Skip to main content

Posts

Showing posts from July 20, 2025

JAMII IMETAKIWA KUWA KARIBU NA WATOTO WENYE ULEMAVU ILI KUWAJENGEA UELEWA

IMEANDIKWA NA REHEMA MOHAMED PEMBA@@@@ JAMII inashauriwa kuwa karibu na watoto wenye ulemavu, ili kuwapatia haki zao za msingi ikiwemo elimu.zuh Hayo yalizungumzwa na sheha wa shehia  ya Chambani wakati  alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi huko kijijini kwao. Alisema kuwa, watoto wenye ulemavu wanahitaji zaidi uangalizi wa mama na baba na sio kumuachia mzazi mmoja peke yake au kumtelekeza kwa bibi.  Alisema, katika jamii kuna baadhi ya watu mara baada ya kupata mtoto ambae ana ulemavu, huamua kumtenga na kumuachia katika uangalizi wa mzazi mmoja hususani mama ili kuweza kukaa nae na baadhi ya wakati kushindwa kuwapatia hata huduma. Alieleza kuwa, si jambo la busara kabisa kwa watoto wenye ulemavu kuwaweka nyumbani bila ya kuwapatia elimu, kwani nao wanayo haki ya kupata elimu bora, kupatiwa matibabu pamoja na mahitaji mengine kama watoto wengine. Vile vile alisema kuwa, ni vyema jamii iondoshe itikadi mbaya ya kuwa mtoto mwenye ulemavu hawezi kufanya chochot...

MWENYE ULEMAVU WA VIUNGO AOMBA KUPATIWA KITI MWENDO

IMEANDIKWA NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ Mohamed Omar Mohamed mkaazi wa Machomane Chake Chake Pemba mwenye ulemavu wa miguu, ameiomba Serikali na jamii kwa ujumla kumsaidia kupata kiti cha magurudumu (wheelchair) kitakachomuwezesha kuendeleza shughuli zake za kijamii na kiuchumi kwa wepesi zaidi. Akizungumza na ZanzibarLeo hapo nyumbani kwake Machomane, Mohamed amesema kiti ambacho amekuwa akikitumia kwa sasa kina zaidi ya miaka mitano na kimechakaa vya kutosha kiasi cha kushindwa kutembelea kwa mwendo unaoridhisha. Amesema kiti alichonacho hivi sasa kimepoteza nguvu na kimekuwa kikiharibika mara kwa mara, hali inayosabisha kubaki muda mrefu bila ya kiti hicho kutokana na ughali wa matengenezo yake. Amesema mara nying kiti hicho huharibika betri ambayo imekuwa ikiuzwa kwa bei ya Tsh. 80,000, kiwango ambacho si rahisi kwake kukimudu kutokana kipato chake kidogo. "Najiona dhaifu mno.  Kiti mwendo ndio miguu yangu nilojaaliwa na Allah. Kutokana na hali ngumu ya kimaisha, nashindwa kununua ...

'WARATIBU WA UCHAGUZI PITIENI SHERIA, KANUNI KWA UMAKINI': JAJI MSTAAFU

NA MOZA SHAABAN, PEMBA WASHIRIKI wa mafunzo ya uratibu wa Uchaguzi kisiwani Pemba wametakiwa kuzipitia na kuzifuata vyema sheria, kanuni, taratibu  na miongozo ya uchaguzi ili kutekeleza ipasavyo majukumu yao. Wito huo umetolewa leo Julai 21, 2025 na  Jaji mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mbarouk Salim Mbarouk ambae pia ni mgeni rasmi katika mafunzo hayo yaliofanyika Wawi Chake  chake Pemba. Alisema ni vyema kwa waratibu hao kutumia muda wao kuzisoma na kuzifuata katiba, sheria, kanuni na miongozo ya uchaguzi ili kutekeleza kwa ufanisi majukumu yao katika kipindi chote cha usimamizi wa uchaguzi Mkuu. Alieleza kua uchaguzi ni mchakato unaojumuisha hatua na taratibu mbali mbali za kisheria, zinazopaswa kufuatwa ili kuimarisha utendaji wa kazi hizo pamoja na kuimarisha amani nchi. "uchaguzi ni mchakato unaojumuisha hatua na taratibu mbali mbali za kisheria zinazopaswa kufuatwa ili kuimarisha utendaji wa kazi  na kujua na kuzifuata sheria hizo kutasaidia  kuimari...