Skip to main content

Posts

Showing posts from August 17, 2025

MKUFUNZI: "ULINZI, USALAMA WA MWANDISHI WA HABARI UNAANZA NA MWENYEWE’’

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WAANDISHI wa habari nchini,    wametakiwa kuzingatia ulinzi na usalama wao   kwanza ,wanapokuwa katika majukumu yao ya kazi, hasa katika kipindi hiki   cha   uchaguzi mkuu wa vayama vingi nchini.   Akifungua mafunzo kwa waandishi wa habari, huko katika ukumbi wa Wizara ya Fedha Gombani Chake chake Pemba, mkufunzi wa mafunzo hayo Mwandishi Maryam Nassor   ambae amejengewa uwezo na   Umoja wa vilabu vya waandishi wa Habari Tanzania  (UTPC) . na yeye kutakiwa kuipeleka elimu hiyo kwa waandishi wengine     Mkufunzi huyo, amesema   kuwa, ulinzi na usalama wa mwandishi wa Habari unaanza na mwandishi mwenyeye , hivyo kuwataka waandishi hao kuwa makini wanapotimiza majukumu yao.   “   Waandishi wa Habari lazima Kujifunza kusoma mazingira kwa haraka (kama vile maandamano au machafuko) ili kubaki salama wakati munatimiza majukumu yenu”         Amese...

'ATCL' LAZINDUA SAFARI ZAKE ARDHI YA PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ SHIRIKA la Ndege la Tanzania 'ATCL' limerejesha tena huduma zake za usafiri kisiwani Pemba, baada ya miaka 30. Shirika hilo limekuja kivyengine kisiwani Pemba, maana limeanza na punguzo maalum la nauli, na ili kulijua punguzo hilo, unatakiwa kuzitembeleza ofisi zao zilizopo mjini Chake chake mkabala na Ofisi ya CCM. Kwa taarifa zaidi soma hapo chini...... WAZIRI wa Uchukuzi wa Jamuhuri ya Muungano Tanzania Prf: Makame Mbarawa Mnyaa, amesema kuanza kwa safari za Shirika la Ndege la Tanzania ‘ATCL’ kisiwani Pemba, ni eneo jingine la kukifungua kisiwa cha Pemba, kiuchumi, kama ilivyokuwa ahadi ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.  A meyasema hayo leo August 20, 2025 kwenye uzinduzi wa safari za ndege za shirika hilo, hafla iliyofanyika uwanja wa ndege wa Pemba na kusema zitaanzia baina ya kisiwa hicho, Unguja na Tanzania bara. Alisema ATCL, sasa litawarahisihia zaidi wananchi wa Pemba, wakiwemo wafanyabiashara, kufika safari zao kwa wakat...

MTAALAM MALEZI, MAKUZI YA WATOTO: 'WAZAZI ACHENI KUWAITA WATOTO WENU MAJINA MABAYA'

  Na Salma Lusangi, WMJJWW Wazazi na Walezi wameshauriwa kuacha tabia ya kuwaita watoto majina mabaya au kumtusi matusi yasiyostahili pale ambapo mtoto amekosea  kwani tabia hiyo inamuathiri kihisia na kupelekea athari katika mambo mengi ikiwemo ufahamu mdogo  katika masomo yake. Akizungumza katika mafunzo ya Waandishi wa Habari yaliyofanyika mwisho mwa wiki iliyopita Dar es Salaam kuhusu Makuzi, Malezi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto Mkufunzi Sharifa Suleiman kutoka Madrasa Early Childhood Zanzibar amesema baadhi ya Wazazi na walezi huwa na tabia ya kuwaita Watoto wao majina ya Wanyama au matusi yasiyostahiki hali ya ambayo inamuathiri mtoto kiakili.  " Niwajibu wa Mzazi na Mlezi kumuonya watoto anapokosea kwa kumuelekeza mema lakini sio kumwita mtoto jina la mbwa, mshenzi, paka,  mwanaharamu, wewe sio vizuri kwani inamuathiri kiakili”. Amesema Sharifa.  Amehafamishwa kwamba utafiti wa kisayansi umeonesha kadiri mtoto anavyoathirika kihisia ndivyo ubongo wa...

WANAWAKE KUSHIRIKI NYANJA ZOTE

  NA MWANDISHI WETU Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Riziki Pembe Juma amesema ajenda ya Wanawake, Amani na Usalama ni matokeo ya Azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa Na. 1325 (2000) ambalo linazitaka nchi wanachama kuandaa na Kutekeleza mipango ya Kitaifa kwa ajili ya kuhakikisha wanawake wanashiriki kikamikifu katika nyanja zote za amani na Usalama. Mhe. Riziki ameyasema hayo   leo katika Uzinduzi wa Mpango kazi wa Kitaifa wa Kutekeleza ajenda ya Wanawake, Amani na Usalama 2025-2029 katika ukumbi wa Chuo cha Mafunzo ya Ulinzi wa Amani Tanzania, Kunduchi Jijini Dar es salaam, wakati akitoa salamu za Zanzibar juu ya ushiriki wake katika uandaaji wa Mpango kazi wa Kitaifa wa Kutekeleza ajenda ya Wanawake, Amani na Usalama 2025-2029. Amesema Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) Kupitia Sera na Mipango mbali mbali, imetekeleza ajenda hiyo kwa vitendo katika nyanja mbali mbali ikiwemo ushiriki wa wanawake katika uongozi na kuongoza katika n...

WAJASIRIAMALI WAOMBA KUPATIWA MBINU UZALISHAJI BIDHAA BORA

  NA FATMA HAMAD, PEMBA@@@@ WAJASIRIAMALI kisiwani Pemba wameomba kupatiwa elimu ya usarifu wa bidhaa, ili waweze kutengeneza zenye ubora na viwango, ambazo zitauzika katika   soko la ndani na nje ya Pemba. Wajasiriamali hao walitoa ombi hilo katika mafunzo ya ujuzi wa kidijitali yaliyofanyika kituo cha uwalimu TC Wingwi wilaya ya Micheweni Pemba. Biamu Omar Mbrouk mwanakikundi cha hapa kazi cha Wingwi, kinachojishughulisha na utengenezaji wa sabuni, mafuta na unga wa mwani, alisema wamekua wakitengeneza bidhaa, ingawa zinashindwa kupata soko, kutokana na kukosa ubora. Alisema mwani umebainika kuwa ni moja ya dawa inayotibu magonjwa mengi katika mwili wa mwanadamu, hivyo ni vyema kupatiwa elimu, ili wawe wazalishaji bora. ‘’Tunatamani siku moja kuona kwamba, na sisi tunaziuza Tanzania bara na hadi nchi za nje bidhaa zetu, kwani kutatuwezesha kutambulika na pia kuinua uchumi wetu,’’alisema. Ali Khatib Ali mjasiriamali wa kikundi cha Tumuombe Mola cha Makangale, kina...

VIKUNDI VYA WATU WENYE ULEMAVU, VYAONESHWA NJIA KUHIFADHI FEDHA KIUSALAMA

    NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ MFUMO mpya wa kidigitali utasaida kuhifadhi fedha za vikundi vya kuweka na kukopa vya watu wenye ulemavu kwa usalama zaidi, na kuondokana na kuhifadhi kwenye masanduku kama ilivyo sasa. Ameyasema hayo Meneja program wa shirikisho la jumuiya za watu wenye ulemavu (SHIJUWAZA) Sophia Azidihery Leghela, alipokuwa akitoa mafunzo ya kuwajengea uwezo vikundi vya watu wenye ulemavu na wawakilishi wao, ukumbi wa Samail Chake chake Pemba.   Alisema mfumo mpya wa digital utasaidia watu wenye ulemavu kuhifadhi pesa zao kiusalama zaidi wa kuweka na kukopa, ili kuondosha hofu ya kupotea kwa fedha zao.   Alieleza kuwa, lengo la mafunzo hayo ni kujifunza kuhusiana na mfumo wa kuhifadhi, kuweka na kukopa, kwenye vikundi vya kijaluba kwa njia ya digitali kwa watu wenye ulemavu. "Niwatake mutumie mfumo huu wa kidigitali wa kuweka na kukopa kwa kuhifadhi fedha zenu, ili kuondoka na kutia ndani ya masanduku," alifafanua. katia hatua nyin...