Skip to main content

Posts

Showing posts from October 29, 2023

SHAHIDI DAKTARI: ''NILIGUNDUA MAREHEMU ALISHAMBULIWA KWA MARUNGU''

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ SHAHIDI nambari 14 kwenye kesi ya mauwaji, ambae ni Daktari wa hospitali ya Vitongoji Chake chake Pemba Ali Juma Ali, amedai mahakamani kuwa, baada ya uchunguzi alibaini kuwa, mjeruhiwa alishambuliwa kwa vitu vyenye cha kali na silaha mfano wa marungu. Alidai kuwa, wakati akiwa kazini kwake hospitalini hapo, Septemba 21, mwaka 2021, alimpokea mjeruhumiwa Suleiman Said Saleh (55) akiwa katika hali mbaya. Shahidi huyo akiongozwa na Wakili wa serikali kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Ali Amour Makame, mbele ya Jaji wa mahakama kuu Zanzibar Ibrahim Mzee Ibrahimu, alidai kuwa uchunguuzi ukabini kuwa kina cha jeraha la kichwani ni nchi nne kwa upana na urefu nchi mbili. Alidai kuwa, jeraha jingine ambalo lilikuwa bega la mkono wa kushoto, lilikuwa na nchi tatu kwa urefu na kina cha kwenda chini likuwa nchi mbili. Akiendelea kuongozwa na Wakili wake, shahidi huyo alidai kuwa, wakati anamfanyia uchunguuzi, alibaini pia mkoja wake wakati ukitoka uli

WAZEE WATAKA UZEE UTAMBULIWE KWA MIAKA 60 NA SI0 70

  Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Abeida  Rashid Abdallah amesema Wizara hiyo imepokea maoni yaliyotolewa na Wazee kuhusu kuifanyia marekebisho sheria ya Masuala ya Wazee, sheria namba mbili (2) ya mwaka 2020 katika kifungu kinachozungumzia umri wa mzee. Akizungumza baada ya kikao cha pamoja baina ya watendaji wa wizara hiyo ,Kamati ya Kanuni na Sheria ndogo ndogo ya Baraza la Wawakilishi, wazee kutoka Jumuiya ya wazee (JUWAZA) pamoja na wazee wanaoishi katika makao ya wazee, kilichofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita katika ukumbi wa Makao ya Wazee Sebleni, Unguja. Alisema wazee wametaka kifungu cha sheria hiyo kifanyiwe marekebisho umri wa mzee uwe miaka 60 badala ya miaka 70. Hivyo watendaji wa wizara hiyo watakaa chini na kutafakari. “Kamati imekuja kututembelea katika makao ya wazee, pamoja kupata maoni ya kanuni, ya masuala ya wazee iliyotungwa hivi karibuni lakini majadala mkubwa umejitokeza, baada ya kanuni hiyo kuonesha umri wa mzee ni miaka 7