Skip to main content

Posts

Showing posts from June 5, 2022

RC SALAMA ATOA NENO KUHUSU WATOTO NI BAADA YA MATEMBEZI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:::- MKUU wa mkoa wa kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib, leo Juni 11, 2022 ameungana na vilabu vitatu vya mazoezi kikiwemo cha Gombani Fitness Club, na wadau wengine wa haki za mtoto wakiwemo TAMWA, kwenye matembezi maalum ya kuelekea kilele cha siku ya mtoto wa Afrika, hapo Juni 16, mwaka huu. Mkuu huyo wa mkoa, akiongozana na vilabu hivyo vya mazoezi, walianza matembezi yao Polisi Madungu na kumalizia uwanja wa michezo Gombani wilaya ya Chake chake. Baada ya kumalizika kwa mazoezi hayo, pia yaliohudhuriwa na wakuu wa wilaya za Chake chake na Mkoani, Mkuu huyo wa mkoa, aliwataka wanamazoezi hao, kuwa wazazi wema kwa watoto wao. Alisema, wapo baadhi ya wazazi wamekuwa wakijitoa mishipa ya fahamu, kwa kuwabaka watoto wao wa kuwazaa, jambo linalosikitisha. ‘’Kwanza nianze na nyinyi, muwe baba na mama wema kwa watoto wenu, maana sasa hali imekuwa ikitisha kwa majanga wanayofanyiwa watoto wetu,’’alieleza. Hata hivyo, amesema wakati umef

WALIOPO KIZUIZINI WANA HAKI YA KUPATA MSAADA WA KISHERIA?

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:::- ‘’WATU wote ni sawa mbele ya sheria, na wanayo haki, bila ya ubaguzi wowote, kulindwa na kupata haki sawa mbele ya sheria,’’ ndivyo inavyofafanua Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984. Maelekezo hayo utayafuma mara ukiifungua Katiba hiyo, kwenye kifungu chake cha 12 (1), ingwa suala la kupata msaada wa kisheria, haliguswi moja moja, lakini msingi wa hilo upo. Ndio maana hapo sasa, kwa kuzingia msingi huo wa sheria mama yaani Katiba (ground norm),  tunaweza kusema kwa kinywa kipana kuwa, haki ya kupata msaada wa kisheria unamgusa kila mmoja. Nikuulize, msingi wa usawa mbele ya sheria kwenye kifungu hicho cha 12, kweli unaweza kuwa na maana, iwapo wenzetu walioko kizuizini, ambao pia uhuru wao umedhibitiwa wasiwe na haki ya kupata msaada wa kisheria? Kwa hakika, tena kwa jicho hata lisilokuwa na uwana sheria utagundua kuwa, haki ya kupata msaada wa kisheria unawahusu, hata walioko kizuizini. AZIMIO LA HAKI ZA BINADAMU Haki ya mtu kuwa huru, na kutokam

BAADA YA JKU, SASA ZAECA YAMNASA ASKARI WA KMKM PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:::- BAADA ya Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu wa Uchumi Zanzibar ‘ZAECA’ mkoa wa kaskazini Pemba, Juni 3, mwaka huu kumshikilia Askari wa JKU kwa tuhma za kupokea rushwa ya zaidi ya shilingi milioni 2.4, sasa ZAECA siku sita baadae, inamshikilia Askari mwengine safari hii, ni wa Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo ‘KMKM’. Askari huyo wa ‘KMKM’ anashikiliwa na ZAECA kuanzia Juni 9, mwaka huu, akikabiliwa na tuhma tatu tofauti, ikiwemo ya ubadhirifu wa mali kwa kuuza bati za miradi ya UVIKO 19. Askari huyo mwenye namba K 2690 mwenye cheo cha ‘PO’ ametambulika kwa jina la Khamis Ali Pembe miaka 45, mkaazi wa Donge Kitaruni Unguja. Kaimu Kamanda huyo wa ZAECA alisema, kosa la kwanza wanalomshikilia askari huyo wa KMKM, ni ubadhirifu wa mali na mapato, kinyume na kifungu cha 42 (1) (a), kosa la pili ni kutumia vibaya mali, ambapo ni kinyume na kifungu cha 43 (1) na kosa la tatu ni matumizi mabaya ya ofisi. Aidha alieleza kuwa, kwa kosa la ta

UNDP: 'TUMERIDHISHWA NA UBUNIFU WA ZLSC'

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:::- SHIRIKA la Maendeleo la Umoja wa Mataifa ‘UNDP’ limesema limeridhishwa mno, na mbinu iliyobuniwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar 'ZLSC' kisiwani Pemba, kwa kuwafuata wananchi vijijini kuwapa elimu, ushauri na msaada wa kisheria bila ya malipo. Kauli hiyo, imetolewa na Mwakilishi wa shirika hilo kutoka Dar-es Salaam Apilike Gordon, wakati akiwasilimia wananchi wa kijiji cha Tundaua, shehia ya Kilindi wilaya ya Chake chake Pemba, kwenye mkutano wa wazi ulioandaliwa na ‘ZLSC’ kwa wananchi hao. Alisema mfumo ulioandaliwa na ‘ZLSC’ unaonesha dhahiri jinsi Kituo hicho kinavyohakikisha, hakuna mwananchi anaekosa haki yake, kwa kutokujua mfumo wa sheria. Alieleza kuwa, pamoja na kutoa elimu ya sheria, lakini kupitia watendaji wa Kituo hicho na wanasheria wengine, wamekuwa wakiwapa ushauri na msaada wa sheria bila ya malipo. ‘’Wananchi wa Tundaua, nafasi mliopewa na ‘ZLSC’ itumieni kuuliza, kutaka ushauri wa msaada wa kisheria

MNG'ARO WA KANZU, KOFIA ZINAZOVALIWA IJUMAA ZIENDANE NA ROHO ZA WAVAAJI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:::- AMA kwa hakika katika siku saba za wiki, waislamu huvaa mavazi ya stara wakiamini kuwa ndio maamrisho ya Muumba hasa kutokana na kuwepo aya na hadithi zinazoeleza hayo. Suala ka kujistiri kwa waislamu ndio la kwanza katika maisha yao ya kila siku, na wengi wao hufanya hivyo kwa siku zote ingawa kwa siku ya Ijumaa huvaliwa kanzu nyeupe na kofia. Uislamu ndio njia ya maisha sahihi kwa mwanadamu, maana kila kitu kilichopo duniani kimeelezwa ndani ya uislamu, jinsi ya kutenda au kuacha kutenda jambo hilo. Roho za watu na kusaidiana nalo halikuachwa ndani ya uislamu na kumbe sio mavazi pekee kama wengine wanavyofikiria kwa kule kuvaa vazi hilo kila siku ya Ijumaa. Ndio maana leo naja kwenu waislamu kuwataka ule mng’aro wa kanzu na kofia zenye kupendeza zinazovaliwa siku ya Ijumaa ni vyema zikaendana na roho za watu. Maana uislamu wala haupendi kuona mvaaji wa kanzu na kofia nzuri na kukimbilia msikitini mapema, ikawa nafsi yake imetawaliwa na choyo, r

WASOMI WANAOSUBIRI UTEUZI WA RAIS WANAITENDEA HAKI ELIMU YAO?

                   NA HAJI NASSOR, PEMBA KILA leo serikali hii ya Mapinduzi ya Zanzibar, imekuwa ikitumia gharama kubwa na hadi kufikia kutoa mikopo, ili kuhakikisha wananchi wake wanapata elimu ya juu kwa maslahi yao na taifa kwa ujumla. Siamini kabisa, kwamba eti serikali hii itumie gharama ya kuwasomesha watu kisha wakirudi masomoni, waje wakae vibarazani wasubiri uteuzi wa rais, la hasha bali ni kuisaidia nchi kufikia uchumi wakati. Maana wapo wasomi walioandika vitabu na tunavisoma   leo hii wakisema kuwa, ili nchi iendelee basi chachu yake kubwa ni kwa wasomi wa ndani kutumia elimu yao kwa ajili maendeleo. Sasa leo nawauliza hawa wasomi wetu wenye chungu na darzeni ya digrii, kama sio masta na PHD wamalizapo vyuo vikuu na kurudi nchini, mbona hatuwaoni wakifanya jambo au wasubiri uteuzi wa rais? Jamani wasomi wetu kama hili ni kweli kwamba mmelewa na kusubiri uteuzi wa rais ili ushike nafasi fulani, je kwa mtindo huo ndio tutaufikia uchumi wa kati. Maana zipo nchi a

CHAPO: 'KARIBUNI WASAIDIZI WA SHERIA WAPYA CHAKE CHAKE'

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:::- MKURUGENZI wa Jumuiya ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake 'CHAPO' Nassor Bilali Ali, amewataka wasaidizi wa sheria wapya, wa majimbo ya wilaya hiyo, kufanyakazi kwa bidi, ili kuisaidia jamii, kupunguza matendo ya udhalilishaji. Alisema, jamii inakabiliwa na majanga kadhaa pamoja na utumiaji wa dawa za kulevya, migogoro ya ndoa, ardhi na matunzo ya watoto, hivyo ni wajibu wao kuona hayo yanapungua. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, baada ya kuwapokea wasaidizi hao wa sheria, alisema amefarajika kuona, Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria, imewapa mafunzo vijana hao. Alisema, moja ya eneo la Zanzibar ambalo haliko salama na majanga mbali mbali ni wilaya ya Chake chake, hivyo wasaidizi hao wa sheria, wanayokazi ya kufanya ndani ya jamii. ‘’Karibuni sana kwenye jumuiya yetu hii, na sisi tumefarajika kuona, tumepata damu changa ya kupambana na majanga mbali mbali, ili tuwe na taifa lenye amani,’’alieleza. Aidha Mkurugenzi huyo

RC KUSINI PEMBA: 'TUJIPE MNAUPIGA MWINGI MAPAMBANO DHIDI YA UDHALILISHAJI'

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:::- MKUU wa Mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahoro Massoud, amesema mchango na juhudi za kupambana na ukatili na udhalilishaji, zinazofanywa na Jumuiya ya Tumaini Jipya Pemba TUJIPE, kama zitaungwa mkono, matendo hayo yanaweza kuwa historia hapo baadae. Alisema, moja ya tasisi inayofanya kazi ya kushirikiana na jamii na ngazi ya serikali ni TUJIPE, hivyo ni wakati kwa wadau wa haki za wanawake na watoto, kuwaunga mkono katika mapambano hayo. Mkuu huyo wa Mkoa, aliyasema hayo Gombani Chake chake leo Juni 6, 2022, wakati akizungumza kwenye kongamano la kujadili changamoto za vitendo vya ukatili na udhalilishaji, lililoandaliwa na ‘TUJIPE’ kwa ufadhili wa the foundation for Civil Society. Alisema, wanaofikiria kuwa serikali pekee inaweza kumaliza matendo hayo ndani ya jamii amekosea, bali juhudi kama za TUJIPE na wengine, wakiungana ni njia moja wapo ya kupunguza matendo hayo. ‘’TUJIPE mmekuwa mkinialika mara kwa mara, katika mikutano au makon

CHIPUKIZI BINGWA FA CUP PEMBA

  NA JAFFAR ABDALLA, PEMBA TIMU ya Chipukizi ya mjini Chake chake Pemba, imefanikiwa kuwaondoa wahasimu wao wa jadi kwenuye soka, timu ya Tekeleza, katika michuano ya kombe la FA CUP, baada ya kuwanagusha kwa mwagoli 2-1. Kufanikiwa kwa Chipukizi kumetokana na kuiotwanga timu hiyo magoli hayo, ni katika mchezo wa fainali ya kutafuta bingwa wa Pemba. Mchezo huo uliyopigwa katika dimba la Gombani, ulihudhuriwa na washabiki wengi kiasi wa soka kutoka kila kona ya kisiwa cha Pemba, kutokana ngebe za timu hizo. Tekeleza ndio iliyotangulia kuliona lango la Chipukizi, kwa bao safi lililofungwa kwenye dakika ya 34 kupitia Khalfan Abdalla. Licha ya Chupukizi kuongeza kasi kwenye dakika 45 za awai, lakini timu hizo zilikwenda mapumziko ikiwa Tekeleza iko mbele kwa bao hilo. Ngwe ya lala salama, timu zote zilirudi na nguvu mpya, huku kila upande ukifanya mabadiliko, na Chipukizi kusawazisha bao hilo kupitia kwa Mundhir Iman, dakika ya 57. Baada ya goli hilo washambul

ZAECA PEMBA YAMDAKA ASKARI JKU

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MAMLAKA ya Kuzuia rushwa na Uhujumu wa Uchumi Zanzibar 'ZAECA' Pemba, inamshikilia Askari wa Jeshi la Kujenga Uchumi Zanzibar 'JKU' kisiwani Pemba, kwa tuhuma za kupokea rushwa, kwa hadaa ya kuwaajiri vijana ajira ya kikosi hicho. Akizungumza na waandishi wa habari Kaimu Kamanda wa ZAECA Mkoa wa kaskazini Pemba' Nassor Hassan Nassir, alisema askari huyo anayetambuliwa kwa jina la Zaharan Mohamed Zaharan miaka 33 mkaazi wa Chokocho wilaya ya Mkoani Pemba. Alisema ZAECA inamshikilia askari huyo kwa kosa la rushwa 'ubadhirifu wa mali na mapato' chini ya kifungu cha 43 (1) (a) cha sheria  Mamlaka ya Kuzuia rushwa na Uhujumu wa Uchuni nambari 1 ya mwaka 2012. Alieleza kuwa, mtuhumiwa huyo kwa nyakati tofauti mwaka huu 2022, akiwa mtumishi wa Jeshi la Kujenga Uchumi Zanzibar 'JKU' akiwa na cheo cha private, bila ya halali alijipatia fedha kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 2.4. Kamanda huyo wa ZAECA alifafanua kuwa askari huyo akij

MASHAHIDI KESI YA DAKTARI IS-HAKA PEMBA WAANZA KUFANYA MAAJABU YAO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:::- MAHAKAMA ya Mkoa Wete, imelazimika kumrejesha tena rumande hadi Juni 15 mwaka huu, daktari Is-haka Rashid Hadid, wa kituo cha afya Gombani, anayedaiwa kumbaka mara tatu, mtoto wa miaka 16, baada ya upande wa mashataka kutopokea mashahidi. Awali daktari huyo, alipelekwa rumade kauanzia Mei 18, mwaka huu na kutakiwa kurudi tena mahakamani hapo Juni 1, ili kuwasikiliza mashahidi. Ingawa upande wa mashataka siku hiyo, haukupokea mashahidi, na mtuhumiwa huyo kulazimika kurejeshwa tena rumande hadi Juni 15, mwaka huu. Mara baada ya mtuhumiwa kuwasili mahakamani hapo akitokea rumande, chini ya hakimu wa mahakama maalum ya makosa ya udhalilishaji, Mwendesha mashataka Juma Mussa aliomba shauri hilo kughgirishwa. Alidai kuwa, leo Juni 1, (jana), walitarajia kuwapokea mashahidi, ingawa hawakufika mahakamani hapo na kuiomba mahakama hiyo, kulighairisha shauri hilo. ‘’Mheshimiwa hakimu, tulirajia sana leo (jana), kuwapokea mashahidi, lakini hawakutokeza mahak