Skip to main content

Posts

Showing posts from August 16, 2026

DONGO MSANII MWENYE NDOTO ZA KUFIKA MBALI KWENYE FANI YA UIGIZAJI

  -Asema, changamoto ya kifedha inawarudisha nyuma kwenye kazi zao NA ZUHURA JUMA, PEMBA    KHAMIS Ali Omar (32), umaarufu ‘dongo’, ni mkaazi wa Kambini Kichokochwe wilaya ya Wete Pemba.   Yeye ni msanii wa kizazi kipya mwenye ndoto za kufika mbali kwenye uigizaji wake.   Alianza fani hiyo mwaka 2017, wakati huo haikuwa moyoni mwake, wala haikuwa katika malengo yake aliyojiwekwea kwenye maisha.   Kipindi hicho alikuwa kwenye kikundi cha mchezo wa sarakasi cha 'Kambini Art Group' , hivyo kulikuwa na maonyesho yanayofanyika kila mwezi wa mwisho kabla ya kuingia kwenye funga, kijijini kwao, ambapo walikutana na vikundi mbalimbali ikiwemo vya uigizaji.   "Hapa kwetu kila mwaka mwezi wa ‘ mrisho’ , ( siku moja kabla ya ramadhan ), kulikuwa kunafanyika onesho 'show' , hivyo vikundi mbalimbali vya burudani vilialikwa na kuonyesha vipaji vyetu," anaeleza Dongo.   Wakati wapo kwenye sarakasi, mmoja wao alizaa wazo la kutaka kuigiz...