Skip to main content

Posts

Showing posts from May 26, 2024

RC. MJINI MAGHARIBI AKITAKA SUZA KUENDELEA KUANDAA MASHINDANO YA WAANDISHI CHIPKIZI

  NA MARYAM NASSOR, ZANZIBAR@@@@ MKUU wa mkoa wa mjini Magharibi Unguja, Idrissa Kitwana Mustafa , amekitaka chuo kikuu cha taifa   Zanzibar ( SUZA) kuendelea kuandaa   mashindano ya waandishi chipukizi, ili   kuwapima uwezo wao katika kada hiyo. Ameyasema hayo, katika hafla ya kuwatunuku vyeti na zawadi washindi wa shindano la waandishi chipukizi, katika   chuo cha SUZA kampasi ya Kilimani.   Alisema ,   fani ya uwandishi wa habari ni kada nyeti sana, hivyo ni vyema wanafunzi wakasoma na kufanya kazi kwa bidii, kwani kumeibuka wimbi kubwa la watu wanaojiita waandishi bila ya kuwa na sifa ya uaandishi au bila ya kusomea. “ Siku hizi kumeibuka wimbi la waandishi makanjanja na wao wanajiita waandishi wa habari, wakati hawajasomea hata cheti katika habari na kuichafua kada hii kwa kwenda kinyume na maadili ya uwandishi,”alisema. Aidha alisema kuwa, kwa kupitia mashindano kama hayo, watapatikana wandishi wazuri na wajuzi wa lugha, kwani ili uwe mwandishi mzuri basi , uwe na uwele

AFANDE KHALFAN. AITAHADHARISHA 'MECCO' WIZI WA VIFAA VYAO

  IMEAKWANA ZUHURA JUMA, PEMBA    MKAGUZI wa shehia ya Pandani Wilaya ya Wete, Inspekta wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba Khalfan Ali Ussi ameutaka uongozi wa kampuni ya ujenzi wa barabara ya MECCO kuchukua tahadhari juu ya vitendo vya uhalifu vinavyoweza kutokea na kuhakikisha vifaa vyao vinakuwa salama.   Alisema kuwa, licha ya kuwepo kwa hali ya usalama katika eneo hilo la ofisi yao lakini hawapaswi kuacha kuchukua tahadhari juu ya uwezekano wa kutokea vitendo vya kihalifu, ili vifaa vyao vibaki salama na waweze kutekeleza majukumu yao vizuri.   Akizungumza wakati wa ziara yake ya kukagua eneo la ofisi hiyo katika shehia ya Pandani ikiwa ni muendelezo wa kudhibiti uhalifu kwenye maeneo mbali mbali, Inspekta huyo alisema, atahakikisha anadhibiti uhalifu na kila mwanajamii anakuwa mlinzi kwa mwenzake.   "Walinzi wawe makini kuhakikisha mali zote zinakuwa salama na iwapo kutatokea uhalifu basi msisite kutoa taarifa mapema kwa Jeshi la Polisi, lakini pia ik

WAMBAA, CHUMBAGENI WALIA ENEO LA BARABARA LILILOKATIKA MWAKA 2017 KUTOTENGENEZWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI wa shehia za Wambaa na Chumbageni wilaya ya Mkoani Pemba, wameikumbusha tena wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, kulifanyia matengenezo ya haraka, eneo la barabara yao lililokotika kwa mvua tokea mwaka 2017. Walisema, eneo hilo tayari kwa mvua za mwaka huu, limeshakatika tena na kuifinya barabara kuu ya Mizingani-Wambaa, jambo ambalo linaweza kusababisha ajali zisizokuwa za lazima. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi leo Mei 29, 2024, kufuatia muendesha baiskeli mmoja kutumbukia eneo hilo, walisema ni muda sasa wamekuwa wakiahidiwa bila ya kutekelezewa ahadi hiyo. Walisema kuwa, eneo hilo sasa limekuuwa tishio zaidi, hasa baada ya kuongezeka kukatika, na huku kukiwa na ongezeko la vyombo vinavyopita eneo hilo. Mmoja kati ya wananchi hao Fatma Abuu Fakih, alisema eneo hilo lilipo kwenye mpindo karibu na kijiji cha Kidutani, sasa limekuwa tishio mara mbili, kwa barabara kuliwa zaidi. Alieleza kuwa, eneo hilo hutumiwa na wa

KATIBU MKUU ABEIDA AWAPA NENO WALEZI WA WATOTO, WAZEE ZANZIBAR

  KATIBU Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee Wazee na Watoto, bi Abeida Rashid Abdallah amewataka walezi wa watoto na wahudumu wa wazee kujifunza mbinu mpya kupitia mitandao ya kijamii ili kuboresha huduma wanazozitoa. Ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo walezi wa watoto Mazizini, wahudumu wa wazee Welezo na Sebleni yaliyofanyika katika ukumbi wa Wazee Sebleni Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja. Bi Abeida amesema endapo watajifunza mbinu za malezi kupitia teknelojia kutarahisisha utekelezaji wa majukumu yao na kukuza ubunifu kwa makundi wanayoyahudumia pamoja na   kusaidia kutoa huduma bora zitakazoimarisha maendeleo ya Wizara na nchi kiujumla. Amewataka wahudumu wa makundi hayo kuongeza nguvu ya ziada kwenye huduma sambamba na kutanguliza imani ya dini zao kwa lengo la kupata malipo hapa duniani na mbele ya Mola wao. Sambamba na hayo amemshukuru na kumpongeza Mhe. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi kwa kuh

WAOMBAJI MIKOPO PEMBA WAPEWA RAI KUIPATA

NA ASHA ABDALLA  ,PEMBA @@@@       KAIMU mkuu wakala wa uwezeshaji Wananchi kiuchumi Ali Mohamed Ali amewataka Wajasiriamali  wazingatie  masharti  na vigezo ambavyo  vinatakiwa katika ukamilishaji wa  kujaza fomu ya kuombea mkopo ili wapatiwe mkopo kwa haraka na kuweza kuyafanya yale  malengo yao waliojiwekea . Aliyasema  hayo  Mei 25 wakati walipokua wakipewa Mafunzo ya kuomba mkopo wa 4 4 2  huko katika ukumbiwa wa baraza la Mji Wilaya ya Chakechake mkoa wa kusini Pemba . Alisema kuwa wajasiriamali ili waweze kuupata mkopo kwa haraka bila usumbufu nilazima wafuate mashatri yote ya kukamilisha vigezo na waondokane nausumbufu ambao utaweza kujitokeza na kuweza kuchelewa kupata mkopo kwamuda wanao taka kupatiwa mkopo huo . Kaimu huyo alisema kua mkopo wa 4 4 2  ulio chini ya Baraza la Mji umeletwa hususani ni kwa  makudi makuu  matatu ambao ndio wanaoweza kupata fursa hiyo yakupatiwa mikopo na kuweza kujiendeleza na  biashara zao ambazo wanataka kuzifanya . "Mkopo huo tumeuandaa k