Skip to main content

Posts

Showing posts from June 26, 2022

MVUTANO WA TAFSIRI NANI MTOTO KIKWAZO KUTOKOMEZA NDOA, MIMBA ZA UMRI MDOGO ZANZIBAR

    Na Haji Nassor, PEMBA “Moto ni mtu aliechini ya miaka 18’’ ndivyo sheria namba 6 ya mtoto ya mwaka 2011 ya Zanzibar inavyotoa tafsiri ya nani mtoto.   Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, yenyewe imeridhia kuwa mtu hatoweza kupiga kuram kama iwapo hatotimizia masharti yaliopo likiwemo la kufikia umri wa miaka 18.   Nayo katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, imekwenda mbali zaidi kwamba mtu hatochaguliwa kuwa rais kama hajatimiza umri wa miaka 40.   Huku taifa la Tanzania likifatua katiba mpya, hata rasimu ya awali ya katiba hiyo iliotolewa Juni 3 mwaka 2013, pamoja na mambo mengine, imerudi ikitaja umri wa miaka 18 ndio wa mtu uzima ndani taifa hili.   Tafsiri hii, imekuwa ikiiumisha kichwa jamii ya Zanzibar ambayo asilimia 99, imekuwa ikifuata Imani ya dini ya kiislamu na kuwepo kwa tofauti kubwa.   Ingawa tasfsiri ya nani mtoto huja kutokana na mazingira yake, na ndio maana kumbu kumbu zinaonyesha kuwa hata wakati wa ukoloni baadhi ya sheri

MADAKTARI WAIBUA JANGA JIPYA KWA WAGONJWA WANAWAKE PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:::- KELELE zinazopigwa na Serikali na jumuiya mbali mbali za kukemea vitendo vya udhalilishaji na ukatili wa watoto, bado wapo wanaotia pamba za masikio.   Cha ajabu na chakusikitisha, wapo hata wazazi na walezi, waalimu na sasa hata kumeibuka wale watoa huduma wa afya, kutajwa katika hilo. Mwaka 2019, kama ilikuwa kisirani kwa watoto na wanawake, kufanyiwa ukatili na udhalilishaji na madaktari kisiwani Pemba. Mfano Novemba 21, mwaka 2019, katika hospitali ya Chake chake, daktari wa kitengo cha Atrasaund, alishikiliwa na ZAECA kwa tuhuma za kuomba rushwa ya ngono kwa mjamzito, kama sharti la kumpa huduma. Kisha kesi hiyo baada ya uchunguzi na kuhojiwa, alifikishwa mahakamani, ingawa Januari 1, mwaka jana aliachiwa huru, kwa sababu mbali mbali zikiwemo ushahidi kutoumuunganisha na kesi Aidha Disemba 18, mwaka 2019, TBC 1 iliripoti Afisa Muuguzi msaidizi wa kituo cha Afya Mamba mkoani Katavi kushikiliwa na Jeshi la Polisi, kwa tuhuma za kumbaka mjamz

MWANAMKE PEMBA AFARIKI KWA AJALI YA PIKIPIKI

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA MWANAMKE mmoja aliejulikana na jina la Tahiya Mbarouk Ali mwenye umri wa miaka 22 mkaazi wa Kifundi Konde amefariki dunia baada ya kuanguka kwenye pikipiki katika eneo la Konde Vilima Vitatu Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba. Mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa, dada huyo kabla ya kufikwa na umauti, alikuwa amepakiwa kwenye pikipiki na mume wake akitokea Konde kwenda Wete na walipofika Vilima Vitatu alianguka na kuumia kichwa. Walisema kuwa, sababu ya ajali hiyo ni kutokana na baibui la dada huyo kuingia kwenye pikipiki hilo na kusababisha kuanguka, ambapo aliangukia kichwa na kufariki. Jirani wa dada huyo Saada Said alieleza kuwa, aliondoka nyumbani kwake kwenda kazini Wete, ambapo alimwambia mume wake ampeleke, kwani alikuwa ameshachelewa. ‘’Kwa kweli ni mitihani kwa sababu hivi karibuni mumewe alimgonga mwanafunzi na kufariki na leo ameshapata ajali nyengine na mke wake amefariki’’, alihadithia dada huyo. Kamanda wa Polisi M

WAZAZI WAONESHWA NJIA KUFANIKISHA MAENDELEO YA ELIMU KWA WATOTO

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA JAMII imetakiwa kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika zoezi zima la ufundishaji na ujifunzaji kuanzia kwenye ngazi ya familia kwa kuwasaidia watoto na kumtengenezea mwanafunzi mazingira rafiki ya kujifunza kwa urahisi. Hayo yameelezwa na Meneja Mwandamizi wa Uratibu na Programu katika mradi wa Boresha Elimu ya Sekondari Zanzibar, John Masenza katika mafunzo ya kuwajengea uwezo walimu wa Hesabati, Sayansi na Kiengereza. Alisema kuwa, ikiwa jamii itashiriki kikamilifu katika ufundishaji na ujifunzaji itasaidia wanafunzi kupata maarifa kwa urahisi hususani katika masomo ya Hesabati, Sayansi na Kiengereza ambayo kwa sehemu kubwa yameonekana kuwa na changamoto kwa elimu ya Sekondari. “Mradi huu tunautekeleza Zanzibar na tunakududia kuwafikia walengwa 220,000 wakiwemo walimu, wanafunzi, kamati za skuli, wakaguzi na wadau wengine wa vituo vya walimu kwenye HUB”, alisema Meneja huyo. Alisema kuwa, katika kufanikisha malengo ya mradi wanakusudia

WATEJA PBZ MTAMBILE WAOMBA STARA KWENYE 'ATM'

  NA HAJI NASSOR, PEMBA WATEJA wanaotumia mashine ya kutolea fedha kwa njia ya kielektroniki ‘ATM-Machine’ ya Benki ya watu wa Zanzibar PBZ, kituo cha Mtambile wilaya ya Mkoani Pemba, wameomba kuwekewa kinga maalum, ili wasionekane na kila mtu, wanapofanya muamala. Walisema kwa sasa, licha ya kuwepo kwa mashine hiyo, ambayo imewapunguzia mafasa ya zaidi ya kilimita 10 kwenda Mkoani, lakini haja ya kujengwa kwa kinga, inahitajika. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, walisema mashine hiyo iko wazi na kila mmoja, anaweza kuona wakati mteja anapofanya muamala. Himid Hija Mjaka wa Mwambe, alisema kukosekana kwa kinga (kibanda) kwenye mashine hiyo ya ‘ATM’ imekuwa ikiwawiya vigumu, wengine kutumia huduma eneo hilo. ‘’Ukitoa fedha kila mmoja anakuona mubashara ‘ live’ hivyo unaweza kuwashawishi wahalifu, mana wanaona kila kitu unachokifanya,’’alisema. Nae Asha Abdalla Abdi wa Kangani, alisema juzi alitaka kufanya muamala wa kutoa fedha, lakini kutokana na kuwepo kwa vijan

SENSA MWARUBAINI KUMALIZA CHANGAMOTO ZA WATU WENYE ULEMAVU, WAOMBWA KUSHIRIKI

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imepanga kufanya sensa ya watu na makaazi, ifikapo Agosti 23, mwaka huu wa 2022. Sensa hufanyika kila baada ya miaka 10, na ya mwisho ni ile iliyofanyika mwaka 2012, ambapo hii ya mwaka 2022 itakuwa ni ya sita kufanyika. Zilizowahi kufanyika ni zile za mwaka 1967 kisha mmwaka 1978, 1988, 2002 na ile ya mwisho 2012. Maana ya Sensa ya Watu na makaazi Ni utaratibu wa kukusanya, kuchambua, kutathmini, kuchapisha na kusambaza takwimu za kidemografia. Lakini pia ni kiuchumi na kijamii kuhusiana na watu wote na makaazi yao katika nchi kwa kipindi maalum. Wapo wanaosema kuwa sensa ni zoezi maalumu lenye lengo la kupata idadi ya watu wote katika nchi, kwa umri na jinsia, mahala wanapoishi na hata hali yao ya elimu. Takwimu hizo za msingi, ndizo zinazoanisha mahitaji halisi ya wananchi yakiwemo makundi maalum, yenye mahitaji maalumu, kwa mfano watu wenye ulemavu, wanawake, watoto, vijana na wazee. Watu wenye u

WANAWAKE WATAJA MATAMU, MACHUNGU KAZI YA UBAHARIA-ZANZIBAR

  NA ABDI SULEIMAN, PEMBA KILA ifikapo Juni 25 ya kila mwaka, dunia huadhimisha siku ya bahari ulimwenguni. Moja ya rasili za asili zenye matumizi lukiki, basi ni bahari iwe kwa usafiri, uvuvi, chanzo cha maji ya kunywa na dawa. Wapo wanaoitumia bahari kuwa ndio chanzo chao kikubwa cha kuwapatia kipato, kutokana na shughuli zao mbali mbali ikiwemo uvuv. Wakati juzi Juni 25, dunia iliadhimisha siku ya bahari, tunapaswa kujiuliza wale walioamua kujiingiza katika shughuli za ubaharia wako hali gani. Ubaharia ni kazi kama zilivyo kazi nyengine, husikii baharia kugoma au kususia kazi kwa sababu moja au mbili tatu kutokea. Miaka yote kazi ya ubaharia ilionekana ni kazi ya wanaume pekee, ingawa kwa sasa hali imekua ikibadilika na hata kwa wanawake kujiingiza.   MABAHARI WANASEMAJE JUU KAZI HIYO “Kwa sasa maisha yamebadilika, ubaharia ni kazi kama zilivyo kazi nyengine, chamsingi ni mtu mwenyewe kujiheshimu na kujitunza hapo utafanikiwa,”amesema bahari Zainab. Zainab Ali Abra