Skip to main content

Posts

Showing posts from January 29, 2023

WAZIRI RAHMA ABAINISHA CHANZO CHA MIGOGORO YA ARDHI ZANZIBAR

  Na Sabiha Keis, Zanzibar Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanzibar Rahma Kassim Ali amesema ongezeko la migogoro ya Ardhi nchini linasababishwa na baadhi ya wananchi kununua Ardhi kwa kutofuata sheria na taratibu zilizowekwa. Kauli hiyo ameitoa mara baada ya kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Bajeti kwa kipindi cha Julai hadi Disemba 2022 kwa kamati ya Mawasiliano,Ardhi na Nishati ya Baraza la Wawakilishi huko katika ukumbi wa Wizara hiyo Maisara, Unguja. “Asilimia 80 ya migogoro ya Ardhi inatokana na mauziano ya wananchi kuuziana ardhi kinyume na sheria, na hao wanasheria ndio balaa, kiwanja kimoja kinauzwa mara mbili hata tatu, afadhali hata masheha wakihusishwa wajua kama kiwanja hichi kimeshauzwa “ Alisema Waziri Rahma. Alieleza kwamba mbali na ununuzi huo wa Ardhi usifuata sheria lakini pia ujenzi holela usiozingatia mipaka halisi ya eneo husika umekua ukichangia kuwepo kwa migogoro hiyo ambapo Wizara yake imejipanga kwa sasa katika kudhibiti hali hiyo. Waziri Rahma al

DC: CHAKE CHAKE AUNGA MKONO KAMATI KUONDOA OMBA OMBA PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA::: MKUU wa wilaya ya Chake chake Abdalla Rashid Ali, ameunga mkono wazo la wanaharakati wa haki za binadamu Pemba, linaloelekea kutaka kupiga marufuku, wananchi wakiwemo watu wenye ulemavu, la kuendeleza kuwa omba omba mitaani. Mkuu huyo wa wilaya, aliyasema hayo leo Januari 31, 2023 ofisini kwake mjini Chake chake, wakati akizungumza na kamati hiyo, iliyoongozwa na Mwenyikiti wake, Tatu Abdalla Msellem, wakati ilipofika kuonana na Mkuu huyo wa wilaya, kwa ajili ya kupata mwelekeo kabla ya kufanyika kwa zoezi hilo. Alisema, wazo la kamati hiyo ni zuri, maana hata wao kama wilaya, linawaumiza kichwa, ingawa walikuwa wakifanya kwa kuwafuata mtu mmoja mmoja, na kufanikiwa kiasi. Alieleza kuwa, sasa kama imejitokeza kamati ya kupinga jambo hilo, wilaya itatoa kila aina ya ushirikiano, ili kufanikisha zoezi hilo, kwa haraka na umakini. Mkuu huyo wa wilaya, alifahamisha kuwa, utamaduni na silka ya wazanzibari sio kufanya omba omba kama kazi ya kila siku na h

ZAFELA: TAKWIMU ZA UDHALILISHAJI MUHIMU KATIKA MAPAMBANO

  MKURUGENZI wa Jumuiya ya   Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA), Jamila Mahmoud Juma, amesema mfumo wa   ukusanyaji wa taarifa za udhalilishaji (database), unasaidia kutambua kasi ya ongezeko au kupungua kwa matukio hayo.   Jamila alieleza hayo huko ofisini kwake Mpendae Mjini Zanzibar, wakati alipozungumza na mwandishi wa habari hizi, ambapo alisema mfumo huo unasaidia kuweka kumbukumbuku za matukio hayo.   Mkurugenzi alisema mfumo huo unarahisisha upatikanaji wa taarifa sahihi za matukio ya vitendo vya udhalilishaji kuanzaia hatua za ufuatiliaji wa kesi mpaka kufikia mahakamani kwa mashirikano na mashirika ya serikali na taasisi mbalimbali.   Jamila alisema tangu kuzinduliwa kwa mfumo huo mwaka 2021 na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, mfumo huo umekuwa msaada mkubwa wa kujua taarifa kwa taasisi zilizomstari wa mbele kwenye mapambano dhidi ya vitendo vya udhalilishaji.   “Mfumo huu ni muhimu na una faida kwa jamii katika

TAMWA-ZANZIBAR: WATOTO WALINDWE DHIDI YA VITENDO VYA UDHALILISHAJI

  Wadau wa haki za watoto hasa watoto wenye umri wa zaidi ya miaka 10  wanahitaji kujadili na kuweka mpango mzuri wa kuwalinda dhidi ya  vitendo vya udhalilishaji na ukatili.   Taakwimu zilizotolewa hivi karibuni na Afisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar zinaonesha kuwa   jumla ya watoto 1, 173 waliathirika  na vitendo vya udhalilishaji na ukatili mwaka 2022.   Kwa mujibu wa taarifa hiyo jumla ya matukio 883 (asilimia 75%) ambayo yaliripotiwa ni kwa watoto hao wenye umri kati ya miaka 11 hadi 17.   Kwa mukhtadha huo, TAMWA-ZNZ inaona kuna umuhimu mkubwa wa kulipa kipaumbele kundi hili na kuona ni matatizo gani yanayolikabili ili kutafuta muafaka wa tatizo.   Utafiti wa kihabari wa TAMWA ZNZ uligundua kuwa matatizo ya matumizi mabaya ya kimtandao kwa vijana wa kiume yanachochea kutaka kujihusisha na masuala ya ubakaji, wakati tamaa kwa watoto wa kike inachangia kujiingiza katika masuala hayo.    Asilimia 63 ya watu walilaumu vijana wa kiume kuangalia video na picha cha

'ASI' SECURITY: 'TUTUMIENI TUKO 'FIT' KIULINZI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA::: UONGOZI wa kampuni ya ulinzi ya Active Security with Integrity ‘ASI ’ umeziomba tasisiza serikali na zile za watu binafsi, kuwatumia katika ulinzi wa maeneo yao mbali mbali, kwani vijana wao, wanayo mafunzo ya kutosha ya kazi hiyo. Ushauri huo umetolewa na Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Salim Khamis Juma, wakati akizungumza hospitali ya Coteji Vitongoji wilaya ya Chake chake, mara baada ya kumalizika kazi ya usafi, iliyofanywa na watendaji wa kampuni hiyo. Alisema, baada ya kusajiliwa rasmi serikalini na kwenye taasisi zake nyingine, sasa ni wajibu wa tasisi mbali mbali kuwatumia wao katika ulinzi. Alieleza kuwa, tayari zipo tasisi chache wameshaanza kuwatumia, lakini kwa idadi ya vijana walionao, ni vyema na tasisi nyingine kuona umuhimu huo. Mkrugenzi huyo alieleza kuwa, ili kufikia azma ya serikali ya ajira 300,000 zilizotangaazwa na rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi, basi ni kuwapatia ajira vijana wa kampuni yao ya ‘ASI’. ‘’Kama tasisi za s