Skip to main content

Posts

Showing posts from August 4, 2024

BARABARA OLE-KENGJA BAADA YA MIAKA MINNE SASA YAWEKEWA ALAMA

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MADEREVA na wananchi wanaotumia barabara ya Ole-Kengeja, iliyofunguliwa mwaka 2020 na aliyekuwa Rais wa Zanzibar na Dk. Ali Mohamed Shein, wamefurahia baada ya zoezi la uwekaji wa alama za barabarani kuanza . Walisema awali, barabara hiyo iliyofunguliwa miaka minne sasa, haikuwa na alama za barabarani, jambo ambalo lilikuwa likiwapa ukakasi, wanapokuwa barabarani. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, walisema kwa sasa wamefurahishwa na uamuzi wa serikali wa awamu ya nane, chini ya Rais Dk. Hussein Ali Mwinyi, kuitaka wizara husika, kuiwekea alama barabara hiyo. Walisema kuwa, kukosekana kwa alama za barabarani, kulikuwa kunatishia maisha yao na watembea kwa miguu, kutokana na kukosekana la alama hizo muhimu. Mmoja kati ya madereva hao, Mohamed Khamis Hasnuu alisema, walikuwa wakipata shida hasa kwa wao wageni wa barabara hiyo, jambo ambalo lingeweza kusababisha ajali. ‘’Hujui wapi kuna skuli, soko, hospitali, mpindo na muunganiko wa baraba

WAZIRI MKUCHIKA AVUTIWA NA PBZ, KUWASAIDIA WAKULIMA LINDI, MTWARA

  Na Mwandishi wetu, Lindi@@@@ WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Raisi, Ikulu (kazi maalum) Kapten George Huruma Mkuchika amevutiwa na huduma zinazotolewa na Benki ya watu wa Zanzibar tawi la Mtwara ambapo ameipongeza benki hiyo.  Akizungumza alipotembelea banda la maonyesho ya nanenane kanda ya kusini yanayofanyika katika viwanja vya ngongo mkoani Lindi amesema kuwa ni benki yenye gharama nafuu.  Amesema kuwa unafuu huo umekuwa ukiwasaidia wakulima kupata malipo yao ya korosho na ufuta kwa wakati.  Akizungumza mbele ya  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Raisi, Ikulu (kazi maalum) Kapten George Huruma Mkuchika,  kwenye Maonyesho ya Nane Nane yanayofanyika katika viwanja vya ngongo kwenye Mkoa wa Lindi Mwakilishi wa Benki hiyo katika maonyesho hayo Nassoro  Mohamed Zaid  amesema kuwa huduma hizo zitawezesha wakulima kuhudumiwa popote walipo.  Amesema kuwa uwepo wao katika maonyesho hayo ni kuhamasisha wakulima na wafugaji kuweza kutumia benki hiyo ambayo imeweza kukua kwa kasi na kusogeza huduma bora kwa

TAMWA -ZANZIBAR INGALI MACHO HADI IPATIKANE SHERIA MPYA YA HABARI ZANZIBAR

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ SHERIA iliyodumu miaka 36 sasa inatajwa kutokuwa rafiiki na uhuru wa habari, ni ile nambari 5 ya mwaka 1988 ya Magazeti, Vitabu na Mawakala wa Habari Zanzibar. Ni miaka 36 sasa, sheria hii inaendelea kutumika Zanzibar, na kutajwa kuathiri na kutishia utendaji kazi wawaandishi wa habari na vyombo vyao hapa visiwani. Maana wadau na waandishi wa habari, wanakubali kuwa, upatikanaji, usambaaji wa habari ni haki ya kikatiba. Kwa Katiba ya Zanzibar yam waka 1984, kwenye kifungu cha 18, kimebainisha hilo sambamba na ile ya Jamhuri ya Mungano wa Tanzania yam waka 1977, kwenye Ibara kama hiyo nayo, imewekwa. HISTORIA YA UPATIKANAJI SHERIA MPYA ZANZIBAR Sheria hiyo tokea mwaka 2010, ilianziwa harakati za kutaka kufutwa, kwa wadau wa habari kujikusanya pamoja, ili sasa iwe na sheria moya ya habari. Kwa wakati huo, tasisi za Baraza la Habari Tanzania ‘MCT’ –ofisi ya Zanzibar, vyama vya waandishi wa habari, taasisi za haki za binadamu na wizara husika, zi