Skip to main content

Posts

Showing posts from May 25, 2025

DC. WETE AFUNGUA MAFUNZO YA WATAALAMU KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA YA MAMA SAMIA

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MKUU wa wilaya ya Wete Pemba, Abdalla Rashid Ali, amesema, uendelezaji wa kampeni ya msaada wa kisheria ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mama Samia Suluh Hassan, ni chachu ya upatikanaji haki kwa wananchi wasiokuwa na uwezo.   Mkuu huyo wa wilaya ya aliyasema leo Mei 31, 2025 ukumbi wa Jamhuri Wete, alipokuwa akifungua mafunzo ya wataalamu wa masuala ya sheria, kabla ya kwenda kutoa msaada wa kisheria wananchi wa wilaya ya Micheweni na Wete kwa siku tisa.   Alisema, wazo la Mama Samia, ni jema ambalo pamoja na kuwasaidia wananchi kutambua haki zao za msingi, ni msingi wa kulinda na kuendelea amani iliyopo.   Alieleza kuwa, iwapo wananchi watafundishwa namna ya kujua haki zao, itasaidia mno kuheshimiana katika mambo mbali mbali, samba mba na kukuza na kuendeleza msingi wa amani na utulivu.   ‘’Kwanza niwapongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na yule wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi kwa, kuanzisha jambo hili...

CHINA: WAANDISHI WA HABARI AFRIKA SAIDIENI KUKUZA UCHUMI

  ZUHURA JUMA NA HAJI NASSOR, BEIJING@@@@ WAANDISHI wa habari wa nchi za Afrika, wametakiwa kuendelea kujifunza lugha mbali mbali, ili kusaidia kukuza uchumi katika mataifa yao. Akifungua mafunzo ya siku 20 katika Ukumbi wa Hoteli ya RoyalLink ZiYu, Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Mawasiliano (CICG) Han Likiang alisema kuwa, kujua lugha mbali mbali ni muhimu katika kukuza uchumi wa nchi, hivyo kuna haja kwa wanahabari kujifuza zaidi. Alisema kuwa, ili uchumi ukue unahitaji mambo mbali mbali ikiwemo waandishi wa habari kujifunza lugha ambazo zitawasaidia kuandaa makala, vipindi na habari zenye tija hususan zinazogusa viashiria vya ukuaji wa uchumi wa ndani. ‘’Watakapotumia lugha mbali bali itawasaidia kuwahabarisha watu wengi duniani ambao wanaweza kuvutia hata wawekezaji na wageni, ambayo ni miongoni mwa kukuza uchumi wa ndani,’’ alisema. Akizungumzia umuhimu wa CICG kuandaa mafunzo hayo ni kuendeleza uhusiano wa kimataifa wa china na mataifa mengine ya Afrika kwa lengo...

HAYA HAPA YALIOJIFICHA NDANI YA 'GREAT WALL' YA CHINA

  NA HAJI NASSOR, BEIJING@@@@ NI wastani wa saa 1:45 kwa mwendo wa gari isiyo kuwa ya umma, kutoka katikati ya jiji la Beijing, hadi iliko milima hiyo. Milima hiyo, kwa hakika ni sawa na ile inayooko baadhi ya mikoa ya Tanzania bara, mfano mzuri ni Mwanza. Maana imejengwa kwa mawe (majabali makubwa), ikiwa imezungurikia nje kidogo ya Beijing, na hata ardhi yake ikiwa ni mfumo wa mawe. Wataalamu wa kichina, waliona milima hiyo isibakie bure, maana kwa zaidi ya miaka 100, sasa tokea kuasisiwa imekuwa ni sehemu ya kutunisha mfuko wao wa pato la ndani. Ni eneo lenye utulivu kiasi, likiwa limezungurukwa na milima ya asili, na kwa hakika ingekuwa vigumu kupitisha barabara, pingine kupata upande wa pili. NAMNA MILIMA HIYO ILIVYOGEUZWA ENEO LA KITALII Zipo zaidi ya mita 5,500 (sawa na umbali wa viwanjwa 55 vya mpira wa miguu), ambavyo zilianza kujengwa vidaraja kuanzia chini. Tunaelezwa kuwa, ujenzi huo ulijengwa kwa matofali maalum ya mawe, kwa mtindo wa kama vidaraja na kushukia ama kupa...

UDHALILISHAJI VYUO VIKUU NI CHANGAMOTO NYINGINE KWA WANAFUNZI, MADAWATI YA JINSIA YAWEZA KUWA MURUBAINI

  IMEANDIKWA N A MOZA SHAABAN,  PEMBA@@@@   V YUO  vikuu na taasisi za elimu ya juu , ni sehemu  zinazotegemewa  katika uzalishaji wa wataalamu  na watumishi mbali mbali nchini . Wataalamu hao ndio nyenzo ya maendeleo katika kila nchi duniani  kote na hili hakuna anayelipinga. Katika miaka ya hivi karibuni, vyuo vikuu na taasisi za elimu ya juu   vimekua vi kik abiliwa na tuhuma za uwepo wa kesi za ukatili wa kijinsia , ikiwemo rushwa ya  ngono,   udhalilishaji, pamoja na ukandamizaji wa kijinsia hususani kwa watoto wa kike .   Ri poti  ya Taasisi ya Kuzuia na K upambana na Rushwa  Tanzania (TAKUKURU) , imeeleza kwamba imeshughulikia    malalamiko ya rushwa ya ngono . Na ndio maana ma jalada ‘file’ 23 yamefunguliwa katika mikoa tofauti Tanzania , jambo linalodhihirisha uwepo wa jambo hilo ovu. Ikafahamika kuwa,  kesi 10 zilifunguliwa mahakamani ambapo kesi tano ‘ 5 ’  zilishinda na kati ya hizo , ...