Skip to main content

Posts

Showing posts with the label UWEKEZAJI

TUNDAUA WATAKA UFAFANUZI MWEKEZAJI ALIWEKA VIKUTA PEMBEZONI MWA BAHARI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@ WANANCHI wa kijiji cha Tundaua shehia ya Kilindi wilaya ya Chake chake, wamesema hawakatai uwekezaji katika maeneo yao, wanachotaka ni kushirikishwa kila hatua, kuelekea uwekezaji huo. Walisema, kwa sasa wamekuwa wakiona uwekaji wa vikuta ‘bacons’ pembezoni mwa bahari, ndani ya maeneo wanayolima mihogo, mpunga na mboga mboga, bila ya taarifa yoyote kutoka serikalini. Wakizungumza na waandishi wa habari, kufuatia uwepo wa vikuta hivyo, kwenye eneo wanaloendesha kilimo, walisema kinachowasikitisha ni kukosa taarifa, juu ya aina ya uwekezaji huo. Walieleza kuwa, hawajapata taarifa kutoka kwa sheha wao, wala kiongozi mwingine yoyote, na kuwaacha njia panda juu ya zoezi ambalo, limeshakamilika la uwekaji wa vikuta. Mmoja kati ya wananchi hao Makame Haji Makame, alisema ingawa wao hawajakwenda kulalamikia jambo hilo kwa sheha wao, lakini na yeye hajaita kuwapa taarifa zozote. Alisema kama ni suala la uwekazaji, walifikiria kuwa, wengeitwa kwenye ...

PEMBA SASA KUEKEZA NI DOLA MILIONI 10 KUTOKA 100 ZA AWALI

                                     NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ SERIKALI ya awamu ya nane inayoongozwa na Dk. Hussein Ali Mwinyi imedhamiria kwa vitendo kukiinua kisiwa cha Pemba kiuchumi. Hii imekuja, baada ya kuonekana kisiwa cha Pemba kwa miaka mingi, kimeachwa nyuma, katika masuala ya ukuaji wa uchumi. Lakini Dk. Mwinyi, hakuwa nyuma katika kuhakikisha wananchi wa Pemba wanapata maendeleo kama wenzao wa Unguja, na ndio maana akatenga maeneo maalum, kwa ajili ya uwekezaji mkakati. Na miongoni mwa mambo, ambayo ameyafanya ili kuvutia wawekezaji ni kuimarisha miundombinu mbali mbali, pamoja na kuweka punguzo la bei kwa mwekezaji atakaeekeza. Kuna mpango wa kujengwa uwanja wa ndege wa kimataifa, bandari ya kisasa pamoja na kuimarisha miundombinu ya barabara, umeme na maji katika maeneo yaliyotengwa kwa uwekezaji, ili uwekezaji uwe wa kiwango kizuri. Kutokana na punguzo la bei lililo...