Skip to main content

Posts

Showing posts from February 12, 2023

INTERNEWS, TAMWA- ZANZIBAR ZAUNGANA KUSAKA SHERIA MPYA YA HABARI ZANZIBAR

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:: KUMBE masuala ya haki za binadamu, yalianza kuingizwa katika mikataba mbalimbali ya kitaifa mwaka 1950. Na kwenye Azimio la kulinda Haki za Binadamu Ulimwenguni lilifikiwa mwaka 1984 na Afrika mwaka 1981. Baada ya hapo, mikataba ya kikanda ilipitishwa, kwa dhamira ya kutoa ulinzi wa haki za kiraia na kisiasa, haki za kiuchumi, kijamii na kiutamaduni, kwa ufanisi zaidi. Maazimio mbali mbali, yaligusia juu ya suala la uhuru wa maoni na kujieleza, likiwemo azimio la ‘UDHR, katiba ya Zanzibar ya   mwaka kifungu cha 18 (1) na (2) kama nayo imeeleza: “Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta kupokea na kutoa habari na dhana kupitia chombo chochote, bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati” Hata kifungu cha (2) ‘’kila raia anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbali mbali nchini na duniani kote ambayo ni muhimu kwa maisha

UNESCO, TAMWA-ZANZIBAR ZASAINI MKATABA KUPAMBANA NA UDHALILISHAJI

  Muhammed Khamis,TAMWA-ZNZ   SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA-Zanazibar) zimesaini mkataba wa mradi  kuwajengea uwezo waandishi wa habari kuandika habari za kukabiliana na ukatili dhidi ya wanawake na watoto. Mradi huo wa miezi mitatu wenye thamani ya dola za Marekani 17,000, umesainiwa kati ya Mkurugenzi wa TAMWA Zanzibar, Dk. Mzuri Issa Ali na Mwakilishi Mkazi wa UNESCO Tanzania, Michael Toto, katika hafla iliyofanyika Tunguu Wilaya ya kati Unguja. Akizungumza katika hafla hiyo, Dk. Mzuri alisema mradi huo  utaongeza nguvu mapambano dhidi ya ukatili na udhalilishaji wa wanawake na watoto ambayo ni moja ya mikakati inayotekelezwa na Serikali ya awamu ya nane chini ya uongozi wa Rais, Dk. Hussein Ali Mwinyi. Alisema hii ni mara ya kwanza kwa TAMWA na UNESCO kushirikiana, hata hivyo aliahidi kutekeleza mradi huo kwa kiwango ili kukidhi matarajio ya UNESCO. Pamoja na hayo alieleza kuwa wanamatum

SHERIA YA MAGAZETI ZANZIBAR MNYORORO MKONGWE KWA UHURU WA HABARI

      NA HAJI NASSOR, PEMBA::: Sheria nambari 5 ya Wakala wa Habari, Magazeti na Vitabu ya mwaka 1988, ambayo imefanyiwa marekebisho mwaka 1997, bado baadhi ya vifungu vyake vinaminya uhuru wa habari nchini.   Kifungu cha 27 (1) ni miongoni mwa vifungu kinachompa Mamlaka Ofisa yeyote wa Polisi, kukamata gazeti lolote, popote litakapoonekana limechapwa au kuchapishwa au ambalo kwa maoni yake tu, atalituhumu kwamba limechapwa au kuchapishwa kinyume na sheria.   Ambapo kifungu cha 27 (3) pia kinampa Mamlaka hakimu kumuamuru Ofisa yeyote wa cheo cha mkaguzi au zaidi, ikiwa ana sababu ya maana ya kuamini kwamba, atachelewa kupata hati ya upekuzi anaweza kutekeleza uwezo alio nao kwa mujibu wa sheria.   Vifungu hivi kwa nyakati za sasa, havipaswi kuwepo katika sheria hiyo kutokana na kuwa sio rafiki kwa uhuru wa vyombo vya habari nchini.   Wadau mbali mbali, wamekaa pamoja kuvifanyia uchechemuzi baadhi ya vifungu vinavyokandamiza uhuru wa vyombo vya habari, tangu mwak

RC MATTAR: ATAJA SABABU WANANCHI KUITILIA MASHAKA MAHKAMA

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA:   MKUU wa Mkoa wa Kusini Pemba Matar Zahor Masoud amesema, wananchi wanashindwa kujua wajibu wao na badala yake wanailalamikia mahakama kwamba haitendi haki.   Alisema kuwa, ipo haja ya wananchi kushirikiana na mahakama katika kutoa ushahidi na kuacha tabia ya kulalamika kwamba mahakama hazitendi haki.   Akizungumza wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya sheria yaliyofanyika katika Uwanja wa Tenis Chake Chake, alisema kuwa bila ya ushahidi hakimu hawezi kumtia hatiani mshitakiwa, hivyo juhudi zinahitajika katika kutoa ushahidi ili keshi zipate hatia.   "Kwanza tuzisimaie kesi zetu vizuri, tuzifiatilie na tutoe ushahidi, hii itasaidia kesi kupata hukumu, lakini ikiwa tunakaa tu hatufiki mahakamani baadae analalamika sio sahihi", alisema.   Aidha alisema, mfumo wa huduma ya haki mtandao watakaotumia mahakama utarahisisha usikilizaji wa mashauri, jambo ambalo litasaidia upatikanaji wa haki kwa haraka.   Kwa upande wake Jaji k

VIFUNGU VYA SHERIA YA TUME YA UTANGAAZAJI ZANZIBAR, VYATAJWA KUWA MWIBA MKALI KWA UHURU WA HABARI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA::: SASA ni miaka 26 tokea kuasisiwa kwa sheria ya Tume ya Utangaazaji Zanzibar nambari 7 ya mwaka 1997, licha ya kujumuisha na marekebisho yake. Sheria hii, imekuja kusimamia, kuangalia mwenendo wa vyombo vya habari Zanzibar hasa redio, televisheni na vile vya kisasa vyenye kurusha maudhui yao mtandaoni. Sheria hii yenye vifungu 30, vilivyobebwa na sehemu sita kuu, inavyovifungu kwa hakika sio rafiki, kuelekea uhuru kamili wa habari hapa Zanzibar. SHERIA KWA UJUMLA Kama ilivyo sheria nyingine zote, kwenye sehemu ya kwanza imeundwa na vifungu vitatu, maana kile cha nne, kimefutwa na kati ya hivyo kimoja kinatoa jina la sheria na maana ya maneno. Kwa mfano, mtangaazaji ni mtu ambaye amepewa leseni chini ya sheria hii ya kutoa huduma za utangaazaji katika vyombo vya habari. Kwenye sehemu ya pili ya sheria hii, yenyewe imeundwa na vifungu kuanzia cha tano (5) hadi cha 10, na kubwa zaidi lililopo ni pamoja na uanzishwaji wa Tume ya Utangaazaji Zanziba