Skip to main content

Posts

Showing posts from March 17, 2024

WANAKISOMO CHA WATU WAZIMA WAOMBA MIWANI YA KUSOMEA

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ WANAKISOMO cha madarasa ya Elimu ya watu wazima kisiwani Pemba wameiomba Wizara pamoja na wafadhili kuwasaidia miwani, ili waepukane na usumbufu wakati wa kusoma na kuandika. Walisema kuwa, madarasa hayo ambayo kwa asilimia kubwa ni wanafunzi watu wazima, wakati mwengine wanashindwa kusoma wala kuandika kutokana na kupungua kwa nuru ya macho. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi katika vijiji tofauti, ikiwemo Mjinikiuyu shehia ya Minungwini Wilaya ya Wete,wanakisomo hao walisema wana shauku ya kujifunza zaidi ingawa wakati mwengine inawapa wakati mgumu kuhudhuria darasa. Walisema kuwa, kuna haja kwa Wizara ya Elimu pamoja na wafadhili wengine kuwasaidia kwa kuwapatia miwani, ili wahudhurie darasani wakiwa na hamasa ya kusoma na kuandika kwa bidii. Mmoja wa wanafunzi hao Viwe Yusuf Malik mwenye miaka 70 alieleza kuwa, anahudhuria darasa siku zote walizopangiwa lakini inapofika wakati wa kuandika ama anapoambiwa asome kwenye ubao macho yanamsumbua sana. &q

DK. SALUM AWAKOLEZA MWENDO WANAOSHUGHULIKIA KESI ZA UDHALILISHAJI

  Mkurugenzi wa Idara ya Uendeshaji na Utumishi kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Salum Khamis Rashid amewataka maafisa ustawi kusimamia vyema kesi za udhalilishwa na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia ili kuendelea kuimarisha hali ya ustawi nchini.   Amesema hayo jana wakati akifungua kungamano la maafisa ustawi kutoka wizara mbali mbali hapa nchini lilifanyika katiak ukumbi wa Sebleni Unguja ikiwa ni   shamrashamra za kuadhimisha siku ya ustawi.   Amesema dhamira ya serikali ni kuondoa kabisa vitendo vya udhalilishaji na ukatili hivyo   maafisa Ustawi wakifanya kazi kwa uweledi wa hali juu na kuondoa muhali katika kusimamia kesi hizo vitendo hivyo vinaweza kutokomezwa kabisa.   Aidha amesema kuendelea kuachiwa na kuoneanaaibu na muhali kunapelekea kuongezeka kwa mmomonyoko wa madili katika jamii na kuzoeleka vitendo hivyo kuwa vya kawaida.   Nao maafisa wa ustawi wameiomba serikali kutoa mafunzo zaidi kwa wanaume kwani wao ndio wahusika