NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ MALEZI bora na makuzi ya mtoto, ni jambo muhimu kwa maendeleo yake,kimwili na kiakili. Hili linajumuisha huduma zote muhimu anazostahili kupewa mtoto, kuanzia miaka 0 hadi 8, ili kumuwezesha kukuwa na kufikia utimilifu wake. Ikiwa ni kimwili, kiakili, kijamii, kihisia na kimaadili, ilikushiriki kikamilifu katika ujenzi wa taifa na kuyamudu mazingirayake. Mara nyingi ni rahisi kupata haya yote, kutoka kwa wazazi au walezi,lakini wengi wao husahau kwamba matumizi ya lugha nzuri kwa watoto,inamchango mkubwa katika ustawi wao. Na zipo sheria zinazopinga ukatili wa aina zote dhidi ya watoto, kwamsingi kwamba malezi bora kwa mtoto, ndio msingi imara kwa makuzi yake. Mfano, Mkataba wa kimataifa wa haki za watoto duniani ( Conventionoftherightsofthechildren ) wa mwaka 1989, ambao umeanza kutumikarasmi mwaka 1990. Ibara yake ya 19 inasisitiza, kuwa‘ nchi wanachama kuhakikishawanakuwa na sheria nzuri zitakazo mlinda mtoto juu ya aina zote zau...