Skip to main content

Posts

Showing posts from November 6, 2022

NAIBU WAZIRI ATAKA HUDUMA HARAKA YA MAJI KIZIMBANI BUBUBU IFIKE

  Na Salma Lusangi NAIBU waziri Wizara Maji, Nishati na Madini (WMNM) Zanzibar Shabaani Ali Othman ameagiza uongozi wa wizara hiyo kufikisha huduma ya maji safi na salama haraka katika Shehia ya Kizimbani Jimbo la Bububu, Wilaya Maghari ‘B’ ili kuwaondolea tatizo liliyopo. Akizungumza na wakaazi wa eneo hilo, alisema haiwezekani wananchi wakose maji kwa muda wa miezi minne hivyo aliitaka Uongozi wa Wizara yake kuhakikisha wakaazi wa shehia hiyo wanafungiwa mashine ya kusukumia maji katika kisima cha rasilihema ili wapate huduma hiyo. Alisema ikiwa changamoto kubwa ya maji katika eneo hilo inatokana na mashine ya kusukumia maji kuungua hivyo Wizara yake inajukumu la kufunga mashine nyengine ili   wananchi wapate huduma hiyo.   Alifahamisha kwamba Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) kupitia wizara hiyo inatekeleza miradi mikubwa ya maji ili kuowandolea wananchi tatizo la maji safi na salama   ikiwa ni ahadi ya Mhe. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Husse

JUMUIYA ZA WATU WENYE ULEMAVU PEMBA ZATOA NENO UAMUZI WA RAIS

    NA  HAJI NASSOR, PEMBA:: JUMUIYA za watu wenye ulamavu kisiwani Pemba, wamepongeza hatua ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, kuvikodisha, visiwa vinane vidogo vidogo, kwa dola za Marekani milioni 271.5 wastani wa shilingi bilioni 600.357 .   Wakizungumza na mwandishi wa habari kwa nyakati tofauti juu ya hatua ya serikali kuvikodisha visiwa hivyo, walisema bila shaka nia ya serikali ni kuongeza mapato ya nchi.   Mjumbe wa kamati tendaji wa Jumuiya ya wanawake wenye ulemavu Zanzibar JUWAUZA Hidaya Mjaka Ali, alisema wazo hilo ni zuri, kwani linaelekea kwenye maslahi bora ya taifa.   Alisema, bila shaka katika hatua hiyo, kila mmoja kwa nafasi yake na alipo yatamfikia matunda ya ukodishwaji huo, ambapo ni hatua moja yapo ya kufikia maendeleo ya kweli.   ‘’Mimi kwa niaba ya JUWAUZA, lazima hili lililoamuliwa na kiongozi wa nchi nilipo ngeze, maana bila shaka linamanufaa kwetu wananchi na taifa kwa ujumla,’’alisema.   Hata hivyo, ameziomba mamlaka husika wasiwaac

NORWAY YATOA USHAURI WA BURE ZANZIBAR KULINDA HAKI ZA WATU WENYE ULEMAVU

  NA HAJI NASSOR, PEMBA JAMII imeshauriwa kubuni kila mbinu na mikakati endelevu, ili kuhakikisha kundi la watu wenye ulemavu linapata haki zao zote za msingi, ikiwemo matunzo.   Akizungumza na mwanadishi wa habari hizi, Wete Mkoa wa kaskazini Pemba, Mshauri kutoka Shirika la watu wenye ulemavu la Norway  (NAD) Christine Cornick alisema, bado jamii haijawapa umuhimu watu wa kundi hilo.   Alisema, watu wenye ulemavu wamekuwa wakidharauliwa, kugawanya, kutengwa na kudhalilishwa, kutokana na mazingira yao, jambo haliingii akili.   Alisema kuwa, ushirikiano wa pamoja ndio utakaoleta nguvu ya kufanya kazi na kuleta mabadiliko ya haraka katika ukondoishaji wa masuala ya watu wenye ulemavu katika nchi mbali mbali.   "Katika mtandao huu tumeshirikisha watu mbali mbali, wanakuwa na sehemu ama mahala ambapo wanakutana na kubadilishana uzoefu katika ngazi mbali mbali na kutoa maamuzi ya kujenga jamii iliyobora", alisema.   Alifahamisha kuwa, watu wenye ulemavu wame

MDHAMINI FEDHA PEMBA ATAKA WASTAAFU WAHARAKISHIWE MAFAO YAO

  NA HANIFA SALUM, PEMBA AFISA Mdhamini ofisi ya Rais Fedha na Mipango Pemba, Abdul-wahab Said Abubakar amezitaka taasisi za umma, kuhakikisha  zinatayarisha nyaraka zote za watumishi wao, wanaotarajiwa kustaafu, ili waweze kupata haki zao kwa haraka kupitia mfuko wa hifadhi ya jamii Zanzibar 'ZSSF'.  Aliyasema hayo alipokuwa akifungua,  mkutano maalumu kwa wastaafu watarajiwa, uliofanyika katika ukumbi wa ZSSF Tibirinzi Chake chake Kisiwani Pemba.  Alisema kuwa, wastaafu wanahitaji matayarisho maalumu kwa mujibu  wa utaratibu uliowekwa kisheria ambao utasaidia kupata stahiki zao kwa wakati sahihi mara tu watakapostaafu.  "Sote tunafahamu kwamba watumishi wa umma wameitumikia serikali, na kuchangia kurithisha elimu kwa watumishi wengine sasa ni vizuri stahiki zao ziandaliwe mapema ili kuwasaidia kufikia malengo waliojiwekea baada ya kustaafu", alisema.  Aidha, Mdhamini huyo aliwataka wastaafu hao watarajiwa kuendelea kuwahimiza watumishi wengine katika maeneo wanayofa

MLAWITI APACHIKWA MIAKA 19 CHUO CHA MAFUNZO PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MSHTAKIWA Khamis Abdalla Khamis ‘kirere’ wa Kangani wilaya ya Mkoani, aliyetiwa hatiani kwa kosa la utawiti, kabla ya kusomewa hukumu ya miaka 19 ya chuo cha mafunzo, ameiomba mahakama ya mkoa Chake chake, kwanza imchunguze akili zake. Hayo aliyadai wakati alipopewa nafasi ya kujitetea kabla ya mahakama hiyo ya maalum ya makosa ya udhalilishaji ya mkoa wa kusini Pemba, chini ya Hakimu Muumini Ali Juma, kumsomea hukumu yake. Mshitakiwa huyo alidai kuwa, anaomba kuchunguuzwa afya yake ya akili, sambamba na kuomba kupunguziwa adhabu, kutokana na umri wake kuwa mdogo. Aidha alidai kutokana na kuhitajika kwake kwenye nguvu kazi ya taifa, aliomba ahuweni mahakamani hapo, kufungwa kifungo cha nje, na adhabu yake iwe ni kufanya usafi. ‘’Mheshimiwa Hakimu naiomba mahakama yako tukufu, kwanza inichunguuze akili, lakini pia inipunguzie adhabu na kunipa kifungo cha nje, maana umri wangu bado mdogo,’’alidai mshitakiwa huyo. Hata hivyo Hakimu wa mahakama hiyo Muu

UCHUMI WA WANAWAKE KASKAZINI PEMBA WAPIGWA MBELEKO NA BARABARA ZA MCC

    NA HAJI NASSOR, PEMBA: MYORORO wa thamani katika kuinua kipato cha wajasiriamali, chachu kubwa ni uwepo miundombinu ya uhakika wa barabara. Ambayo huwaunganisha wajasiriamali hao na wateja wao, iwe walioko kwenye masoko makuu au wale mmoja mmoja katika vitongoji na vijiji, au mitaa. Aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa rais Zanzibar (marehemu) Maalim Seif Sharif Hamad, aliwahi kusema kuwa, mnyororo wa thamani huanzia kwenye kilimo, uvunaji, soko la uhakika, ubora wa bidhaa na miundombinu ya uhakika ya barabara. Kilomita 35 za barabara zilijengwa kwa kiwango cha lami kwa ufadhili wa watu wa Marakeni kupitia mradi ‘MCC’ zikijumuisha ile ya Kipangani-Kangagani, Chwale-Kojani, Mzambarau takao-Pandani Finya na ile ya Bahanasa- Mtambwe. BAADA YA UJENZI WA BARABARA HIZO Kuanzia mwaka 2014, wanawake walichangamkia kuanzisha vikundi vya ushirika, ili kutanua pato lao, kupitia kazi wanazozifanya. Wakati aliyekwuwa rais wa Zanzibar wa awamu ya sita Dk. Ali Mohamed Shein, akizifungua

BILIONI 2.9/= ZAKUSANYWA KUTOKA MALIASILI ZISIZOREJESHA ZANZIBAR

  Na Salma Lusangi, ZANZIBAR Wizara ya Maji, Nishati na Madini (WMNM) Zanzibar, imekusanya jumla ya shilingi bilioni 2.97   katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita ikiwa ni mauzo ya mchanga na vibali kutokana na utaratibu   mzuri wa usimamizi pamoja kuimarika kwa mfumo wa kielektroniki wa maombi ya vibali vya Maliasili   Zisizorejesheka (Madini Management System). Taarifa hiyo imetolewa na Naibu Waziri, WMNM   Shabaan Ali Othman katika kikao cha utekelezaji wa programu za Wizara kwa kipindi cha Julai –Septemba, 2022 katika kikao cha pamoja na kamati ya Mawasiliano, Ardhi na Nishati ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar kilichofanyika jana katika ukumbi wa ZURA Maisara, Unguja. Alisema usimamizi mzuri pamoja na kuimarika kwa mfumo wa kieletroniki wa maombi ya vibali vya Maliasili   Zisizorejesheka umesaidia udhibiti wa mchanga ambapo Sekta ya Madini imekusanya shilingi 2.97 bilioni sawa na asilimia 120 ya makadirio ya   kukusanyo 2.46 bilioni. Pia alisema Idara ya Nishati na Mad