Skip to main content

Posts

Showing posts from September 15, 2024

JAMII TOENI USHAHIDI MAHKAMANI KESI ZIPATE HATIA

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ WANAJAMII wametakiwa kuwa makini katika suala la kutoa ushahidi mahakamani, kwani ndio unaoweza kumtia hatiani mshitakiwa au kumuachia huru. Azungumza na wananchi wa Daya shehia ya Mtambwe Kusini, Hakimu wa Mahakama ya Wilaya Wete Maulid Hamad Ali alisema, ushahidi ni kitu muhimu katika kesi, hivyo kuna haja ya kutoa ushahidi kwa kina pale unapohitajika. Alisema kuwa, kuna makosa mbali mbali yanayotendeka katika jamii ikiwemo ya udhalilishaji, wizi na madawa ya kulevya, hivyo wasipokuwa makini katika kutoa ushahidi, washtakiwa wataendelea kuachiwa huru huku wanajamii wataendelea kulalamika. ‘’Ushahidi ndo ambao utamtia mshtakiwa hatiani au kuachiwa huru, kwa sababu unaangaliwa uzito wa ushahidi, hivyo tuwe makini tunapokwenda mahakamani kutoa ushahidi,’’ alisema Hakimu huyo. Aidha aliwataka vijana kuacha kutumia madawa ya kulevya kwani yanasababisha kujiingiza katika mambo maovu ikiwemo kuiba na hatima yake kuishia chuo cha mafunzo. Alisema kuwa, v

WATEULE 'EJAT' MWAKA 2023/2024 HAWA HAPA

                                 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Dar es Salaam, Alhamis, Septemba 19, 2024   MAJAJI saba wa Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari Tanzania (EJAT) wamehitimisha kazi ya kutathmini ubora na weledi wa kazi zipatazo 1,135 na kuwateua waandishi wa habari 72 watakaoingia katika kinyang’anyiro cha kumtambua mshindi wa kwanza, wa pili na wa tatu na mshindi wa jumla. Kati ya waandishi wa habari 72, wanaume ni 45 (sawa na 62.5%) na wanawake 27 (sawa na 37.5%). Kati ya wateule hao, wateule 14 (19%) wanatoka katika runinga; 13 (18%) wanatoka vyombo vya mtandaoni, redio 20 (28%) na wateule 25 (35%) wanatoka kwenye magazeti. Wateule wamepatikana kwa kukidhi vigezo vya ubora ambavyo ni pamoja na ukweli, usahihi, uanuai, haki, kina, utafiti, ubunifu, uvumbuzi, upekee, uchambuzi, uwajibikaji, ufichuaji maovu, uadilifu, uwasilishaji unaoeleweka na uchunguzi. Ifahamike pia kwamba vigezo maalum vilitumika kuzingatia aina tofauti ya vyombo vya habari kama vile redio, televishe