Skip to main content

Posts

Showing posts from January 15, 2023

MADEREVA PEMBA WAKERWA NA WANAFUNZI WANAOPUUZA HONI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:: MADEREVA wa vyombo vya moto kisiwani Pemba, wamewataka wanafunzi wa skuli, kutodharau honi wanazowapigia au mingurumo maalum ya mshine, ili kuepusha ajali zinazoweza kuzuilika. Walisema, wanafunzi waliowengi wamekuwa na tabia ya kudharau honi au mivumo isiyokuwa na kawaida, wanayoifanya ili wakae pembeni, jambo ambalo linaweza kuleta madhara. Wakizungumza na mwandishi wa habari eneo la Ngwachani, ambapo dereva mmoja aliyekataa kutaja jina lake, alipoteremka kwenye gari, kuwaeilimisha wanafunzi waliodharau honi aliyowapigia mara tatu. Alisema, alilazimika kuweka gari pembeni, na kuwapa maneno makali kundi la wanafunzi, baada ya kuwapigia honi na mivumo mikali ya mashine, bila ya kujali. Dereva huyo alieleza kuwa, alikuwa amebeba mzingo akitokea bandarini Mkoani, na alipofika karibu na njia ya Tangaani, aliwapigia honi wanafunzi, ili wakae pembeni, ingawa hawakutii. ‘’Mbele yangu kuna gari mbili za abiria zinafukuzana zikitokezea mjini Chake chake, n

KUSINI WAONGOZA KWA UVAMIZI WA ARDHI- SMZ

                       Taarifa kwa Vyombo vya Habari    Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanzibar imesema kumekua na uvamizi pamoja na uuzaji holela wa maeneo ya ardhi ya akiba kitendo ambacho kinachangia ongezeko la migogoro ya ardhi Zanzibar. Kauli hiyo imetolewa jana na waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanzibar Rahma Kassim Ali alipokutana na Masheha wa Wilaya ya Kusini Unguja, kikao maalum kilichofanyika ofisi za Mkuu wa Wilaya hiyo alisema    kumekua na uvamizi na uuzaji holela wa maeneo ya ardhi ya akiba yaliyotengwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ). Waziri Rahma alisema Wizara yake itahakikisha inaweka mikakati imara ya udhibiti wa uuzaji ardhi kiholela hasa katika maeneo ya ardhi ya akiba yaliyotengwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Aidha alieleza kwamba Wilaya ya Kusini Unguja inaongoza kwa uvamizi na uuzaji wa   ardhi kiholela hasa katika maeneo ya fukwe za bahari yiliyopo wazi   hivyo kutokana uwezo wa wizara yake kupewa dhamana ya usi

Danube Hospitality and AirOWater introduces a sustainable drinking water solution to the MENA region

  BY ZANZIBAR: CORESPONDENT Danube Hospitality, the one-stop, end-to-end solution provider for hospitality businesses for the Middle East is paving the way towards sustainability with its multi category, multi brand tie-ups that employ sustainable practices to supply eco-friendly products and services, helping reduce carbon footprint. The brand has recently signed up extensive assortment of sustainable products for the hospitality and healthcare industry. Governments and decision-makers in different sectors have realized the importance of sustainable, earth-friendly solutions to global problems like scarcity of natural resources, pollution, plastic waste, and other factors that damage the planet.  Danube Hospitality aligns with the thought of the leadership in different sectors to play its part in the sustainability movement that is gaining momentum rapidly.   “Danube Hospitality aims to pioneer the sustainability movement across the MENA region. With our partnership with AirOWater tec

TAMWA-ZNZ YATAKA MABADILIKO YA HARAKA SHERIA MPYA YA HABARI

      Na Muhammed Khamis,TAMWA-ZNZ Chama cha waandishi wa habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA-ZNZ) kimesema kuna haja ya taasisi husika za mabadiliko ya sheria kuweka kipaumbele kufanyiwa marekebisho yanayoendana na matakwa ya wadau katika sheria za habari Zanzibar ili zitoe mazingira ya uwepo wa uhuru wa vyombo vya habari katika kutekeleza majukumu yao.   Mkurugenzi wa Chama hicho Zanzibar, Dkt. Mzuri Issa akizungumza na wandishi wa habari katika mkutano wa kuwasilisha ripoti ya sheria za habari Zanzibar zilizofanyiwa mapitio na TAMWA ZNZ kwa kushirikiana na Shirika la INTERNEWS Tanzania ambazo zinakinza uhuru wa habari pamoja na uhuru wa kujieleza vyombo vya habari alisema uhuru wa habari ni nguzo muhimu katika maendeleo ya taifa. Alisema uhuru wa habari ni nguzo muhimu inayoweza kusaidia kwa kiasi kikubwa ukuzaji wa maendeleo kwenye Nchi hivyo inapotokea sheria ya tasnia hiyo kubana ni sawa na kuchelewesha maendeleo ambayo yanahitajika na kila mtu.   Alieleza, “lazima tufahamu

WATUMISHI WA UMMA: 'MUSIANZISHE MIJDALA YA KUKEBEHI, KUDHARAU MWELEKEO WA SERIKALI' : MDHAMINI THABITI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA: OFISA Mdhamini Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ, Thabit Othman Abdalla, amewataka watumishi wa umma kisiwani Pemba, kutoungana na watu wengine, katika kukebehi na kudharau mipangano, sera na mikakati ya serikali, kwani kufanya hivyo ni ukiukwaji wa maadili ya kazi. Alisema, kila mtumishi wa umma anapofanyakazi katika kitengo na idara yoyote ile, ajue kuwa anamwakilishi kiongozi wa nchi, hivyo lazima asikubali kuwa sehemu ya kuongoza mijadala ya kukibehi mwelekeo wa serikali. Ofisa Mdhamini huyo aliyasema hayo Januari 15, 2023, ukumbi wa mikutano Baraza la mji wa Chake chake, wakati akiyafunga mafunzo ya siku tatu, kama sehemu ya uthibitishwaji wa kazi, kwa watumishi wapya wa umma, yalioendeshwa na Chuo cha Utawala wa Umma ‘IPA’. Alisema, wapo baadhi ya watumishi wa umma kwa kule kutokujua nafasi zao, wamekuwa wakiungana au wakati mwengine kuanzisha mijadala ya kudhoofisha mikakati ya serikali. Alieleza kuwa, kiu

HAKI HAISUBIRIWI, INATAFUTWA: LAZIMA WANANCHI WAWE NA UWELEWA WA HAKI ZAO - WADAU

  ZANZIBAR::: KATIKA kuhakikisha jamii inakuwa na uwezo wa kutambua umuhimu  wa kudai upatikanaji wa haki zao za msingi, kamati za wananchi kutoka shehia za Wilaya za Micheweni, Wete, Mkoani na Chake Chake Pemba zimeshauriwa kuendelea kuwashirikisha wananchi kujadili changamoto zinazowakabili ili kuzipatia ufumbuzi kwa njia na wakati sahihi bila kusababisha madhara. Ushauri huo umetolewa wakati wa mkutano na kamati za wananchi kutoka shehia za wilaya hizo kisiwani Pemba ulioandaliwa na Jumuiya ya Utetezi wa Mazingira na Jinsia Pemba (PEGAO) kwa kushirikiana na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ) kwa lengo la kuzijengea uwezo kamati hizo kufuatilia kero zinazokwaza haki za wanawake ambazo ziliibuliwa na wahamasishaji jamii kwenye maeneo yao. Akizungumza katika mkutano huo ambao ni utekelezaji mradi wa kuwawezesha wanawake kwenye uongozi unaofadhiliwa na Ubalozi wa Norway Tanzania, afisa tathimini na ufuatiliaji wa TAMWA ZNZ, Moh’d Khatib, alihimiza jami

USHIRIKIANO WIZARA ZA ARDHI SMZ, SMT KUIBUA KASI UJENZI NYUMBA NAFUU

Mashirikiano ya Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya   Makaazi ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makaazi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) yanatarajiwa kuibua kasi ya kiutendaji   katika sekta ya ujenzi wa nyumba za bei nafuu ili wananchi waweze kuzimudu. Akizungumza Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi (SMZ) Dkt. Mngereza Mzee Miraji katika kikao cha mashirikiano ya kiutendaji kilichofanyika mwisho wa wiki iliyopita   katika ukumbi wa Wizara hiyo   Maisara Unguja, alisema kupitia vikao   vya mashirikiano baina sekta mbili hizo vitasaidia katika kuibua kasi ya utendaji hasa katika sekta ya ujenzi wa nyumba za bei nafuu zenye kukidhi mahitaji ya wananchi wenye kipato tofauti. Alisema kwamba kunamafanikio yameanza kuonekana kupitia vikao hivyo ikwemo kukamilika rasimu mbili ya makubaliano (MOU) zimekamilika kiutendaji ambapo zitarajiwa kusainiwa katika kikao kijao cha ngazi ya mawaziri wa pande zote mbi