NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAKIKUNDI cha ufugaji wa majongoo bahari, ‘ tumuombe mola’ cha Makangaale wilaya ya Micheweni Pemba, wanatarajia kujipatia shilingi milioni 20 mwishoni mwa mwaka huu, ikiwa watafanikiwa kuuza bidhaa hiyo, baada ya kuekeza vifaranga vyenye thamani ya shilingi million 1.6 mwaka jana. Fedha hizo, ni uwekezaji wa vifaranga 3,300 vya majongoo habari, walivyovinunua kwa shilingi 1,650,000 wastani wa shilingi 500 kila kifaranga kimoja, chenye urefu kati ya nchi nne hadi tano. Wanakikundi hao cha ‘ tumuombe mola ’ wamesema kati ya vifaranga hivyo, wanatarajia kuvuna majongoo yaliokwisha pevuka 2,500 na kisha kila moja kuliuza kwa bei ya shilingi 8,000 na kujipatia shilingi milioni 20. Mwenyekiti wa kikundi hicho Hator Hassan, alisema haiwezekani kuotesha vifaranga vya idadi 3,300 kisha kuvuna kama ilivyo. ‘’Zipo changamoto kama za kufa na hasa wakati wa usafirishaji wa vifaranga kutoka eneo moja kwenda kwenye bwawa lao, wizi na wingine kufa kabla ya kufikia k...