Muungano huo, taifa jipya sasa limezaliwa, nalo ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Yapo malengo mablimbali yaliosababisha hata waasisi wetu, Julias Kambarage Nyerere kwa Tanzania bara na Sheikh Abeid Amani Karume kwa Zanzibar, yaliowasukuma kuungana. Moja wapo ni kuimarisha uhusiano wa umoja wa kitaifa, sambamba na kutanua fursa za uongozi, kwa nchi mbili hizi, ikiwa ni pamoja na kitaaluma, uongozi na biashara. Na ndio maana katika safu ya uongozi, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekuwa ikitanua wigo wa uongozi kwa wazanzibari, amb...