Skip to main content

Posts

Showing posts from December 3, 2023

HAMA HAMA WATUMISHI WA UMMA, IPA YAGUNDUA JAMBO

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ CHUO cha Utawala wa Umma Zanzibar ‘IPA’ kimegundua sababu mbali mbali, zinazowafanya watumishi wa umma, kuhama sehemu moja kwenda nyingine, ikiwemo mabadiliko ya sayansi na teknolojia. IPA imegundua sababu nyingine kuwa ni, miundo ya kiutumishi, maslahi na ndoa kwa watumishi wanawake na wanaume, kwa kumfuata mwenzake sehmu alipo kimakaazi. Hayo yameelezwa leo Disemba 8, 2023, na Mkuu wa Divisheni ya Utafiti na Ushauri Elekezi kutoka ‘IPA’ Haji Jumbe Haji, wakati akizungumza kwenye uwasilishaji wa matokeo ya awali wa tafiti nne walizozifanya, kwenye hafla iliyofanyika ukumbi wa Chuo, hicho mjini Chake chake. Alisema, sababu hizo na nyingine, zinazowafanya watumishi wahame kutoka sehemu moja kwenda nyingine, wakati mwingine huathiri mtiririko mzuri wa kazi za sekta ya umma. Alisema, tafiti hizo ambazo walizifanya katika mwaka wa fedha wa 2020/2021, zilichukua takriban miezi sita hadi kukamilika kwake, ambapo watendaji mbali mbali wa sekta za umma z

WANAWAKE WAKULIMA WA MWANI PEMBA WAMALIZA MAFUNZO YA KUOGELEA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAWAKE wanaolima na kilimo cha mwani cha kina kirefu, wa kijiji cha Tundaua shehia ya Kilindi wilaya ya Chake chake Pemba, wamesema baada ya kumalizika kwa mafunzo ya siku 15, sasa wanajiamini kuogelea, hadi urefu wa uwanja wa mpira wa miguu bila ya kupumzika. Walisema, mafunzo hayo, yamewajengea uthubutu wa kuogelea na hata kuokoana, pindi ikitokezea ajali wakati wa kwenda ama kurudi kwenye shughuli yao ya kilimo cha mwani, kwenye maji yenye kina kirefu. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, kwenye bahari ya Tundaua walikokuwa wakifundishwa, walisema kwa sasa wamejitoa woga na wanajiamini kogelea hadi mita 100 (urefu wa uwanja wa mpira wa miguu), bila ya kumpunzika. Walieleza kuwa, wazo lililoibuliwa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar kipitia Idara ya Mazingira chini ya mradi wa ‘SAPPHIRE’ umekuja kuwapa uhakika wa kazi zao. Mmoja kati ya wanufaika wa mafunzo hayo ambae ni mkulima wa mwani wa kina kirefu, Hassina Seif Baki, alis

WAVUVI WA DAGAA WESHA WATAKIWA KUZINGATIA HILI KWANZA.................

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WAVUVI wa dagaa wa shehia ya Wesha wilaya ya Chake chake Pemba, wamekumbushwa kujiwekea mazingira ya usafi, kuanzia nguo wanazovaa, madau yao pamoja na vyombo vyingine wanavyotumia, ili kuliongezea thamani dagaa lao. Ushauri huo umetolewa leo Disemba 6, 2023  na Mratibu wa Mradi wa Kuimarisha Jamii kwa kuzingatia Ikolojia na shughuli za kijipatia kipato, kwa wavuvi wadogo katika eneo la hifadhi ya mkondo wa Pemba ‘’SAPPHIRE’ Aisha Abdalla Rashid, alipokuwa akifungua mafunzo, kwa wavuvi hao, yaliyofanyika ukumbi wa Manispaa ya Chake chake. Alisema, kwa sasa ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar kupitia Idara ya Mazingira, chini ya mradi huo wa ‘SAPPHIRE’ imeamua kukutana na wavuvi na waanika dagaa, ili kujengea uwezo kwa lengo la kuongeza thamani. Alieleza kuwa, moja ya jambo hilo ni usafi wa wavuvi, kuanzia nguo wanazovaa wakati wanapokwenda kwenye shughuli zao za uvuvi, madau yao na ndoo wanazotumia. ‘’Usafi wa bidhaa ya dagaa kavu au bichi,

WAANIKAJI DAGAA NDAGONI WAPIGWA MSASA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WAANIKAKAJI dagaa wa shehia ya Ndagoni wilaya ya Chake chake Pemba, wameshauriwa kuzitumia njia nzuri za uanikaji, ikiwemo kutumia chanja za miti zilizoinuka ‘chanja’ ili kuepusha vumbi na taka taka, zinzoweza kupunguza thamani ya bidhaa hiyo. Walielezwa kuwa, njia nyingine ambayo ni nzuri kwa uanikaji na kutumia sakafu iliyasafi, ambayo ni vyema ikazungumshiwa kinga maalum, ambayo itazuia taka taka na wanyama kuliharibu wakati wa uanikaji. Hayo yamelezwa na Kaimu Afisa Mkuu Idara ya Maendeleo ya Uvuvi na Mazao ya Baharini Pemba Mayasa Hamad Ali, wakati akitoa mada njia ya uanikaji bora dagaa, kwa waanikaji na wavuvi wa shehia ya Ndagoni, mafunzo yaliyofanyika ukumbi wa Manispaa ya Chake chake. Alisema, njia nyingine ambayo waanikaji wanapaswa kuitumia ni kutumia wavu, ambao kitaratibu hutakiwa kuwekwa juu juu, ili kuhakikisha dagaa haliingii wadudu na taka taka. Alieleza kuwa, njia hizo pamoja na ile ya kutumia moshi kwa magamba ya miti maalum,