Skip to main content

Posts

Showing posts with the label NGOs

MDHAMINI FEDHA PEMBA: ‘NGOs NJOONI MCHUKUE TAKWIMU SAHIHI KWETU KABLA ANDIKO LA MRADI’

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ A FISA Mdhamini wizara ya Fedha na Mipango Pemba Abdul-wahab Said Abubakar, amezitaka asasi za kiraia Pemba, kuitumia ofisi yake, wakati wanapotaka kuandika miradi, ili kupata takwimu sahihi. Alisema, ili waweze kupata andiko lenye mashiko la mradi, hawanabudi kuwa karibu mno na ofisi hiyo, ili kupata takwimu sahihi, zinazotambuliwa na mamlaka husika. Afisa Mdhamini huyo aliyasema hayo, leo Novemba 24, 2024  ukumbi wa Kiwanda cha Makonyo Wawi Chake chake, alipokuwa akifungua mjadala kwa asasi za kiraia, juu ya changamoto za sekta zilizopo kisiwani Pemba zilizolalamikiwa kurudisha nyuma harakati za maendeleo kwa asasi  na wananchi . Alisema, asasi za kiraia zimekuwa ndio mdomo wa changamoto zilizopo ndani ya jamii, hivyo wakiitumia ofisi yake, wanaweza kupata takwimu zinazoweza, kupata mashiko ya hoja zao. Alifahamisha kuwa, haiwezekani kwa asasi za kiraia, kukaa mbali na wizara ya Fedha, kwani imekuwa ndio eneo pekee lenye kukusanya kodi na tak...

MRADI 'URAIA WETU' PEMBA, WAIBUA RUNDO LA CHANGAMOTO ZA KISHERIA, SERA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MWEMVULI wa asasi za kiraia Pemba ‘PACSO’ umekutana na wadau wake, ili kuibua changamoto za kisheria na kisera, zinazotajwa kurejesha nyuma, utendaji wa kazi zao na jamii kwa ujumla. Akizungumza kwenye mkutano huo uliofanyika leo Novemba 3, 2024 ukumbi wa Maktaba Chake chake, Katibu Mkuu wa ‘PACSO’ Sifuni Ali Haji, alisema lengo la mkutano huo, ni kuibua changamoto hizo na kuzifanyia kazi. Alisema, ‘PACSO’ kwa sasa inaendelea na utekelezaji wa mradi wa urai wetu, ambapo moja ya eneo la utekelezaji wake, ni kuibua changamoto za kisheria na sera, zinazokwaza makundi ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu. Alieleza kuwa, changamoto hizo kisha, huziwasilisha kwa jumuia pacha wanaotekeleza mradi huo pamoja, ambayo ni Jumuiya ya wanawake wenye ulemavu Zanzibar ‘JUWAUZA’. Katibu Mkuu huyo alifahamisha kuwa, mfano wa jambo kama hilo, tayari zipo changamoto ambazo awali ya mwaka huu, ziliibuliwa na ‘PACSO’ na kuzifikisha kwa ‘JUWAUZA’ kwa hatua ya ...