Skip to main content

Posts

Showing posts from March 26, 2023

GORA AWAAMSHA WATUNZA SIRI, MAKATIB MHUTASI WA SERIKALI PEMBA

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ NAIBU Katibu mkuu wizara ya Nchi, Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Zanzibar, Omar Haji Gora amewakumbusha watunza kumbu kumbu wa tasisi za serikali, kuwa, roho ya wizara ya ni sehemu za masjali. Naibu Katibu mkuu huyo, aliyasema hayo, kwa nyakati tofauti wakati akiyafungua mafunzo ya siku mbili, kwa makatibu muhutasi na watunza kumbu kumbu za serikali, kisiwani Pemba. Akizungumza na watunza kumbu kumbu hao, kwenye mafunzo yaliyofanyika ukumbi wa wizara ya Fedh Gombani, alisema masjali ndio eneo nyeti pekee, katika kila wizara. Alieleza kuwa, ofisi hiyo ndiyo inayotegemewa na wafanyakazi wote, kwa kuhifadhi kumbu kumbu zao mbali mbali, kama vile barua za ajira. Naibu Katibu mkuu huyo, alisema masjali sio sehemu ya kuwekwa ovyo ovyo, na inatakiwa kuangaliwa kwa macho zaidi ya mawili, kwani ni eneo la kutunzia haki za wafanyakazi. ‘’Msipokuwa makini kwenye masjali, mnaweza kumsababishia mfanyakazi, ugonjwa, maradhi na hati

WAZAZI MICHEWENI: 'WAPENI WATOTO VYAKULA VYA ASILI KUJENGA MWILI'

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ WAZEE wa shehia ya Majenzi Wilaya ya Micheweni Pemba wamesema, iwapo wazazi wa watoto wanaozaliwa miaka ya sasa wanafuata utaratibu wao waliokuwa wakuwapikia vyakula vya lishe, wangekuwa na nguvu pamoja na afya bora. Walisema kuwa, mambo mengi ya zamani yameachwa kutekezwa hali ambayo inasababisha madhara kwao, hivyo ni vyema wakafuata utaratibu waliokuwa wakitumia wao zamani kwa lengo la kujenga afya bora ya mtoto. Walisema kuwa, utamaduni wao wa malezi ya watoto wachanga waliokuwa wakiufuata uliwajenga sana watoto wao kwa kupata nguvu sambamba na kuepukana na husda pamoja vijicho. ‘’Maisha ya sasa kila kitu watu hawakitaki, utasikia mtoto mchanga ana gesi, mbona sisi zamani walikuwa watoto wetu hawaumwi ovyo na walikuwa na nguvu’’, awalisema wazee hao. Hamad Mbwana Shaame mkaazi wa shehia hiyo alisema kuwa, kutokana na utamaduni wao wa Micheweni, mtoto anapofikia siku saba tu alikuwa anapikiwa kibwabwa au papai na kurambishwa, ili kuku

PAC YATOA MAAGIZO KWA WAHASIBU RISITI ZA KIELEKTRONIKI

IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA WAHASIBU wametakiwa kuhakikisha wanafuatilia na kutunza vielelezo vya matumizi ya fedha za serikali pamoja na fedha za miamala ya kodi, ili wafanye kazi kwa ufanisi na zipatikane kwa wakati. Akizungumza wakati wa uwasilishaji wa Utekelezaji wa Hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali, Mwenyekiti wa Kamati za Kuchunguza na Kudhibiti Hesabu za Serikali (PAC), Juma Ali Khatib aliwataka wahasibu hao kuacha kufanya kazi kwa mazoea na muhali na badala yake wafuate sheria na kuilinda fani yao. Alisema kuwa, ili wafanye kazi kwa ufanisi na kuepusha ubabaishaji kuna haja ya kufuatilia na kutunza vielelezo vyote, kwani ni muhimu katika kuweka taarifa sawa za mapato ya Serikali.  ‘’Msikubali kuendeshwa, fanyeni kazi kwa kuzingatia fani yenu, ili kujijengea heshima na kuziweka kumbukumbu vizuri, ili zikihitajika katika Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali zipatikane kwa wakati’’, alisema Mwenyekiti huyo. Kwa upande wake Mjumbe wa Kamati hiyo Mihayo Jum

''KIMBILIENI ZAECA WANAWAKE MNAOGOMBEA MKIOMBWA RUSHWA YA NGONO''

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAMLAKA ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu wa Uchumi Zanzibar kisiwani Pemba, imewataka wanawake wanaogombea nafasi mbali mbali za uongozi, wasisite kuwaripoti wanaowanyemelea kwa rushwa ya ngono. Afisa kutoka ZAECA Kassim Yussuf Ali, aliyasema hayo Machi leo 29, 2023 kwenye mafunzo ya siku tatu, ya kuwajengea uwezo, wanawake wenye dhamira ya kugombea katika uchaguzi mkuu ujao. Alisema, kama wanaona suala la rushwa ya ngono kwao limekuwa changamoto kuelekea katika kila chaguzi, wahakikishe wanaandaa mazingira ya kuwaripoti wanaotaka kuwachafua. Alieleza kuwa, ZAECA imeanzishwa kisheria kwa kushughulikia changamoto kadhaa ikiwemo viongozi wanaotumia madaraka na uwezo wao vibaya. Alifafanua kuwa, ZAECA imekuwa ikishughulikia migogoro ya ina hiyo, inayowakumbuka watu wa makundi mbali mbali, hivyo na wao wasisite kuwafikisha wale wanaowakwaza, katika kutafuta haki ya uongozi. ‘’Wanawake mmekuwa woga kuwaripotia wale wanaowakwaza katika kutafuta uongozi, na

KAMPENI YA RAIS SAMIA YA 'MSAADA WA KISHERIA' YATAMBULISHW KWA WADAU PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ AFISA Mdhamini wizara ya nchi, afisi ya rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Utawala bora Pemba, Halima Khamis Ali, amesema kampeni ya kitaifa ya Rais ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mama Samia Suluhu Hassan ya msaada wa kisheria, inalenga kutoa ulinzi na upatikanaji haki, kwa wanawake, watoto na wale wa makundi maalum. Afisa Mdhamini huyo aliyasema hayo Machi 28, 2023, ukumbi wa wizara hiyo Gombani Chake chake Pemba, kwenye mkutano maalum wa kuutambulisha mkakati wa kampeni hiyo, kwa wadau wa haki jinai wakiwemo wasaidizi wa sheria kisiwani humo. Alisema, kampeni hiyo iliyopewa jina la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kutokana na maono yake ya kwa makundi hayo na mengine, ya upatikanaji wa msaada wa kisheria, kampeni hiyo inakuja kuondoa changamoto hizo. Alieleza kuwa, kampeni hiyo inagusa kila taasisi katika utekelezaji wake, ikiwemo wasaidizi wa sheria, Jeshi la Polisi, Tume ya haki za bindamu, vyombo vya sheria, Ofisi za ustawi, wizara

MHADHIRI SUZA: WANAWAKE WENYE DHAMIRA YA KUGOMBEA ANZENI MATARISHO SASA

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAWAKE wenye dhamira ya kugombea uongozi wa nafasi mbali mbali katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, wameshauriwa kuanza sasa kutengeneza mazingira, ikiwa ni pamoja na kufanyakazi kwa karibu na jamii husika. Kauli hiyo imetolewa na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ Salim Ali ofisi ya Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba, kwenye mafunzo ya siku tatu ya kuwajengea uwezo, wanawake wenye dhamira ya kugombea. Alisema, maandalizi ya kuelekea kugombea, hutakiwa kuanza mapema, ili kujua mipango, mikakati, njia za kupita, namna ya kuwafikia wapiga kura na wasaidizi wake. Alieleza kuwa, haiwezekani mwanamke anaetaka kugombea kwa nafasi yoyote, ile kujiacha na kutojishirikisha vyema ndani ya chama chake, na kugonjea miezi miwili, kabla ya uchaguzi mkuu ndio ajitokeze. ‘’Maandalizi ya kuingia kwenye uchaguzi wa kiushindani, hutakiwa kuanza mikakati ya kimnya kimnya mapema, ikiwa ni pamoja na kutambua ud