Skip to main content

Posts

Showing posts from December 11, 2022

WATU 300 KUTOKA DUNIANI KOTE KUSHIRIKI KONGAMANO LA KISWAHILI PEMBA

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA: ZAIDI ya watu 300 kutoka nchi mbali mbali ikiwemo Marekani, wanatarajiwa kushiriki katika Kongamano la sita la Kiswahili la kimataifa, litakalofanyika Disemba 17 na 18 katika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Wete mkoa wa Kaskazini Pemba. Akizungumza na waandishi wa habari Afisa Mdhamini Wizara ya Habari, Utamaduni, Vijana, Utamaduni na Michezo Pemba, Mfamau Lali Mafamau alisema kuwa, maandalizi ya Kongamano hilo yameshafikia asilimia 90. Alisema kuwa, ni faraja kwa kisiwa cha Pemba, kufanyika Kongamano hilo, kwani wananchi walio wengi, watanufaika kwa namna mbali mbali kutokana na wageni watakaoingia pamoja sambamba na kujifunza mambo mbali mbali ya Kiswahili na utamaduni. ‘’Kwa kweli tunaona fahari Kongamano hili kufanyika kisiwani hapa, wageni wengi wataingia na kushiriki, hivyo wananchi watanufaika kwa namna moja ama nyengine’’, alisema Mdhamini huyo. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Kiswahili Zanzibar Saade Said Mbarouk alisema kuwa, mada mb

WATU WENYE ULEMAVU WAIPA NENO WIZARA YA AFYA PEMBA

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA: WATU wenye ulemavu kisiwani Pemba wameiomba Serikali kupitia Wizara ya Afya kuweka kitengo maalumu cha kuwapatia huduma, ili kuepuka usumbufu wanaoupata wakati wanapofika kutaka huduma za matibabu. Walisema kuwa, wameona kwamba kuna vitengo mbali mbali vimewekwa ikiwemo vya Ukimwi, kitengo cha maradhi ya macho, viungo, kifua kikuu na vyengine, ingawa wao hawajatengewa, jambo ambalo linawapa usumbufu wakati wanapofika hospitali. Walieleza kuwa, ipo haja kwa Wizara husika kuwawekea kitengo chao maalumu ambacho kitakuwa kina mahitaji yote ya watu wenye ulemavu, ikiwemo kuweka miundombinu imara ya ufikiaji, wakalimani pamoja na madaktari ambao watakuwa wanajua lugha za alama. Wakizungumza katika kongamano la Watu Wenye Ulemavu ambalo liliwashirikisha wadau mbali mbali, walieleza kuwa wanapoifuata huduma ya afya wanateseka sana, hivyo watakapowekewa kitengo chao wataondokana na usumbufu ambao wanaupata. “Kitengo ni muhimu kwetu kwa sababu tutakuwa na ‘one

WAZIRI HAROUN AIPA KAZI IDARA YA KATIBA KUSIMAMIA MAAZIMIO 16 YA JUKWAA

  NA HAJI NASSOR, UNGUJA::: WAZIRI wa Nchi Afisi ya Rais Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Zanzibar Haroun Ali Suleman, ameiagiza Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria kwa kushirikiana na tasisi ya LSF, kukutana kila baada ya miezi mitatu, ili kuona maazimio 16 yaliobuliwa kwenye jukwaa la msaada wa kisheria yanafanyiwa kazi. Alisema, Zanzibar imekuwa hodari wa kuanzisha mambo na kisha kuyaweka kwenye karatasi bila ya kufanyiwakazi, lakini kwa hayo maazimioa 16, lazima wajitahidi kuhakikisha wanayatekeleza. Waziri Haroun ameyasema hayo Disemba 14, 2022 wakati akilifunga jukwaa la pili la Msaada wa Kisheria Zanzibar, lililoandaliwa na Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar kwa ufadhili wa LSF na kufanyika Chuo cha Utalii Maruhubi Unguja. Alieleza kuwa, kila baada ya miezi mitatu anahitaji kupata ripoti ya utekelezaji wa maazimio hayo, ili kuona waliolengwa wanufaika nayo. ‘’Mhakikishe Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria kwa kushirikiana na wadau wenu LSF, na m

MAKAMU WA PILI AWAPA NENO WASAIDIZI WA SHERIA ZANZIBAR AKIFUNGUA JUKWAA LA PILI

    NA HAJI NASSOR, UNGUJA MAKAMU wa Pili wa Rais Zanzibar Hemed Suleiman Abdullah, amewataka wasaidizi wa sheria na watoa msaada wa kisheria kuendelea kufanya kazi zao kwa uweledi, na hasa kuelekeza nguvu zao, katika mapambano ya udhalilishaji, rushwa na dawa za kulevya. Alisema, bado jamii inakabiliwa na changamoto hizo, hivyo ni wajibu wao kuendelea kutumia weledi wao, ili wananchi waishi kwa salama, bila ya kuwa na changamoto hizo . Makamu huyo wa Pili, ameyasema hayo leo Disemba 13, 2022 ukumbi wa Chuo cha Utalii Maruhubi mjini Unguja, kwenye jukwaa la pili la msaada wa kisheria Zanzibar, lililoandaliwa na Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria Zanzibar. Alisema, serikali inayoongozwa na Dk. Mwinyi inaelewa kazi inayofanywa na wasaidizi wa sheria, hivyo lazima wazidishe kasi na juhudi za kuhakikisha wanaifikisha elimu hiyo kwa jamii. Makamu huyo wa Pili alisema, serikali itaendelea kuwa karibu mno na Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria, ili kuona wanafanikisha malengo

MAKAMU WA PILI MGENI RASMI JUKWAA LA MSAADA KISHERIA ASUBUHI HII ZANZIBAR

  NA HAJI NASSOR, ZANZIBAR::: MAKAMU wa Pili wa rais Zanzibar Hemed Suleiman Abdallah, asubuhi ya leo Disemba 13, 2022 anatarajiwa kuwa mgeni rasmi, katika jukwaa la mwaka la pili la msaada wa kisheria Zanzibar. Shughuli hiyo inatarajiwa kufanyika ukumbi wa Chuo cha Utalii Maruhubi mjini Unguja, na tayari matayarisho ya shuguli hiyo, yameshakamilika kwa asilimia 100. Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa baadhi ya watendaji wa Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar, walisema jambo jengine ambalo limeshamilika ni kupatikana kwa ukumbi husika. Afisa sheria wa Idara hiyo Pemba Bakari Omar Ali, alisema wajumbe watarajiwa wa jukwaa hilo, wakiwemo kutoka kisiwani Pemba tayari wameshawasili kisiwani Unguja. Alisema jukwaa hilo, ambalo litadumu kwa muda wa siku mbili, pamoja na mambo mengine, litaangalia manufaa ya uwepo wa Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria kwa wananchi wa Zanzibar. Alisema, aidha wajumbe hao waalikwa wakiwemo wasaidizi wa sheria, watoa msaada wa kisheria, w