Skip to main content

Posts

Showing posts from July 31, 2022

ZLSC: 'MNAOPATA ELIMU YA UTATUZI WA MIGOGORO MSIIKALIE'

    HABIBA ZARALI, PEMBA KITUO cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC, kimeitaka jamii kisiwani Pemba, kuendelea kutoa elimu ya sheria inayohusiana na utatuzi wa migogoro na ujenzi wa amani, wanayoipata kupitia kituo hicho, ili kuifanya jamii kuishi kwa usalama na kupata haki zao. Kauli hiyo imetolewa na Mratibu wa kituo hicho tawi la Pemba, Safia Saleh Sultan, katika mkutano wa kutoa elimu ya utatuzi wa migogoro, uliowashirikisha viongozi wa dini, kisiasa na wahamasishaji jamii kutoka shehia za Njuguni na Mihogoni Wilaya ya Micheweni. Alisema elimu inayotolewa kituoni hapo, kupitia makundi mbalimbali ya jamii kisiwani humo, ni miongoni mwa njia wanazozifanya za kuhakikisha wanawajengea wananchi uwezo wa kisheria ili waweze kutatuwa migogoro kwa njia ya amani. Alieleza kuwa, katika jamii kuna migogoro mingi ikiwemo ya kesi za madai kama vile ya ardhi, ndoa, matunzo ya watoto, madeni, hivyo ni vyema wakavitumia vikao vya familia, kuyamaliza. ‘’Kesi kama hizi mnapokimbilia mahakama

UKWELI KUHUSU UWEZO WA UBONGO WA MTOTO MCHANGA HUU HAPA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA: email: hajipembatoday@gmail.com JAMII imetakiwa kufahamu kuwa, ubongo wa mtoto mchanga unakuwa na ufahamu wa asilimia 25, katika kipindi cha miezi mitatu baada ya kuzaliwa, hivyo ni wakati mzuri kwa familia kumuandaa mtoto huyo watakavyo. Tafiti zinaeleza kuwa, kama wazazi wanataka kuwa na mtoto mwenye ufahamu wa kujua mambo kadhaa, waanze nae ndani ya miezi mitatu ya mwanzo, kwa kuzungumza nae, kumshirikisha na kumtajia majina ya vitu kama vilivyo. Mtaalamu wa malezi ya kisayansi ya awali ya watoto ‘SECD’ Rashid Said Nassor, alisema sio sahihi katika kipindi hicho, wazazi kuzungumza na mtoto wao, kwa kuigizia sauti ya kichanga. ‘’Sio vyema kwa wazazi na walezi kuyatumia maneno kama mma, nyamu, chamaki, mbobo, dizi, ledio, chimu, pecha bali kwa wakati huo, wanapowasiliana na watoto wao, wayatamke majina kama yalivyo,’’alieleza. Aidha mtaalamu huyo alisema, sayansi ikaubali kuwa, mtoto anauwezo mkubwa wa kusikia na kuhifadhi kila kitu kinachozungumza k

MCT LATOA TATHIMINI UHURU WA VYOMBO VYA HABARI NCHINI

  Taarifa kwa Vyombo vya Habari Tathmini ya Baraza la Habari Tanzania (MCT) kuhusu hali ya uhuru wa vyombo vya habari nchini   leo Agosti 04, 2022 Kanzidata ya Baraza la Habari Tanzania (MCT) imerekodi matukio 10 ya madhila ambayo waandishi wa habari wamekutana nayo katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Julai mwaka 2022. Hii ni kwa mujibu wa kanzadata hiyo ambayo inapatikana kwenye www.pressviolations.or.tz Madhila ambayo Baraza limeyarekodi kwenye kanzidata yake katika kipindi hicho ni matukio matatu ya vyombo vya habari kufungiwa, tukio moja la kunyanyaswa, matukio matatu ya kukamatwa, kunyimwa taarifa na matukio mawili ya waandishi kutishiwa. Katika matukio hayo polisi wanaongoza kwa kuwa taasisi yenye migogoro na waandishi wa habari, ikifuatiwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA). Matukio mengine ni ya waandishi wa habari kutishwa, yakitolewa na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma tukio moja, na la watu wasiojulikana pia tukio moja. Kipindi kama hiki mwaka j

WASINDIKAJI, WASAMBAAZAJI MAZIWA MBADALA NA VYAKULA VYA WATOTO ZINGATIENI SHERIA

  JOCYCE JOLIGA Sekta binafsi, wasindikaji, wasambazaji na wauzaji wa  maziwa mbadala na vyakula vya watoto wameagizwa kuepuka matangazo ya bidhaa zao ili kuzingatia sheria na kanuni ya kudhibiti uuzaji na usambazaji wa maziwa na vyakula vya watoto wachanga na wadogo. Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu Mhe. Mwanaidi Khamis wakati akiongea na wananchi wa  Halmashauri ya Ikungi, Mkoani Singida katika uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji maziwa ya mama kwa watoto duniani. "Mnapaswa kuzingatia Sheria na Kanuni ya Kudhibiti Uuzaji na Usambazaji wa Maziwa na Vyakula vya Watoto wachanga na wadogo kwa kuepuka utoaji wa matangazo, ushawishi na kufanya promosheni ya maziwa mbadala na vyakula vya watoto wachanga kwenye vyombo vya habari au katika maeneo yoyote". Aidha, alisema   Viongozi wa kijamii wakiwemo Viongozi wa Dini na Siasa, watu maarufu wenye ushawishi katika jamii, wasanii na wanamichezo wana wajibu wa kuhamasi

REVIEW OF THE STATE OF THE MEDIA IN TANZANIA 2020-2021

    By Our correspondent This brief review dwells mostly on what I consider major omissions in the report, which, if included, would have added more value to the findings.   CHAPTER ONE 1.0 LEGAL, REGULATORY AND POLICY REGIME The findings should have been specific about the key role played by the Director of Information in suppressing press freedom, particularly with regard to newspapers, during the period under review. It should be noted that it was specifically the Director of Information who used powers vested in his office to ban newspapers viewed as critical of the government. Editors were also frequently summoned to either appear in person at the Tanzania Information Services (Maelezo) offices, or ordered to explain in writing content that apparently did not go down well with the powers that be. There were also instances of editors being intimidated into not publishing content that was viewed as “hostile”, particularly when reporters sought the chief governm

SAKINA KHAMIS WA PEMBA: RUZUKU YA TASAF YAMZALISHIA RUNDO LA MIRADI

  Alianzia nazi, genge, samaki wa kukaanga, sasa auza nguo NA HAJI NASSOR, PEMBA::: email:: hajipembatoday@gmail.com ‘’MIMI sasa sijioni mwanamke, najiona kama mwanamme mwenye uwezo mkubwa, ndio maneno ya mwanzo wa mlengwa kaya maskini Sakina Khamis Mbwana miaka 37, wa kijiji cha Tumbe Mashariki Pemba. Nilipotaka kujua kwanini asijifananishe na mwanamke aliyepata mafanikio, kwanza aliagusha kicheko na kusema, ameshahama kwenye uwanawake kiuwezo, na sasa ni sawa na mwanamme. Nilipomng’ang’ania sababu za kujifananisha na mwanamme, alisema ilishazoeleka na kuaminika kuwa mwanamke hawezi kwa na mafanikio. KABLA YA KUFIKIWA NA TASAF Sakina kwa bahati mbaya, mwaka 2013 alifiliwa na mume wake, aliyemuachia watoto sita, wakati huo wakiishi kwenye nyumba ya miti na makuti. Matunzo ya watoto hao, anakumbuka kuyapata ndani mwezi mmoja, baada ya kufiliwa na muumewake, ingawa kuanzia hapo, hakuna tena mchango hata wa kupata majani ya chai kutoka kwenye familia. Hadithi ikawa kwake

ZECO LAPIGWA BAO NA WATEJA VISHOKA

  Na Salma Lusangi, ZANZIBAR::: ASILIMIA 17 ya umeme unapotoea Zanzibar kutokana na baadhi ya watu kuunga umeme kinyume na sheria, hali ambayo inapelekea nchi kukosa mapato.   Waziri wa Maji, Nishati na Madini Shaibu Kaduara alisema wanaotumia umeme kinyume na Sheria ni kosa la jinai na atakaebainika atashtakiwa kwa kosa la kuhujumu uchumi wa Nchi.   Hayo yalisemwa na Waziri huyo wakati aliposhiriki katika zoezi lililopewa jina la ''Kaduara'' ambalo limejikita katika kuwatafuta wananchi wanaojiunganishia nishati ya umeme kinyemela.   Alisema zoezi limebainika wapo wananchi wengi wanaotumiya umeme kinyume na Sheria kwa kujiunganishia majumbani, kitendo ambacho kinatia hasara kwa Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO).   Alisema Wizara yake imeanzisha operesheni hiyo ambayo lengo lake ni kuwafungia mita ya umeme wananchi pamoja na kufanya msako wa kuwatafuta watu wanaojipatia huduma ya nishati kinyume na Sheria zilizowekwa.   Aidha, alisema operesheni imewakamata baadhi ya watu

PACSO PEMBA YAWAPA UJUMBE MZITO WASIOPENDA MIGOGORO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA: email: hajipembatoday@gmail.com: JAMII kisiwani Pemba, imetakiwa kujitenga mbali na baadhi ya watu wanaotumia vibaya nafasi zao, kwa kushawishi kujiingiza kwenye migogoro isiyokuwa na tija, kwani amani itakapochafuka, gharama ya kuirejesha ni kubwa. Hayo yalielezwa na mtoa mada, ya utatuzi wa migogoro kisiwani humo, Ali Abdalla Juma, wakati akielezea njia za kujinga na migogoro, kwenye mafunzo ya siku mbili ya utatuzi wa migogoro, yalioandaliwa na Jumuiya mwemvuli ya asasi za kiraia kisiwani Pemba PACSO, na kufanyika Chake chake. Alisema, inawezekana mtu kwa sababu ya cheo chake au umaarufu wake katika jamii, akalikusanya kundi mfano kama la vijana, na kuwashawishi kuvunja amani, akijua matokeo yake ni kujipatia maslahi yake binafsi. Mtoa mada huyo alieleza kuwa, jamii lazima ione umuhimu wa kuwepo kwa amani na utulivu, na vivyo hivyo wawe mashuhuda wazuri, kwa nchi zilizotumbikia kwenye migogoro, namna ambavyo maisha yanakuwa magumu. ‘’Sisi jamii,