Skip to main content

Posts

Showing posts from October 16, 2022

WAJAWAZITO MWAMBE, WAMBAA, KENGEJA WALILIA BARABARA CHAKAVU

  NA HAJI NASSOR, PEMBA WAJAWAZITO wa shehia za Mwambe, Kengeja, Wambaa na Chumbageni wilaya ya Mkoani Pemba, wameomba kufanyiwa matengenezo ya dharura barabara zao, ili zipitike kwa utulivu wakati wote. Walisema, wamekuwa na changamoto ya usafiri kwa salama, kutokana na barabara zao kuharibika kwa kuwepo mashimo yenye kina kirefu. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti, walisema wakati umefika sasa kwa mamlaka husika kuwaonea huruma, kutokana na barabara wanazozitumia kuchakaa. Asha Amini Hilali wa Mwambe alisema, baarabara yao, sasa imekuwa tishio hata kwa garia ya aina gani, kwa kuwepo mashimo yanayohatarisha usalama wao. ‘’Wakati mwengine sisi wajawazito tunalazimika kwenda hospitali ya rufaa ya Abdalla Mzee, lakini wasisi ni kupata mitikisiko kwa ubovu wa barabara,’’alisema. Nae Hamida Machano Makame, alisema mwanzoni mwa mwaka huu, alijifungulia ndani ya gari eneo la Mahuduthi, baada ya gari aliyokuwa akipelekewa hospitali kuingia shimoni na kuka

WAJUMBE WATORO KAMATI YA SIKU 16 KUPINGA UDHALILISHAJI WAOMBWA JAMBO PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA::::: WAJUMBE wa kamati ya kuelekea kilele cha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kisiwani Pemba, wameombwa kuacha dharura zisizo za msingi, na kushiriki kikamilifu katika vikao vya matayarisho.   Kauli hiyo, imetolewa Oktoba 20, mwaka 2022 na Katibu wa muda wa kamati hiyo, Safia Saleh Sultan kwenye kikao kazi cha kupanga mikakati na namna ya kufanikisha kilele hicho, kilichofanyika Kituo cha Huduma za sheria Zanzibar ‘ZLSC’ tawi la Pemba.   Alisema jambo hilo ni jepesi mno kulifanikisha, ikiwa wajumbe waliojikubalisha kuingia kwenye kamati hiyo, watahudhuria kwenye vikao vinavyoitwishwa.   Alieleza kuwa, kutokana na mpangilio walivyofikiria kufanikisha siku 16 za kupinga udhalilishaji, unaweza kufanikiwa ikiwa wajumbe hawatokatisha vikao vinavyoitwisha kila muda.   ‘’Moja ya changamoto kubwa ni wajumbe kujaa dharura wakati tunapoendesha vikao vyetu, sasa kwanza waje kisha tuone tunafanikisha shughuli yetu kwa wepesi,’’alieleza.   Katik

TUME YA TAIFA UNESCO YAWAFARIJI WAHANGA AJALI YA MOTO ZANZIBAR

  NA HAJI NASSOR, ALIPOKUWA UNGUJA TUME ya taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzanian imesema iliguswa mno na ajali ya moto iliyoteketeza nyumba za familia 19 mwezi August mwaka huu eneno la mji Mkongwe Zanzibar na mtu mmoja kufariki. Kauli hiyo imetolewa na Katibu mtendaji wa tume hiyo katika hatuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Kaimu Katibu Aboud Idd Khamis kwenye hafla ya kukabidhi ubani wa fedha taslim kwa wahanga hao hafla iliyofanyika nyumba za wazee Sebleni mjini Zanzibar. Alisema UNESCO ni sehemu ya familia ya mji Mkongwe na jamii kwa ujumla hivyo iliguswa na kuhuzunishwa mno na ajali hiyo ambayo pia mtu mmoja alifariki dunia. Kaimu Katibu huyo mtendaji alieleza kuwa ajali hiyo ilipoteza pia mali za wakaazi wa shehia ya Kiponda kufuatia kukosa muda wa kuziokoa ingawa hilo ni mipango ya Muumba. '"Sisi tulipopata taarifa hii kwa kweli tulikosa amani na kuwakumbuka mno binadamu wenzetu na hasa kwa vile kulikuwa na kifo na majeruhi,"alisema. Katika hatua

WAKAAZI KIBOJE WAIPA TANO WIZARA YA NISHATI ZANZIBAR KUTIMIZA AHADI

  NA SALMA LUSANGI, ZANZIBAR WAKAAZI wa kijiji cha Kinooni Shehia ya Kiboje Mkoa wa Kusini Unguja wameishukuru Serikali  kupitia Wizara ya Maji Nishati na Maadini Zanzibar kwa kutimiza ahadi ya kuwafikishia huduma ya umeme ndani ya wiki moja  ili waondokane na gharama za kutumia umeme wa jenereta.           Wakizungumza mara baada ya kupatiwa huduma hiyo wananchi hao walisema hawana budi kutoa shukrani zao hizo kutokana na sasa watapata unafuu mkubwa wa utumiaji wa huduma hiyo ya umeme kwa kutumia jenereta ambapo gharama zake ilikuwa ni kubwa.     Bi Yusta Clauzi alisema jitihada ambazo zinafanywa na Serikali kama wananchi wanapasawa kuunga mkono kutokana na viongozi wao kuonesha utayari wa kuwatumikia wananchi wake.   “Hatuna budi kutoa shukrani zetu kwa Serikari na pia tumpongeze Naibu Waziri wa Maji Nishati na Madini Shaaban Ali Othman ambaye alituahidi kutufikishia umeme katika eneo letu na leo tumeshuhudia ukeli wake’’, alisema.   Alisema Naibu waziri huyo alifika kusikiliza malal