CFP YAANZA KUMALIZA KIU YA UKOSEFU WA MAJI KWA WAKULIMA KILIMO MSITU PEMBA, FATMA BAKAR AANZA KUUAGA UMASKINI
NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@ ….nilianza na shamba moja la ekari moja, na sasa nimeongeza mawaili yenye ukubwa na nusu nusu eka kila moja, ndio maneno ya mkulima kilimo msitu Fatma Bakari wa Chato. Chato hiyo, sio ile ya Mkoani Dodoma Tanzania bara, hapana ipo kijiji cha Gombeume, shehia ya Mchanga mdogo wilaya ya Wete Pemba. Hapo ndio anapoishi mkulima huyo, ambae kwa sasa anajiita mtaalamu wa kilimo msitu, ama kilimo mchanganyiko wa miti ya biashara na chakula. ALIANZAJE KILIMO MSITU Alianza kuwataja Jumuiya ya Uhifadhi yaw a Misutu Pemba ‘CFP’ na Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar, kwamba ndio waliomzua yeye na sasa kuwa mkulima mtaalam wa kilimo msitu. Alijifunza nini maana ya kilimo hicho, kinalimwaje na faida zake za muda mfupi na mrefu, katika maisha ya kila siku. Baada ya mafunzo, huku na muume, akiwa ameshafariki, ndipo mwaka 2024 mwezi wa August, alipoanza kilimo hicho ndani ya shamba la urithi la aliyekuwa muume wake. Hapo akiwa na utaalamu, ...