Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

HIVI NDIVYO TAMWA -ZANZIBAR ILIVYOFANIKIWA KUWAJENGA WAANDISHI VIJANA, MASUALA YA WANAWAKE NA UONGOZI

  Na Nihifadhi Abdulla, UNGUJA. Jitihada mbalimbali zinaendelea kuchukuliwa siku hadi siku kuhakikisha usawa wa kijinsia unachukua nafasi yake kwa kupitia mikataba ya kimataifa, kikanda, sera, sheria, matamko na mbinu nyengine tofauti Mpango wa utekelezaji wa beijing katika maelezo ya dhamira namba 7 imeeleza  uezeshaji wa mwanamke na ushiriki katika vyombo vya maamuzi kwa kuangalia uwiano wa jinsia ili kuhakikisha wanawake na wanaume wanapata nafasi sawa ya kushiriki katika ngazi zote za maamuzi Aidha Mkataba wa kikanda wa nchi za kusini mwa afrika kifungu cha 12 kinasisitiza ushiriki sawa wa wanawake kufikia asilimia 50/50 kwenye nyanja za maamuzi, pia kifungu namba 13 kinaeleza kuwekwa mikakati madhubuti ya kuwawezesha wanawake kushiriki katika mchakato mzima wa uchaguzi na upigaji kura na kuondosha mila na desturi potofu zinazopingana na maendeleo ya mwanamke katika siasa na uongozi Chama cha waandishi wa habari wanawake TAMWA Zanzibar ni taasisi inayotetea mambo mengi ya haki ikiw
Recent posts

DIWANI WA KIUYU ADHAMIRIA KUMALIZA KERO NDANI YA WADI YAKE

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA    DIWANI wa Wadi ya Kiuyu Pemba kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Nasra Salum Mohamed amesema, atahakikisha anatatua changamoto zote zinazowakabili wananchi ili kuleta maendeleo katika wadi yake.   Alisema kuwa, ametatua changamoto mbali mbali na anaendelea kushirikiana na wananchi kuziibua changamoto nyengine ili zipatiwe ufumbuzi kwa ajili ya maslahi yao na Taifa kwa ujumla.    Akizungumza na mwandishi wa habari hizi katika wadi yake alisema, baadhi ya changamoto alizotatua ni pamoja na kuhamasisha kujengwa vyumba vinne vya madarasa katika skuli ya Minungwini na vyumba vinne katika skuli ya maandalizi Kangagani.   Mambo mengine aliyoyatatua Diwani huyo ni kuchimba shimo la vyoo (chamber) katika skuli ya Minungwini, kuezeka vyumba viwili vya skuli ya Mjinikiuyu, kujenga matundu manne ya vyoo katika skuli ya tutu Penjewani na ujenzi wa kituo cha Afya Minungwini.   Diwani huyo alisema pia alitatua changamoto ya umeme katika kijiji ch

FCS: YAVUTIWA NA PACSO UTEKELEZAJI MRADI 'URAIA WETU'

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ TAASISI ya The Foundation for Civil Society ya Tanzania bara 'FCS' imesema inaendelea kuridhishwa na utendaji kazi wa Mwemvuli wa asasi za kiraia Pemba ‘PACSO’, katika utekelezaji wa mradi ‘uraia wetu’ hasa kwa kule kuwanganisha wadau husika. Hayo yameelezwa na mwakilishi wa taasisi hiyo Neil Ngala, wakati akitoa salamu zake, kwenye mkutano wa siku moja, wa kuibua changamoto za kisheria na sera, zinazokwaza wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, uliofanyika Gombani Chake chake. Alisema PACSO, imekuwa ikiendelea vyema na utekelezaji wa mradi huo, jambo ambalo limeanza kutoa taswira ya mafanikio yaliyotarajiwa, ikiwa ni pamoja na kuibua changamoto za kisheria na sera. Alieleza kuwa, mradi huo ambo unatekelezwa na taasisi za PACSO, CYD na JUWAUZA kama hatua ya kitaifa, PACSO imekuwa ikifanya vyema kwa kule kuwakutanisha wadau hisika. ‘’Sisi FCS, tumekuwa tukijivunia mno kila tunapofanyakazi na ‘PACSO’ maana kile ambacho wanakifanya, mat

SHAMRA SHAMRA ZA MIAKA 60 YA MUUNGANO, DK . MWINYI AFUNGUA BARABARA MAENEO HURU MICHEWENI

    NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameziagiza taasisi, serikali ya Mkoa na Wilaya kuhakikisha wawekezaji wanaajiri vijana wa maeneo ambayo watawekeza, ili azma ya Serikali kukiinua kisiwa cha Pemba kiuchumi iweze kufikiwa.   Alisema kuwa, sio jambo zuri kuona mwekezaji anaajiri vijana wa mbali na kuwaacha vijana wa eneo husika, hivyo ni vyema lisimamiwe vizuri hilo, ili kuhakikisha wananchi wananufaika na uwekezaji, hali ambayo itasaidia kukuza kipato cha wananchi na kuimarika kiuchumi.   Akizungumza kwenye uzinduzi wa barabara katika maeneo huru ya uwekezaji Micheweni Aprili 23, 20204, ikiwa ni katika shamra shamra za maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano wa Tanzania Dk. Mwinyi alisema, Serikali ya awamu ya nane ya Mapinduzi Zanzibar imedhamiria kukiinua kisiwa cha Pemba kiuchumi, hivyo ipo haja kwa wananchi kunufaika na uwekezaji utakaokuwepo.   Dk. Mwinyi alieleza kuwa, kuna mambo mbali mbali yanayo

RC: SALAMA: KIONGOZI WA MFANO, AWAONESHA WENGI KUFIKIA NDOTO ZAO

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA @@@@ UNAPOZUNGUMZIA nafasi ya mkuu wa  mkoa mwanamke kwa Pemba, kamwe huwezi kuliacha jina la Salama Mbarouk Khatibu.   Salama hakumbukwi tu kwa nafasi hiyo, kwa wale wanaofuatilia historia yake, kwanza alianzia nafasi ya kuhudumu ukuu wa wilaya za Chake chake na Micheweni kwa nyakati tofauti.   Wapo wanaokumbuka ngarambe zake na jitihada zake za uongozi, wakati ule wa awamu wa saba, alipokuwa mkuu wa wilaya ya Chake chake kabla ya kuhamishiwa wilaya ya Micheweni. Kiongozi huyu mwanamke anachukuwa mfano wa mwanamke Hajar na Ibrahim, ambae nae bila ya kujali changamoto na maneno ya kukatishwa tamaa, aliutumika umma. Hajar, ambae alikuwa mwanamke jasiri, mwenye nia nzuri, aliyeihama nchi yake, ili aende akaishi kando ya nyumba ya Mungu katika ardhi, kame isiyo na maji wala manyasi ili amwabudu Muumba. HUYU HAPA MKUU WA MKOA KASKAZINI PEMBA Salama Mbaroku Khatib, nae ni kama mfano huo, ndivyopale anapoamuwa kutekeleza majukumu yake ya uongozi ndani ya mkoa wa Kaska