Skip to main content

Posts

Showing posts from November 13, 2022

ZIJUWE HAKI ZA MUAJIRIWA ZISIZOTANGAAZWA KWA KINYWA KIPANA NA MUAJIRI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA::: KANUNI ya Utumushi wa Umma ya Zanzibar ya mwaka 2014, imeundwa na vifungu wastani wa 134. Kanuni hii, ni zao la sheria ya Utumishi wa Umma ya Zanzibar, ambayo nayo ilitungwa na Baraza la Wawakilishi, kwa lengo la kubainisha na kuweka wazi haki, wajibu wa watumushi wa umma. Kanuni hii, imekuja kufafanua na kuweka taarifa kwa upana zaidi kwa watumishi wa umma wa Zanzibar, ili kuongeza kasi, ari, hamasa na juhudi za kuwahudumia wananchi. Kanuni hii ya utumushi wa umma ambayo ilisainiwa Mei, 29 mwaka 2014 kazi iliyofanywa na aliyekuwa Waziri wa nchi ofisi ya rais, kazi, na utumishi wa umma Zanzibar Haroun Ali Suleiman. UTEKELEZAJI WA KANUNI HIYO Watumishi waliowengi wa umma Zanzibar, kwao kanuni hii imekuwa maarufu na kuitekeleza kwenye vifungu vichache ambavyo, pengine vinamsaidia mwajiri na sio mwajiriwa. Kwa mfano, wengi wa watumushi wa umma, wanaelewa kuwa kanuni hiyo inavifungu vya kuhimiza kufika kazini saa 1:30 na kuondoka saa 9:30 kama s

MWENYE MIAKA 42 ANAKESI YA KUJIBU TUHMA ZA UBAKAJI MTOTO WA MIAKA 4

    NA HAJI NASSOR, PEMBA: MAHAKAMA maalum ya makosa ya udhalilishaji mkoa wa kusini Pemba, imemkumkuta na hatia ya ubakaji, wa mtoto wa miaka 4, mtuhumiwa Edson Saymon Shija ‘ mtuhumishi’ miaka (42) wa Machomane Chake chake.   Mahakama hiyo chini ya Hakimu wake Muumini Ali Juma, ilisema, hayo yanajiri baada ya wiki mbili zilizopita, upande wa mashataka, kukamilisha na kufunga ushahidi wao.   Alisema, mashahidi wote watano walioletwa mbele ya mahakama hiyo, na kisha kuongozwa na Wakili wa serikali, ilitosha kuonesha kuwa, mtuhumiwa huyo anahusika moja kwa moja.   Alisema, kwa ushahidi wa awali na kwa kiasi ikubwa umeishawishi mahakama hiyo, kuamini kuwa mtuhumiwa huyo, alimbaka mtoto wa miaka minne.   ‘’Mshitakiwa, unanifahamu kuwa, kwa ushahidi wa awali uliotolewa mahakamani hapa, na upande wa mashataka, umekukuta na hatia, sasa unatakiwa ujipange ili uutie doa ushahidi huu,’’alisema.   Hakimu huyo, alimfahamisha mtuhumiwa huyo, njia tatu ambazo anaweza kuzitumi

ZECO PEMBA LATOA UFAFANUZI MITA KUPACHIKWA JUU

    NA HAJI NASSOR, PEMBA SHIRIKA la Umeme la Zanzibar ZECO, limesema mita za kisasa zinazoendelea kuwekwa juu ya posi za nyumba ya mteja, hazina athari yoyote, kutokana na jinsi zilivyotengenezwa.   ZECO limesema, mita hizo zina waya maaluma wa arthing ambao unaweza kukijikinga yenyewe na mishutuko yenye mfano wa moto kama radi, jua na hata kuzuia kuingia maji ya mvua.   Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu, Afisa Mawasiliano na Huduma kwa wateja wa ZECO Pemba Haji Khatib Haji, alisema wananchi wasiwe na wasiwasi juu ya mita hizo kupachikwa juu.   Alisema, mita hizo kukana na mjengeko wake, zinakinga maalum ambayo hairuhusu maji kupenya wala kusambuliwa na wadudu ambao wanaweza kupelekea athari ya mita hiyo.   Alieleza kuwa, mita hizo ni kisasa na tayari wenzao wa Shirika la Umeme la Tanzania ‘TENESCO’ wameshaanza zoezi hilo kwa muda mrefu na hakuna athari hadi sasa.   ‘’Lazima wateja wetu na wananchi waelewe kuwa, mita hizo hazina athari, maa

ZLSC YAIKUMBUSHA JAMBO JAMII SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI

    NA HAJI NASSOR, PEMBA:::: MKURUGENZI wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ Harusi Miraji Mpatani, amewakumbusha wananchi kuwa, njia pekee ya kumaliza matendo ya ukatili na udhalilishaji, dhidi ya wanawake na watoto, ni wahanga kutokubalia kurubuniwa kwa fedha au ahadi ya ndoa.   Alisema, mfumo uliopo sasa kwa wadhalilishaji wakiona wazazi wa muhanga anamsimamo wa kufikisha na kuisimamia kesi ya mtoto wake, watuhumiwa huanza kutoa ahadi za ndoa na fedha, ili kuzilainisha kesi hizo.   Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu leo Novemba 18, 2022  kuelekea siku 16 za kupunga ukatili n audhalilishaji, Mkurugenzi huyo alisema, tayari zipo kesi kadhaa ambazo zimeshafikisha mahakamani, na hukosa hatia kutokana na wazazi kukubali kurubuniwa.   Alileza kuwa, wakati huu wa kuelekea siku 16 za kupinga ukatili na udhalilishaji wa wanawake na watoto, ni vyema jamii, ikamka na kutetea haki za watoto waliodhalilishwa.   Mkurugenzi huyo alifafanua kuwa, ik

WATOTO 14 TUNDURU WALAZWA KWA HOMA YA KUHARISHA, MADIWANI WAIPA NENO WIZARA YA AFYA

  Joyce Joliga,Songea   Tunduru. BARAZA la Madiwani Haashauri ya wilaya ya Tuneueu limeiomba Wizara ya afya kutoa elimu kufuatia  kuzuka kwa homa ya kuharisha na kutapika kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano ambapo tayari watoto 41 wamelazwa na mmoja amefariki dunia .  Ombi hilo limetolewa jana na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Tunduru Hailu Mussa,kufatia Diwani wa kata ya Nakayaya  Daud Hamlima Mpendwa  wakati akichangia hoja ya kamati ya huduma za jamii, Afya ,maji na elimu kwenye kikao cha baraza la kawaida kilichotokea kwenye ukumbi wa Klasta ya walimu wa tarafa ya mlingoti mjini hapa.   Akifafanua taarifa hiyo Mpendwa alisema kuwa amelazimika kutoa taarifa hiyo ili kuwakumbusha wataalam kutimiza wajibu wao kwa kufanya uchunguzi na kutoa majibu haraka kabla ya ungonjwa huo ulio ingia wa kuharisha  kuathiri afya za wananchi.  Aidha, Diwani huyo amewaomba wataalamu kufanyia kazi na kudhibiti hali hiyo na kulitafutia majibu tukio hilo kabla ugonjwa huo haujaleta madhara makubwa k

MWENYE MIAKA 18 ADAIWA KUMBAKA MWENYE MIAKA 17 CHAKE CHAKE PEMBA

    NA HAJI NASSOR, PEMBA MAHAKAMA maalum ya makosa ya udhalilishaji mkoa wa kusini Pemba, imemsweka rumande kijana Nassor Ali Ramadhan miaka 18 wa Msingini wilaya ya Chake chake, kwa tuhma za ubakaji.   Akiwa juu ya kizimba cha mahakama hiyo, chini ya hakimu Muumini Ali Juma, Mwendesha mashtaka wa serikali kutoka Afisi ya Mkurugenzi wa mashtaka Ali Amour Makame, alidai kuwa, tukio hilo lilitokea Oktoba 10, mwaka huu.   Alidai kuwa, kijana huyo bila ya halali na bila ya ridhaa ya wazazi wa wa mtoto wa kike, alimbaka mtoto wa miaka 17, akijua kuwa kufanya hivyo ni kosa.   Alidai kuwa, siku hiyo mtuhumiwa alimuingilia mtoto, jambo ambalo ni kosa kisheria, kinyume na kifungu cha 108 (1), (2), (e) na kifungu cha 109 (1) cha sheria ya Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018, sheria ya Zanzibar.   Mara baada ya kusomea maelezo hayo, hakimu wa mahakama hiyo, alimuuliza mtuhumiwa, ikiwa amefahamu vyema maelezo yaliotolewa mahakamani hapo.   ‘’Mtuhumiwa, je umefahamu vyema maelezo

UFAULU WAONGEZEKA, UTORO WATOWEKA SHULE KUPATA CHAKULA: MWALIMU MKUU

  Joyce Joliga ,Songea MWALIMU Mkuu shule ya Msingi Halale Gaudence Luambano amesema utoaji wa chakula shuleni umesaidia kupunguza tatizo la utoro wa wanafunzi na hivyo kuweza kuongeza ufahulu. Hayo ameyasema jana wakati wa mahojiano maalum na mtandao huu ambapo alifafanua zaidi kuwa  shuke hiyo inawanafunzi  722 ambao wote wanapata chakula shuleni hapo kutokana na michango ya wazazi wao. Alisema,wazazi wameajili  mpishi  ambaye wanamlipa kila mwezi kwa ajili ya kuandaa chakula cha wanafunzi hao pindi wakiwa wanaendelea na masomo yao " Utoaji lishe mashuleni umechochea sana kupunguza Utoro kwa wanafunzi ,kwani wanahuakika wa kupata chakula hapa hapa shuleni ,hivyo kujikita wakifanya vema kwenye masomo yao:" Aliongeza kuwa anawashukuru wazazi wenye watoto shuleni hapo kwani wanekuwa mstari wa mbele kuhakikisha wanachangia chakula pamoja na maendeleo ya shule kwa vitendo ili watoto wao waweze kusoma kwenye mazingira mazuri na kupata elimu Aidha,ameishukuru Halmashauri ya wilaya

JUWALAZA YAIWATA WANANCHI KUJIFUNZA LUGHA YA ALAMA

    NA HAJI NASSOR, PEMBA:: JAMUIYA ya wakalimani wa lugha ya alama Zanzibar ’JUWALAZA’ imeitaka jamii kujiunga na jumuiya hiyo, ili kujifunza lugha ya alama, ili kukidhi haki ya mawasiliano kwa watu wenye ulemavu wa uziwi.   Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia simu, leo Novemba 18, 2022 Katibu Mkuu wa jumuiya hiyo Kheir Mohamed Simai alisema, bado jamii haijaona umuhimu, wa kujifunza lugha ya alama, na kuwasaidia viziwi katika mawalisiliano.   Alieleza kuwa, kundi la viziwi katika jamii ni sawa na kundi jengine lolote, ambalo linahaki ya kuwasiliana baina yao na kundi jengine, ingawa wao ni kwa kutumia lugha ya alama.   ‘’Mawasiliano ya wenzetu hawa ni maalum, hivyo kila mmoja ana haki ya kuhakikisha anawasiliana nao, ili kutumiza utu na ubinadamu, lakini jambo la kwanza ni kujifunza lugha ya alama,’’alieleza.   Aidha Katibu mkuu huyo, alisema Jumuiya tokea mwaka 2019, imekuwa na utaratibu wa kufanya maadhimisho ya siku ya wakalimani, ingawa kwa mwaka hu

MWENYEKITI KAMATI SIKU 16 KUPINGA UKATILI PEMBA AWAONESHA NJIA WAJUMBE KUFANIKISHA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:::: WAJUMBE wa kamati maalum ya kuelekea siku 16 za kupinga ukatili wa wanawake na watoto, kisiwani Pemba, wametakiwa kutoa michango yao ya hali na mali, ili kufanikisha shughuli hiyo.   Kauli hiyo imetolewa leo Novemba 17, 2022 na Mwenyekiti wa kamati hiyo Nassor Bilali Ali, wakati akizungumza kwenye kikao kazi cha kamati hiyo, kilichofanyika Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ chenye lengo la kupanga mikakati ya kufanikisha shughuli husika.   Alisema, kwa wakati na siku zilizobakia, ni lazima kwa kila taasisi ambayo inaunda kamati hiyo, kutoa fedha au kitu kinachotakiwa kufanikisha shughuli hiyo, ikiwa ni pamoja na maji, chakula na usafiri.   Alisema, kama jambo hilo walilianzisha kwa furaha na bashasha, sasa wakati wa kulimaliza umefika, kwa wajumbe wa kamati hiyo, kuanza wao kutoa michango yao, kabla ya kuzifuatilia tasisi zilizoombwa.   ‘’Kwanza wajumbe waache dharura ambazo sio za msingi, pili ni wakati na wao kuwasilisha michango